Katibu Tawala wa Wilaya ya Kiteto Ndg. Mufandii Msaghaa ameongoza Kikao cha Maandalizi ya Mapokezi ya Mwenge wa Uhuru 2025 kilichofanyika Mei 27,2025.
Kikao hicho ambacho kimefanyika katika Ukumbi wa Maktaba ya Wilaya na kuhudhuliwa na wadau mbalimbali, kililenga kupanga na kuratibu shughuli zote muhimu zitakazofanyika wakati wa mapokezi ya Mwenge wa Uhuru ikiwa ni pamoja na maandalizi ya miradi itakayozinduliwa, kufunguliwa au kuwekwa jiwe la msingi.
Mwenge wa Uhuru unatarajiwa kupokelewa Wilayani Kiteto Julai 13,2025 katika kijiji cha Ndedo ukitokea wilayani Simanjiro, na utakabidhiwa siku Julai 14,2025 kwa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu.
Kauli mbiu ya Mbio za Mwenge wa Uhuru ni "Jitokeze Kushirki Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025, kwa Amani na Utulivu"
Kibaya-Kiteto
Anwani ya Posta: P.o.Box 98, Kibaya-Kiteto
Simu ya Mezani: +255 027-2552099
Simu ya kiganjani:
Barua Pepe: ded@kitetodc.go.tz
Hakimiliki@2017 Halimashauri ya Kiteto.Haki zote zimehifadhiwa