• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe watumishi |
    • Malalamiko |
Kiteto District Council
Kiteto District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Teknolojia,Habari ,Mawasiliano na Mahusiano
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Uchimbaji Madini
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Ardhi na Maliasili
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • This page is under construction
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi mipya
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

SHULE 16 ZA MSINGI ZAKABIDHIWA MADAWATI 358

Imetumwa : March 22nd, 2024

Jumla ya madawati 358 yamegawiwa katika shule za msingi 16 wilayani Kiteto katika mpango mkakati wa kukabiliana na changamoto ya upungufu wa madawati katika shule za msingi.

Hafla hiyo ambayo ilihudhuriwa na viongozi mbali mbali wa Serikali na Chama, baadhi ya madiwani, Kaimu Mkurugenzi, Watumishi, wananchi pamoja na wanafunzi, imefanyika Machi 21, 2024 katika viwanja vya Shule ya Msingi Kaloleni ambapo Mgeni Rasmi alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Kiteto Mh. Remidius Mwema.

Akitoa taarifa ya hali ya upatikanaji wa madawati katika shule za msingi, Mkuu wa Idara ya Elimu ya Awali na Msingi Mwl. Papakinyi Kaai amesema kwamba, Halmashauri inahitaji jumla ya madawati 21,883 ya kukaliwa na wanafunzi watatu watatu, ila kwa sasa Halmashauri ina madawati 14,281 hivyo kuna upungufu wa madawati 14,281.

Aidha Mwl. Papakinyi amesema kwamba upungufu huo wa madawati unasababisha wanafunzi wengi kubanana kwenye dawati moja na katika baadhi ya shule wanafunzi wengine wanakaa chini darasani kwa kukosa madawati.

“Hali hii inasababisha kwa kiwango kikubwa kazi ya ufundishaji na ujifunzaji kuwa ngumu na matokeo yake wanafunzi wengi wa wilaya ya Kiteto hawafanyi vizuri katika maendeleo ya kitaaluma,” ameongeza Mwl. Papakinyi.

Ili kukabiliana na upungufu wa madawati, Wilaya ilikuja na mpango mkakati wa kukabiliana na changamoto ya upungufu wa madawati katika shule za msingi ambapo toka mpango huo uanze Novemba 2022, mpaka Machi 2024, jumla ya madawati 3,353 yamekwisha tengenezwa na kati ya hayo madawati 358 yamekadhiwa kwa shule 16 kwenye hafla hiyo.

Akiongea kabla ya kukabidhi madawati hayo, Mh. Mwema amewapongeza wadau wote na jamii kwa ujumla kwa kazi kubwa waliyoifanya kwa ajili ya kupatikana kwa madawati hayo.

Vilevile Mh. Mwema ameishukuru serikali ya Mh. Dkt Samia Suluhu Hassan kwa fedha ambazo wilaya inazipokea kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya ujenzi wa vyumba vya madarasa ambayo madawati pia yanatengenezwa kupitia miradi hiyo.

Aidha Mh. Mwema ameahidi kuendeleza kampeni ya upatikanaji wa madawati na aliwasihi wadau na wananchi kwa ujumla kuendelea kuhamasishana ili kuwezesha Halmashauri kumaliza kabisa changamoto ya upungufu wa madawati.

“Nitoe pongezi za dhati kwa jitihada za Idara ya Elimu ya Awali na Msingi katika kukabiliana na changamoto hii ya upungufu wa madawati ila niwaombe jitihada hizi ziende sambamba na kuongezeka kwa ufaulu” aliongeza Mh. Mwema.

Naye Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto, Mh. Abdalla Bundala, amewapongeza wote waliochangia kupatikana kwa madawati hayo.

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA 11.06.2025 June 11, 2025
  • TANGAZO NAFASI YA KAZI- MWENYEKITI BODI YA MFUKO WA ELIMU June 08, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI JUNI 2025 June 07, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 06, 2025
  • Angalia zote

Habari mpya

  • MAFUNZO YA MFUMO WA E-UTENDAJI KWA WATUMISHI.

    June 12, 2025
  • KIKAO CHA MAANDALIZI YA MWENGE WA UHURU 2025

    June 11, 2025
  • WATOTO WA UMISSETA KITETO, WAWATOA JASHO WATU WAZIMA!

    June 10, 2025
  • WALIMU KITETO WAPEWA MAFUNZO YA AFUA JUMUISHI ZA ELIMU YA AFYA SHULENI

    June 05, 2025
  • Angalia zote

Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.

MWENGE MAKABIDHIANO MKOA WA MANYARA 2018
Video Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Hati ya Mshahara

Viunganishi vya Tovuti Nyingine

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • MANYARA
  • NECTA
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Kibaya-Kiteto

    Anwani ya Posta: P.o.Box 98, Kibaya-Kiteto

    Simu ya Mezani: +255 027-2552099

    Simu ya kiganjani:

    Barua Pepe: ded@kitetodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki@2017 Halimashauri ya Kiteto.Haki zote zimehifadhiwa