Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto, Mhe. Athumani Kilimo, Februari 12, 2026, amekabidhi vyeti kwa shule za sekondari zilizofanya vizuri katika Matokeo ya Mtihani wa Taifa wa Kidato cha Nne na Mtihani wa Upimaji wa Kidato cha Pili mwaka 2025.
Akitoa taarifa ya matokeo hayo katika Kikao cha Baraza la Madiwani, Mkuu wa Idara ya Elimu Sekondari, Mwl. Ally Kichuri, alisema kuwa kwa miaka mitatu mfululizo ufaulu umeendelea kuongezeka na kufikia asilimia 97.8 mwaka 2025. Alieleza kuwa mwaka 2026 wataalamu wataongeza juhudi ili kuhakikisha ufaulu huo unaendelea kupanda na kufikia asilimia 100, kama ilivyokuwa kwa watahiniwa wa Kidato cha Sita.
Katika hafla hiyo, Mhe. Kilimo alikabidhi vyeti vya pongezi kwa makundi mawili ya shule. Kundi la kwanza lilihusisha shule zilizokidhi vigezo vya KPI, ambapo shule sita zilitunukiwa vyeti kwa matokeo ya Kidato cha Nne, huku Shule ya Sekondari Kiteto ikikidhi kigezo hicho katika mtihani wa Kidato cha Pili.
Kundi la pili lilihusisha shule zilizofaulisha kwa asilimia 100, bila mwanafunzi yeyote kupata daraja sifuri. Shule tisa zilitunukiwa vyeti katika kundi hili, ikiwa ni ongezeko ikilinganishwa na matokeo ya Kidato cha Nne mwaka 2024, ambapo shule sita pekee zilifikia kiwango hicho.
Viongozi wa Chama na Serikali waliwapongeza wataalamu wa Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji kwa usimamizi madhubuti wa sekta ya elimu, wakisisitiza kuwa mafanikio hayo ni matokeo ya juhudi za walimu, uongozi wa shule na ushirikiano wa jamii.
Utoaji wa vyeti mbele ya Baraza la Madiwani umeelezwa kuwa ni chachu ya kuongeza motisha kwa walimu na shule zote wilayani, huku ukiimarisha utamaduni wa ubora na ushindani chanya katika kuinua viwango vya ufaulu.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto, Mhe. Athumani Kilimo, Februari 12, 2026, amekabidhi vyeti kwa shule za sekondari zilizofanya vizuri katika Matokeo ya Mtihani wa Taifa wa Kidato cha Nne na Mtihani wa Upimaji wa Kidato cha Pili mwaka 2025.
Akitoa taarifa ya matokeo hayo katika Kikao cha Baraza la Madiwani, Mkuu wa Idara ya Elimu Sekondari, Mwl. Ally Kichuri, alisema kuwa kwa miaka mitatu mfululizo ufaulu umeendelea kuongezeka na kufikia asilimia 97.8 mwaka 2025. Alieleza kuwa mwaka 2026 wataalamu wataongeza juhudi ili kuhakikisha ufaulu huo unaendelea kupanda na kufikia asilimia 100, kama ilivyokuwa kwa watahiniwa wa Kidato cha Sita.
Katika hafla hiyo, Mhe. Kilimo alikabidhi vyeti vya pongezi kwa makundi mawili ya shule. Kundi la kwanza lilihusisha shule zilizokidhi vigezo vya KPI, ambapo shule sita zilitunukiwa vyeti kwa matokeo ya Kidato cha Nne, huku Shule ya Sekondari Kiteto ikikidhi kigezo hicho katika mtihani wa Kidato cha Pili.
Kundi la pili lilihusisha shule zilizofaulisha kwa asilimia 100, bila mwanafunzi yeyote kupata daraja sifuri. Shule tisa zilitunukiwa vyeti katika kundi hili, ikiwa ni ongezeko ikilinganishwa na matokeo ya Kidato cha Nne mwaka 2024, ambapo shule sita pekee zilifikia kiwango hicho.
Viongozi wa Chama na Serikali waliwapongeza wataalamu wa Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji kwa usimamizi madhubuti wa sekta ya elimu, wakisisitiza kuwa mafanikio hayo ni matokeo ya juhudi za walimu, uongozi wa shule na ushirikiano wa jamii.
Utoaji wa vyeti mbele ya Baraza la Madiwani umeelezwa kuwa ni chachu ya kuongeza motisha kwa walimu na shule zote wilayani, huku ukiimarisha utamaduni wa ubora na ushindani chanya katika kuinua viwango vya ufaulu.
Kibaya-Kiteto
Anwani ya Posta: P.o.Box 98, Kibaya-Kiteto
Simu ya Mezani: +255 027-2552099
Simu ya kiganjani:
Barua Pepe: ded@kitetodc.go.tz
Hakimiliki@2017 Halimashauri ya Kiteto.Haki zote zimehifadhiwa