• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe watumishi |
    • Malalamiko |
Kiteto District Council
Kiteto District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Teknolojia,Habari ,Mawasiliano na Mahusiano
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Uchimbaji Madini
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Ardhi na Maliasili
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • This page is under construction
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi mipya
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

BARAZA LA MADIWANI KITETO LAPITISHA BAJETI YA SHILINGI BILIONI 41.9 KWA MWAKA WA FEDHA 2026/2027

Imetumwa : January 27th, 2026

Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto, Januari 27, 2026, limepitisha bajeti ya Shilingi bilioni 41.9 kwa mwaka wa fedha 2026/2027, hatua inayolenga kuimarisha utekelezaji wa ajenda ya maendeleo ya kijamii na kiuchumi kwa wananchi wa wilaya hapa.

Akizungumza wakati wa kikao cha Baraza hilo, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto, Mhe. Athumani Hamisi Kilimo, alisema kuwa halmashauri inatarajia kukusanya, kupokea na kutumia jumla ya Shilingi 41,907,909,000, ambapo Shilingi 5,148,249,000 ni mapato ya ndani ya halmashauri.


Mhe. Kilimo alieleza kuwa halmashauri imetenga asilimia 40 ya mapato ya ndani kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo, akisisitiza kuwa mwelekeo wa bajeti hiyo unalenga kuongeza ustawi wa jamii na kuimarisha miundombinu katika sekta mbalimbali.


“Halmashauri imetenga asilimia 40 ya mapato ya ndani, ambapo fedha hizo zitaelekezwa katika utoaji wa mikopo kwa wanawake, vijana na watu wenye ulemavu, pamoja na utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika sekta ya kilimo, mifugo na maeneo mengine muhimu yanayogusa maisha ya wananchi moja kwa moja, ikiwemo sekta za elimu na afya,” aliongeza Mhe. Kilimo.


Katika hatua nyingine, Baraza hilo pia lilipitisha mipango na bajeti za taasisi nyingine za serikali zinazotoa huduma ndani ya Wilaya ya Kiteto, zikiwemo Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA), Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA), pamoja na Mamlaka ya Maji Mji wa Kibaya (KIUWASA).


Upitishwaji wa mipango na bajeti hizo ni ishara ya dhamira ya uongozi wa Wilaya ya Kiteto katika kusukuma mbele maendeleo, kuimarisha uwajibikaji wa kisiasa na kuhakikisha rasilimali za umma zinatumika kuboresha huduma za kijamii na kukuza fursa za kiuchumi kwa wananchi.

Kwa upande wao, Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto wameeleza imani yao kuwa bajeti ya mwaka wa fedha 2026/2027 itatekelezwa ipasavyo ili kukidhi mahitaji ya wananchi na kuboresha utoaji wa huduma bora.

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA MAPOKEZI YA FEDHA SEPTEMBA 2025 September 16, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU September 01, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI September 01, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI JUNI 2025 June 07, 2025
  • Angalia zote

Habari mpya

  • BARAZA LA MADIWANI KITETO LAPITISHA BAJETI YA SHILINGI BILIONI 41.9 KWA MWAKA WA FEDHA 2026/2027

    January 27, 2026
  • DC MWEMA AAGIZA USIMAMIZI MADHUBUTI WA SHERIA NA ULINZI WA MIUNDOMBINU YA SERIKALI

    January 26, 2026
  • WATENDAJI WILAYANI KITETO WAKUMBUSHWA KUONGEZA JUHUDI KATIKA UTEKELEZAJI WA AFUA ZA LISHE.

    January 14, 2026
  • KITETO YAJIPANGA KIKAMILIFU KUTEKELEZA BIMA YA AFYA KWA WOTE

    January 07, 2026
  • Angalia zote

Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.

MWENGE MAKABIDHIANO MKOA WA MANYARA 2018
Video Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Hati ya Mshahara

Viunganishi vya Tovuti Nyingine

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • MANYARA
  • NECTA
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Kibaya-Kiteto

    Anwani ya Posta: P.o.Box 98, Kibaya-Kiteto

    Simu ya Mezani: +255 027-2552099

    Simu ya kiganjani:

    Barua Pepe: ded@kitetodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki@2017 Halimashauri ya Kiteto.Haki zote zimehifadhiwa