• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe watumishi |
    • Malalamiko |
Kiteto District Council
Kiteto District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Teknolojia,Habari ,Mawasiliano na Mahusiano
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Uchimbaji Madini
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Ardhi na Maliasili
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • This page is under construction
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi mipya
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

KITETO YAJIPANGA KIKAMILIFU KUTEKELEZA BIMA YA AFYA KWA WOTE

Imetumwa : January 7th, 2026

Wilaya ya Kiteto imeanza rasmi maandalizi ya utekelezaji wa Mpango wa Bima ya Afya kwa Wote kufuatia kikao maalum cha Kamati ya Afya ya Msingi (PHC) ngazi ya Wilaya kilichofanyika Januari 06, 2026 Mjini Kibaya, kikilenga kutoa elimu ya awali na kujenga uelewa kwa wadau kuhusu mpango huo wa kitaifa.


Akizungumza katika kikao hicho, Mkuu wa Wilaya ya Kiteto na Mwenyekiti wa Kamati ya PHC, Mhe. Remidius Mwema, alisema kikao hicho ni mwanzo wa mchakato wa kuandaa jamii kabla ya kuanza kwa vikao maalum vya Tarafa zote saba kuanzia Januari 08, 2026, vitakavyofuatwa na mikutano ya wananchi katika ngazi ya vijiji.


Mhe. Mwema alisisitiza kuwa Mpango wa Bima ya Afya kwa Wote ni utekelezaji wa ahadi ya Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ndani ya siku 100, wenye lengo la kuhakikisha wananchi wote wanapata huduma bora za afya bila vikwazo na kwa gharama nafuu.


Kwa upande wake, Katibu Tawala wa Wilaya ya Kiteto, Ndg. Mufandii Msaghaa, alisema mpango huo ni dhamira ya dhati ya Serikali ya kuboresha upatikanaji wa huduma za afya, huku akiahidi kuwa viongozi wa Wilaya watahakikisha wananchi wanapata elimu sahihi na ya kina.

Naye Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto, Mhe. Athumani Kilimo, alibainisha kuwa uhamasishaji na uelewa wa wananchi ni nguzo muhimu ya mafanikio ya mpango huo, na kuwataka wajumbe wa Kamati hiyo wanafikisha elimu  hiyo kwa wananchi  kwa kuzingatia makundi na mazingira ya jamii husika.

Kikao hicho kilihusisha pia viongozi wa dini, vyama vya siasa, viongozi wa kimila pamoja na makundi maalum, hatua inayodhihirisha mshikamano wa kijamii na kisiasa katika kuhakikisha Bima ya Afya kwa Wote inakuwa agenda ya kila mwananchi Kiteto.

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA MAPOKEZI YA FEDHA SEPTEMBA 2025 September 16, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU September 01, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI September 01, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI JUNI 2025 June 07, 2025
  • Angalia zote

Habari mpya

  • KITETO YAJIPANGA KIKAMILIFU KUTEKELEZA BIMA YA AFYA KWA WOTE

    January 07, 2026
  • MRADI SHULE MPYA YA MSINGI KATA YA KALOLENI KUPUNGUZA ADHA YA WANAFUNZI KUTEMBEA UMBALI MREFU.

    December 30, 2025
  • HABARI PICHA:

    December 23, 2025
  • WANUFAIKA WA MIKOPO YA 10% WILAYANI KITETO WAASWA KUTUMIA MIKOPO HIYO KAMA FURSA KUJIKWAMUA KIUCHUMI.

    December 08, 2025
  • Angalia zote

Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.

MWENGE MAKABIDHIANO MKOA WA MANYARA 2018
Video Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Hati ya Mshahara

Viunganishi vya Tovuti Nyingine

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • MANYARA
  • NECTA
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Kibaya-Kiteto

    Anwani ya Posta: P.o.Box 98, Kibaya-Kiteto

    Simu ya Mezani: +255 027-2552099

    Simu ya kiganjani:

    Barua Pepe: ded@kitetodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki@2017 Halimashauri ya Kiteto.Haki zote zimehifadhiwa