• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe watumishi |
    • Malalamiko |
Kiteto District Council
Kiteto District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Teknolojia,Habari ,Mawasiliano na Mahusiano
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Uchimbaji Madini
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Ardhi na Maliasili
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • This page is under construction
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi mipya
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

DC Magessa Awataka Madiwani Kuwa Mfano Katika Uanzishaji wa Viwanda Wilayani Kiteto.

Imetumwa : February 23rd, 2018


Mwenyekiti wa Kikao cha DCC Mhe. Tumaini Magessa akiendesha kikao cha DCC  kilichofanyika katika ukumbi wa halmashauri ya wilaya ya Kiteto.

Mwenyekiti wa Kikao cha DCC Mhe. Tumaini Magessa (wa kwanza kushoto) ,Katibu wa kikao Ndg .Tamim Kambona (wa pili kutoka kushoto),katibu tawala (W) Kiteto Ndg. Stephano Ndaki(wa pili kulia)  na katibu wa CCM (W) Kiteto Ndg. Shekue Pashua ( wa kwanza kulia) wakifuatilia kwa makini mwenendo wa kikao cha DCC kilichofanyika katika ukumbi wa halmashauri ya wilaya ya Kiteto


Katibu wa Kikao cha DCC Ndg. Tamim Kambona  akifunga kikao hicho  kilichofanyika katika ukumbi wa halmashauri ya wilaya ya Kiteto


Mwenyekiti wa Halmashauri (W) Kiteto Mhe. Lairumbe Mollel  (wa kwanza kulia) ,Mwenyekiti wa CCM (W) Kiteto Ndg. Mohamed Kiondo ( wa katikati)  na  Makamu mwenyekiti wa halmashauri (W) Kiteto Mhe. Hassan Benzi ( wa kwanza kushoto) wakiwa kwenye  kikao cha DCC kilichofanyika katika ukumbi wa halmashauri ya wilaya ya Kiteto


Meneja wa TRA Wilaya ya Kiteto   Akiwasilisha taarifa ya taasisi yake wakati wa kikao cha DCC kilichofanyika katika ukumbi wa halmashauri .

Meneja wa TFS Wilaya ya Kiteto  Akiwasilisha taarifa ya taasisi yake wakati wa kikao cha DCC kilichofanyika katika ukumbi wa halmashauri .

Meneja wa TANESCO  Wilaya ya Kiteto  Akiwasilisha taarifa ya taasisi yake wakati wa kikao cha DCC kilichofanyika katika ukumbi wa halmashauri .





Wajumbe wa DCC wakiwa kwenye  kikao cha DCC kilichofanyika katika ukumbi wa halmashauri ya wilaya ya Kiteto.


Wajumbe wa DCC wakishauri kuhusiana na masuala mbalimbali  ya maendeleo ya wilaya  ya kiteto wakati wa kikao cha DCC kilichofanyika katika  ukumbi wa halmashauri .



..................HABARI KAMILI..........................

DC  Magessa Awataka Madiwani  Kuwa Mfano Katika Uanzishaji wa Viwanda Wilayani Kiteto.


Mkuu wa wilaya ya Kiteto mheshimiwa Tumaini Magessa amewataka waheshimiwa madiwani wa halmashauri ya wilaya ya Kiteto kuwa viongozi wa mfano kwa kutekeleza kauli mbiu ya Mhe Rais Magufuli ya Tanzania ya viwanda,kwa kuanzisha  viwanda.Mheshimiwa Magessa ameyasema hayo wakati akifungua kikao cha Kamati ya ushauri ya wilaya (DCC)  kilichofanyika katika ukumbi wa halmashauri ya wilaya ya Kiteto.

Akizungumza katika kikao hicho Mhe. Magessa amesema kwamba wilaya ya Kiteto inatakiwa kuanzisha viwanda vipya 15 ,lakini hadi sasa viwanda ambavyo vimekwisha kuanzishwa ni viwanda viwili tu . Mhe. Magessa amesema kwamba kuwa kiongozi ni kuonyesha mfano ,hivyo Wahe. Madiwani wanapaswa kuwa wa kwanza  kuanzisha viwanda.Akisisitiza kuhusu kauli yake hiyo Mhe.Magessa  anasema ‘‘Nilitegemea kusikia madiwani wameanza kukusanya fedha za kuanzisha viwanda.Sasa sisikii, sijui labda inabidi DC ndio nianzishe .Sijasikia diwani hata mmoja anasema mimi pale kwangu naanzisha cha kusaga mahindi.Naona kimya tu’’.Aidha  Mhe. Magessa amewataka wajumbe wa DCC kama washauri katika masuala mbalimbali wilayani kuwahamasisha wananchi kuanzisha viwanda vidogo vidogo kwani anavyoiona wilaya ya Kiteto anaamini kwamba upo uwezekano wa kuwa na viwanda zaidi ya 20.
 
Kikao  hicho cha DCC kilikuwa na agenda 11 ikiwemo taarifa ya mwenendo wa utekelezaji wa bajeti ya mwaka 2017/2018.Mpango wa bajeti wa halmashauri kwa mwaka 2018/2019,ambapo bajeti iliwasilishwa ,wajumbe walitoa ushauri katika  baadhi ya vipengele vya bajeti hiyo na hatimaye kuiridhia bajeti hiyo.

Ukusanyaji mapato  na ulipaji kodi TRA  ni ajenda nyingine muhimu ya kikao hicho, mwenyekiti aliwataka wajumbe wote kutoa ushauri utakaowezesha kuongezeka kwa ukusanywaji mapato ya halmashauri na kodi inayolipwa  TRA.Wajumbe walibainisha vyanzo vingine vya mapato  na kushauri ufuatiliaji ufanyike ili serikali kuu na halmashauri iweze kupata mapato  kupitia vyanzo hivyo.
Migogoro ya ardhi iliyopo wilayani  Kiteto na hatua mbalimbali zinazoendelea kuchukuliwa na uongozi wa wilaya , ni ajenda njingine ya kikao hicho ambapo mwenyekiti wa kikao  aliwaeleza wajumbe wakikao hicho kuhusu mikakati mbalimbali ambayo uongozi wa wilaya umeiweka ili kumaliza migogoro wilayani Kiteto , vilevile wajumbe wa kikao walizungumzia  kuhusiana na migogoro hiyo na kushauri juu ya nini kifanyike katika kutokomeza migogoro hiyo.

Agenda nyingine ni utunzaji wa mazingira na marufuku ya ukataji miti na uvunaji ovyo wa mazao ya misitu. Akiwasilisha ajenda hiyo Katibu Tawala wa wilaya ya Kiteto ndugu Stephano Ndaki amesema kwamba mipango ya matumizi bora ya ardhi ipo,hakuna mwananchi asiyejua kwamba katika kijiji chake eneo la malisho ni lipi,eneo la makazi ni lipi na eneo la kilimo ni lipi.Hivyo ni vema wananchi wakazingatia mipango ya matumizi bora ya ardhi iliyopo.Na iwapo kuna haja ya kufanya mapitio ili kufanya marekebisho katika mipango hiyo ,mapitio yatafanywa baada ya wao kuzingatia mipango iliyopo.Na kwamba kuheshimu matumizi bora ya ardhi yaliyopangwa  ndio njia pekee ya kumaliza migogoro.

Katika hatua nyingine  ndugu Ndaki amegongelea msumari agizo la RC wa Manyara la kuwekwa kwa adhabu kali  kwa wafugaji watakaochungia katika mashamba ya wakulima,ambapo wafugaji hao watalazimika kulipa fidia itakayokuwa imetokana na tathmini ya uharibifu wa mazao .Pamoja na kulipa fidia ya uharibifu wa mazao, adhabu ya faini itatozwa kwa kila ng’ombe aliyeingia kwenye shamba na kufanya uharibifu huo.Kadhalika kwa wakulima watakao vamia na kulima maeneo ambayo sio kwa ajili ya matumizi ya mashamba watapewa adhabu ya kuotesha miti kulingana na idadi ya miti waliyokata katika mashamba hayo baada ya afisa misitu kufanya tathmini ya miti iliyokatwa.Pia ndugu Ndaki  amepiga marufuku uanzishwaji wa vitongoji visivyo rasmi ,ambapo amesema kwamba vitongoji hivyo vinaanzishwa bila utaratibu, vinaanzishwa katika maeneo ambayo sio ya makazi , jambo ambalo linasababisha uharibifu wa mazingira na kuchochea migogoro ya ardhi.

Kikao cha kamati ya ushauri ya wilaya hufanyika kila baada ya miezi mitatu .Dhima ya kikao hicho ni kushauri katika masuala mbalimbali yanayohusu wilaya ikiwemo upatikanaji wa mapato na matumizi ya halmashauri .


.........................MWISHO.................................

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA 11.06.2025 June 11, 2025
  • TANGAZO NAFASI YA KAZI- MWENYEKITI BODI YA MFUKO WA ELIMU June 08, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI JUNI 2025 June 07, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 06, 2025
  • Angalia zote

Habari mpya

  • HAYAWI HAYAWI SASA YAMEKUA: HATIMAYE KALOLENI YAPATA SHULE MPYA YA MSINGI

    July 30, 2025
  • SHULE YA MSINGI KINANGALI NAYO YANUFAIKA NA MRADI WA BOOST

    July 30, 2025
  • SERIKALI YA AWAMU YA SITA YAENDELEA KUWEKEZA KWA VITENDO: KURASH YAPATA MRADI MWINGINE WA MILIONI 153 KUPITIA BOOST

    July 30, 2025
  • KATA YA BWAWANI YAPATA MRADI WA SHULE MPYA YA ELIMU MSINGI.

    July 28, 2025
  • Angalia zote

Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.

MWENGE MAKABIDHIANO MKOA WA MANYARA 2018
Video Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Hati ya Mshahara

Viunganishi vya Tovuti Nyingine

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • MANYARA
  • NECTA
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Kibaya-Kiteto

    Anwani ya Posta: P.o.Box 98, Kibaya-Kiteto

    Simu ya Mezani: +255 027-2552099

    Simu ya kiganjani:

    Barua Pepe: ded@kitetodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki@2017 Halimashauri ya Kiteto.Haki zote zimehifadhiwa