• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe watumishi |
    • Malalamiko |
Kiteto District Council
Kiteto District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Teknolojia,Habari ,Mawasiliano na Mahusiano
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Uchimbaji Madini
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Ardhi na Maliasili
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • This page is under construction
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi mipya
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

DC Magessa Atoa Somo kwa Wafanyakazi Kiteto

Imetumwa : May 1st, 2018

Mgeni rasmi ,ambaye pia ni mkuu wa wilaya Mhe. Tumaini Magessa  akihutubia  wafanyakazi   katika  maadhimisho ya siku ya wafanyakazi duniani  wilayani Kiteto  . Maadhimisho hayo  yamefanyika  ndani ya uwanja wa halmashauri uliopo  karibu na kituo kikuu cha mabasi  - Kibaya .

Wafayakazi  kutoka taasisi mbalimbali wilayani Kiteto  wakiandamana kusheherekea maadhimisho ya siku  ya wafanyakazi duniani  ( Mei Mosi) . 


Mgeni rasmi  ambaye ni mkuu wa wilaya ya Kiteto Mhe. Tumaini Magessa  akipokea maandamano ya wafanyakazi  katika  maadhimisho ya siku ya wafanyakazi duniani ( Mei Mosi) . 

Wafayakazi  kutoka taasisi mbalimbali wilayani Kiteto pamoja na meza kuu wakiimba wimbo wa mshikamano katika maadhimisho ya  siku ya wafanyakazi duniani ( Mei Mosi) . 


Wafayakazi wakimsikilza mgeni rasmi mkuu wa wilaya ya Kiteto Mhe. Tumaini Magessa wakati akihutubia katika maadhimisho ya  siku  ya wafanyakazi duniani ( Mei Mosi) . 

Mwl. Rehema Sudi akisoma risala ya wafanyakazi kwa mgeni rasmi mkuu wa wilaya ya Kiteto Mhe. Tumaini Magessa katika maadhimisho ya siku  ya wafanyakazi duniani ( Mei Mosi) . Aliyesimama pembeni yake ni Mama Lymo, mtumishi katika ofisi ya DC.


...................HABARI KAMILI....................



Mgeni rasmi katika maadhimisho ya  siku ya wafanyakazi duniani ( Meimosi)  wilayani Kiteto ambaye pia ni mkuu wa wilaya ya Kiteto, mheshimiwa Tumaini Magessa amewataka watumishi kujiwekea akiba  ili waweze kujiendeleza kimaisha  kabla ya kustaafu.Mhe. Magessa ameyasema hayo  wakati akiwatubia wafanyakazi  wa taasisi mbalimbali wilayani Kiteto katika maadhimisho hayo , ambapo kiwilaya yamefanyika katika uwanja wa halmashauri, uliopo  jirani na kituo kikuu cha mabasi Kibaya .


Akizungumza  na wafanyakazi  wakati wa  hotoba yake Mhe. Magessa amesema wafanyakazi waweke akiba wakati wakiwa kazini , kwani  kutokuweka akiba , na kuwa na mawazo ya kutegemea pesa ya kiinua mgongo kuna madhara.Akisisitiza juu ya umuhimu wa wafanyakazi kuweka akiba Mhe. Magessa amesema “Tunategemea muweke akiba sasa, ukianza kuweka  akiba sasa,kama una miaka 30 , baada ya miaka 20,utakuwa na miaka 50, akiba hiyo itakusaidia, utaweza kujenga kibanda chako.Lakini ukisema  unasubiri kiinua mgongo ndipo ujenge nyumba, utakufa mwaka unaofuata, kwa sababu utakapojenga nyumba pesa yote  itakwisha halafu baadae itakuwaje? Na wewe ulizoea kunywa chai asubuhi, kula chakula mchana  na jioni. Sasa kwenye uzee utabadilisha maisha, utakuwa unakunywa chai,unakula mara moja usiku. Maana yake nini? Umekiita kifo mwenyewe. Pesa yote umeweka kwenye nyumba, na kifo kina kufuata sasa”.


Aidha Mhe Magessa amesema kwamba wafanyakazi waweke  akiba  katika umri walionao, kwani maandalizi ya kustaafu yanapaswa  kuanzia katika maisha waliyonayo sasa.Ili wakati wa uzee usiwe ni wakati wa kujenga au kupanga kufanya miradi.  Kwani kwa kufanya hivyo maisha ya uzee yatakuwa magumu sana, hali ya kuwa wametumia muda wao mwingi katika utumishi, wataona kama vile kiinua mgongo hakikuwasaidia chochote kutokana na kutokuweka mipango  mapema  ya namna ya kuishi baada ya kustaafu.


Maadhimisho hayo ya siku ya wafanyakazi duniani ( Meimosi) yalianza kwa maandamano ya wafanyakazi  ambayo yalianzia katika ofisi za halmashauri ya wilaya ya Kiteto ( Bomani)  na kupokelewa na mgeni rasmi ( Mhe. Tumaini Magessa) uwanjani.Kadhalika Sherehe hizo zilipambwa na  burudani mbalimbali kama muziki, mashairi na tenzi  pamoja na michezo kama vile  sarakasi ,mashindano ya kukimbiza kuku ,mashindano ya kukimbia  ndani ya magunia,kuvuta kamba  na kukuna nazi.



.....................MWISHO......................


Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA 11.06.2025 June 11, 2025
  • TANGAZO NAFASI YA KAZI- MWENYEKITI BODI YA MFUKO WA ELIMU June 08, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI JUNI 2025 June 07, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 06, 2025
  • Angalia zote

Habari mpya

  • HAYAWI HAYAWI SASA YAMEKUA: HATIMAYE KALOLENI YAPATA SHULE MPYA YA MSINGI

    July 30, 2025
  • SHULE YA MSINGI KINANGALI NAYO YANUFAIKA NA MRADI WA BOOST

    July 30, 2025
  • SERIKALI YA AWAMU YA SITA YAENDELEA KUWEKEZA KWA VITENDO: KURASH YAPATA MRADI MWINGINE WA MILIONI 153 KUPITIA BOOST

    July 30, 2025
  • KATA YA BWAWANI YAPATA MRADI WA SHULE MPYA YA ELIMU MSINGI.

    July 28, 2025
  • Angalia zote

Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.

MWENGE MAKABIDHIANO MKOA WA MANYARA 2018
Video Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Hati ya Mshahara

Viunganishi vya Tovuti Nyingine

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • MANYARA
  • NECTA
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Kibaya-Kiteto

    Anwani ya Posta: P.o.Box 98, Kibaya-Kiteto

    Simu ya Mezani: +255 027-2552099

    Simu ya kiganjani:

    Barua Pepe: ded@kitetodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki@2017 Halimashauri ya Kiteto.Haki zote zimehifadhiwa