• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe watumishi |
    • Malalamiko |
Kiteto District Council
Kiteto District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Teknolojia,Habari ,Mawasiliano na Mahusiano
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Uchimbaji Madini
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Ardhi na Maliasili
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • This page is under construction
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi mipya
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

DC Awataka Madiwani Kudhibiti Utoroshwaji wa Mazao Kiteto

Imetumwa : July 2nd, 2018

Mkuu wa wilaya ya Kiteto Mhe. Tumaini Magessa akitoa maelekezo ya serikali katika kikao cha baraza la madiwani  kilichofanyika katika ukumbi wa halmashauri.

Diwani wa kata ya Sunya Mhe. Mussa Brighton akiwasilisha taarifa ya kamati  yake katika kikao cha baraza la madiwani la halmashauri ya wilaya ya Kiteto.

                                         Kikao cha baraza la madiwani la halmashauri ya wilaya ya Kiteto kikiendelea.



..........HABARI KAMILI...........



Mkuu wa wilaya ya Kiteto Mheshimiwa Tumaini Magessa  amewataka Waheshimiwa madiwani  kushirikiana kuimarisha ulinzi katika maeneo yao ili  kudhibiti utoroshwaji wa mazao unaotokea wakati wa mavuno, hali inayosababisha Halmashauri kupoteza mapato. Mhe.  Magessa ameyasema hayo wakati  alipokuwa akitoa maelekezo ya serikali  katika kikao cha baraza la madiwani la Halmashauri ya  wilaya ya Kiteto.

Akizungumza wakati akitoa maelekezo hayo Mhe. Magessa amesema “Njia zinazopitishwa mazao zinajulikana,Kila diwani akisimama imara tutapata taarifa sahihi kuhusu mazao yanayosafirishwa.”

Mheshimiwa magessa amesema kwamba wakidhibiti vizuri, sulala la utoroshaji mazao lisipokuwepo watamsaidia Mkurugenzi , ambapo ataweza kujenga shule, kujenga zahanati na kufanya shughuli nyingine nyingi za maendeleo .

Akisisitiza kuhusu madhara ya halmashauri kukosa mapato Mhe. Magessa amesema “Kama hakuna pesa hapa itakuwa shida sana hapa,itakuwa ni ugomvi Jumatatu hadi Jumatatu.Halmshauri yetu inalindwa na mazao,tusiruhusu mazao yapite”.

Katika hatua nyingine Mhe Magessa amezungumzia masuala mbalimbali likiwemo maonyesho ya kilimo maarufu kama Nanenane  na ujio wa mwenge wa uhuru na viwanda, ambapo katika suala la maonyesho ya Nanenane amewataka Wahe. madiwani kuhakikisha kwamba kila kata inatoa watu kwenda kwenye maonyesho, na sio tu kwenda kushiriki, bali wawe na vitu vya kwenda kuonyesha kwa lengo la kushindana.

Katika suala la ujio wa mwenge wa Uhuru , Mhe. Magessa amesisitiza kuhusu ushiriki wa wana Kiteto,ambapo amesema kwamba kila  mtu ashiriki katika kufanya maandalizi ya mwenge kwani mwenge  unaleta uhalisia wa nembo ya Taifa.

Aidha katika suala la viwanda  Mheshimiwa Magessa amewataka madiwani kuhakikikisha kwamba kila mmoja katika kata yake  kunakuwa na kiwanda kipya.

Katika kikao hicho  ajenda mbalimbali zimejadiliwa ikiwa ni pamoja na kusoma na kuthibitisha muktasari wa kikao kilichopita sambamba  na kupokea na kujadili taarifa za kamati za kudumu.



....................MWISHO.....................

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA 11.06.2025 June 11, 2025
  • TANGAZO NAFASI YA KAZI- MWENYEKITI BODI YA MFUKO WA ELIMU June 08, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI JUNI 2025 June 07, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 06, 2025
  • Angalia zote

Habari mpya

  • MAFUNZO YA MFUMO WA E-UTENDAJI KWA WATUMISHI.

    June 12, 2025
  • KIKAO CHA MAANDALIZI YA MWENGE WA UHURU 2025

    June 11, 2025
  • WATOTO WA UMISSETA KITETO, WAWATOA JASHO WATU WAZIMA!

    June 10, 2025
  • WALIMU KITETO WAPEWA MAFUNZO YA AFUA JUMUISHI ZA ELIMU YA AFYA SHULENI

    June 05, 2025
  • Angalia zote

Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.

MWENGE MAKABIDHIANO MKOA WA MANYARA 2018
Video Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Hati ya Mshahara

Viunganishi vya Tovuti Nyingine

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • MANYARA
  • NECTA
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Kibaya-Kiteto

    Anwani ya Posta: P.o.Box 98, Kibaya-Kiteto

    Simu ya Mezani: +255 027-2552099

    Simu ya kiganjani:

    Barua Pepe: ded@kitetodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki@2017 Halimashauri ya Kiteto.Haki zote zimehifadhiwa