• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe watumishi |
    • Malalamiko |
Kiteto District Council
Kiteto District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Teknolojia,Habari ,Mawasiliano na Mahusiano
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Uchimbaji Madini
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Ardhi na Maliasili
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • This page is under construction
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi mipya
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Wananchi Watakiwa Kufuata Utaratibu Katika Uvunaji wa Mazao ya Misitu

Imetumwa : July 4th, 2018

Mkuu wa wilaya ya Kiteto Mhe. Tumaini Magessa akitoa maelekezo kuhusu uvunaji wa mazao ya misitu katika kikao cha baraza la madiwani la halmashauri ya wilaya ya kiteto



............HABARI KAMILI............



Mkuu wa wilaya ya Kiteto Mheshimiwa Tumaini Magessa amewataka wakazi wa wilaya hiyo pamoja na wageni wote wanaoingia wilayani humo kwa lengo la uvunaji wa mazao ya misitu  kufuata utaratibu katika uvunaji huo ili kuwezesha utunzaji mazingira endelevu .Mhe. Magessa  ameyasema hayo wakati akizungumza katika baraza la madiwani la Halmashauri ya wilaya ya Kiteto mwishoni mwa mwezi juni 2018.


Akielekeza  kuhusu utaratibu wa uvunaji mazao ya misitu Mhe. Magessa amesema” mtu yeyote atavuna mazao ya misitu baada ya kupata kibali  na leseni  kutoka kwa kamati ya uvunaji.Kamati ya uvunaji  iko wazi kupokea maombi ya uvunaji .Baada ya kupokea maombi ,kamati itakaa, baada ya kikao tutaidhinisha  nani wamepewa vibali  vya uvunaji, na afisa misitu wa wilaya anazo leseni za kuwapatia watu hao”.


Mhe. Magessa amesema kwamba waraka wa mkuu wa mkoa wa Manyara unaelekeza kwamba ili mtu aweze kuvuna mti mmoja anatakiwa awe amepanda miti kumi na imeota,lakini vijiji havionyeshi  mahali pa kupanda miti ,isipokuwa vinaonyesha mahali pa  kuvuna tu.


Aidha Mhe. Magessa amesema kwamba wananchi wana haki ya kuvuna mazao  ya misitu,  lakini wanatakiwa kufuata utaratibu na mwongozo wa serikali. Akisisitiza kuhusu kauli yake hiyo Mhe. Magessa amesema” Kuna watu wanatembea na bendera huko mitaani wanasema tumezuia uvunaji wa mkaa,hatujazuia uvunaji,tunataka  watu wafuate utaratibu”.


Mhe. Magessa pia ameeleza kuhusu madhara ya kutokuwa na utunzaji wa mazingira endelevu,  Mhe. Magessa amesema“Tusipoheshimu mazingira leo,tukaanza kuweka mikakati ya kuyafanya mazingira yetu yaendelee kuwa endelevu, tutaadhibiwa kesho.Watu walime,watu wafuge, lakini mazingira yetu yaendelee kuwa salama.Tukifika hapo tunaweza kufanikiwa bila wasi wasi”.


Wilaya ya Kiteto imekuwa katika tishio la kuwa jangwa baada ya uvunaji miti holela ambao umekuwa ukifanywa na watu kwa malengo mbalimbali.Hata hivyo mwanzoni mwa mwaka huu 2018 Mkuu wa mkoa wa Manyara Mhe. Alexander Mnyeti alitoa waraka unaoelekeza utaratibu  utakaotumika katika uvunaji wa mazao ya misitu.



............MWISHO..............

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA 11.06.2025 June 11, 2025
  • TANGAZO NAFASI YA KAZI- MWENYEKITI BODI YA MFUKO WA ELIMU June 08, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI JUNI 2025 June 07, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 06, 2025
  • Angalia zote

Habari mpya

  • MAFUNZO YA MFUMO WA E-UTENDAJI KWA WATUMISHI.

    June 12, 2025
  • KIKAO CHA MAANDALIZI YA MWENGE WA UHURU 2025

    June 11, 2025
  • WATOTO WA UMISSETA KITETO, WAWATOA JASHO WATU WAZIMA!

    June 10, 2025
  • WALIMU KITETO WAPEWA MAFUNZO YA AFUA JUMUISHI ZA ELIMU YA AFYA SHULENI

    June 05, 2025
  • Angalia zote

Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.

MWENGE MAKABIDHIANO MKOA WA MANYARA 2018
Video Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Hati ya Mshahara

Viunganishi vya Tovuti Nyingine

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • MANYARA
  • NECTA
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Kibaya-Kiteto

    Anwani ya Posta: P.o.Box 98, Kibaya-Kiteto

    Simu ya Mezani: +255 027-2552099

    Simu ya kiganjani:

    Barua Pepe: ded@kitetodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki@2017 Halimashauri ya Kiteto.Haki zote zimehifadhiwa