• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe watumishi |
    • Malalamiko |
Kiteto District Council
Kiteto District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Teknolojia,Habari ,Mawasiliano na Mahusiano
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Uchimbaji Madini
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Ardhi na Maliasili
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • This page is under construction
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi mipya
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

“Madiwani Tembeleeni Maeneo Yenu ” DC Kiteto

Imetumwa : November 2nd, 2018

Mkuu wa wilaya ya Kiteto Mhe. Tumaini Magessa akitoa maelekezo ya serikali ,katika siku ya pili ya  kikao cha baraza la madiwani Oktoba 31,2018, ndani ya ukumbi wa halmashauri .Waliokaa pembeni yake , upande wake wa kulia ni Mbunge wa jimbo la Kiteto Mhe. Emmanuel Papian, na upande wake wa kushoto ni Makamu mwenyekiti wa Halmashauri Mhe. Hassan Benzi.


.......... HABARI KAMILI.......



Mkuu wa wilaya ya Kiteto Mheshimiwa Tumaini Magessa amewataka Waheshimiwa madiwani  kuonyesha uwajibikaji kwa wananchi wao kwa kutembelea maeneo yao kukagua shughuli za maendeleo, kuhimiza maendeleo na kutatua matatizo mbalimbali yanayowakabili wananchi.Mheshimiwa Magessa ameyasema hayo Oktoba 31,2018 ,wakati akitoa maelekezo ya serikali katika kikao cha baraza la madiwani la Halmashauri ya wilaya ya Kiteto, kilichofanyika katika ukumbi wa Halmashauri .

Akizungumza wakati akitoa maelekezo hayo Mheshimiwa Magessa amesema ‘‘Madiwani wengi hamuendi kwenye maeneo yenu, madiwani  mnatakiwa kwenda kwenye kata zenu ili muweze kufuatilia maendeleo ya wananchi , kama hamfanyi hivyo , uwajibikaji wenu unakuwa haupo, kwa sababu  ninyi ni madiwani wa wananchi,maana yake mnatakiwa kujua matatizo ya wananchi,mnatakiwa kujua maendeleo ya wananchi , tembeleeni maeneo yenu , zungumzeni na wananchi, kafanyeni kazi ya kutatua matatizo ya wananchi”.

Mheshimiwa Magessa amesema kwamba wananchi wakiwaona madiwani wao mara kwa mara ,wanakuwa na uhakika kwamba mambo yatakwenda vizuri. Wasipofanya hivyo, wananchi wataondoa imani kwao na watawakataa. Akisisitiza kuhusu hilo Mheshimiwa Magessa amesema “ Isifike wakati wa uchaguzi ukasema kwamba DC ndiye ameliondoa jina langu, mimi huwa natembea sana, kwa hiyo kama diwani hafiki kwenye eneo lake, mimi najua kwamba hafiki, maana wananchi wananiambia huyu bwana hafiki, ndio leo umekuja nae.Tufike tuhimize elimu, tuzungumze na kukemea kuhusu tatizo la mimba za utotoni”.

Aidha mheshimiwa Magessa amewataka waheshimiwa madiwani kuwa na mienendo mizuri,ili kwamba wanapokemea vitendo viovu wao wawe wasafi. Amesema kwamba ili mtu aweze kuhimiza jamii kutenda matendo mema, ni lazima  yeye mwenyewe mwema .Asiwaambie watu fuateni maneno yangu,msifuate matendo yangu,ni lazima huyo mtu awe na matendo mema, ili wale anaowaelekeza kutenda mema waige mfano kutoka kwake. Hivyo wao kama madiwani wasiwe kama sehemu ya kuweka miiba katika maeneo yao. Ili wawe viongozi wazuri lazima maneno yao yaendane na matendo yao.

Katika hatua nyingine  mheshimiwa Magessa amewataka waheshimiwa madiwani kuhimiza kuhusu suala la elimu, kwamba asiwepo mtoto asiyekwenda shule kwa kisingizio chochote,  wafuatilie kuhusu ufundishaji , kiwango cha ufaulu kiendelee kuongezeka.Kuwahimiza wazazi kuchangia chakula shuleni kwa ajili ya wanafunzi kupata chakula cha mchana , waweze kusoma vizuri, lakini pia amesisitiza kwamba waheshimiwa Madiwani wawaelimishe wazazi na walezi kuhusu chakula wanachopeleka shule, kwamba wapeleke chakula chenye ubora kinachofaa kwa matumizi ya binadamu. Kisiwe chakula ambacho kimewekwa dawa za kuua wadudu (viuatilifu)  ndani ya muda mfupi ili kuepuka madhara yanayoweza kuwapata wanafunzi kutokana na kula vyakula vibovu ama vyenye kemikali za kuua wadudu.

Kuchangia chakula shuleni ni moja wapo ya mikakati ya wilaya ya Kiteto katika kuinua taaluma na kiwango cha ufaulu kiwilaya. Na kwa kiasi kikubwa wazazi wamehamasika, japo kuna changamoto za hapa na pale ambazo viongozi wa wilaya kwa kushirikiana na madiwani ambao ndio wawakilishi wa wananchi wamekuwa wakizitatua  .




.........MWISHO............

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA 11.06.2025 June 11, 2025
  • TANGAZO NAFASI YA KAZI- MWENYEKITI BODI YA MFUKO WA ELIMU June 08, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI JUNI 2025 June 07, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 06, 2025
  • Angalia zote

Habari mpya

  • HAYAWI HAYAWI SASA YAMEKUA: HATIMAYE KALOLENI YAPATA SHULE MPYA YA MSINGI

    July 30, 2025
  • SHULE YA MSINGI KINANGALI NAYO YANUFAIKA NA MRADI WA BOOST

    July 30, 2025
  • SERIKALI YA AWAMU YA SITA YAENDELEA KUWEKEZA KWA VITENDO: KURASH YAPATA MRADI MWINGINE WA MILIONI 153 KUPITIA BOOST

    July 30, 2025
  • KATA YA BWAWANI YAPATA MRADI WA SHULE MPYA YA ELIMU MSINGI.

    July 28, 2025
  • Angalia zote

Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.

MWENGE MAKABIDHIANO MKOA WA MANYARA 2018
Video Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Hati ya Mshahara

Viunganishi vya Tovuti Nyingine

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • MANYARA
  • NECTA
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Kibaya-Kiteto

    Anwani ya Posta: P.o.Box 98, Kibaya-Kiteto

    Simu ya Mezani: +255 027-2552099

    Simu ya kiganjani:

    Barua Pepe: ded@kitetodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki@2017 Halimashauri ya Kiteto.Haki zote zimehifadhiwa