• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe watumishi |
    • Malalamiko |
Kiteto District Council
Kiteto District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Teknolojia,Habari ,Mawasiliano na Mahusiano
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Uchimbaji Madini
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Ardhi na Maliasili
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • This page is under construction
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi mipya
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

DC AZINDUA BODI YA HUDUMA YA AFYA WILAYA

Imetumwa : February 7th, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Kiteto, Mh Remidius Mwema Emmauel, amezindua Bodi ya Huduma ya Afya ya Wilaya ambayo moja ya majukumu yake ni kuhakikisha jamii inapata huduma bora za Afya inazozimudu na zinazoimarisha Afya zao.

Uzinduzi huo mbali na kuhudhuriwa na wadau mbalimbali,  pia ulihudhuriwa na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Kiteto Ndugu Abdala Bundala, Makamo Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya  Ndugu Hassan Benzi, Mkurugenzi Mtendaji (W) CPA. Hawa Abdul Hassan pamoja na Katibu Tawala wa Wilaya, Bi Mufandii Msaghaa,  umefanyika Februari 7,2024 katika Ukumbi wa  Maktaba ya Wilaya.

Akiongea katika uzinduzi huo, Mgeni Rasmi, Mh Mwema alisema kwamba serikali ina matumaini makubwa kutoka kwenye bodi hiyo na pia bodi hiyo inahesabu ya kutoa baada ya miaka mitatu .

“Kuna changamoto ya muingiliano wa majukumu hivyo ni vyema wajumbe hawa wa bodi wakapewa semina  ili wafahamu vizuri majukumu yao” alisema Mh. Mwema.

Aidha Mh Mwema aliwasihi wajumbe hao  wa bodi kufanya kazi kwa kushirikiana na kutimiza wajibu wao kwa uadilifu  pasipo kutanguliza maslahi yao binafsi.

“Kazi ya Bodi ni kuangalia huduma ya afya inaendaje, ni vyema mkasome muongozo vizuri,  tunaamini mtatuvusha. Matarajio yangu bodi hii iwe bodi ya mfano bora katika Mkoa”, aliongeza Mh. Mwema.

Nae Mwenyekiti wa Halmashauri Ndugu Abdala Bundala alisema bodi ina wajibu wa   kusimamia utoaji wa huduma za afya wilayani hapo. “ Mnapaswa mjue kua mna jukumu la kufanya kwa kushirikiana na sisi” aliongeza  Ndugu Bundala.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Bodi hiyo Bi. Elizabeth Joseph Urio, alisema kwamba wapo tayari kufanya kazi kwa taratibu zilizowekwa na zaidi kwa kujitolea.

Nae Mganga Mkuu wa Wilaya, Dr. Vicent Gyunda  ambaye pia ni Katibu wa Bodi hiyo alisema kwamba mipango ya semina imeshawekwa sawa na wajumbe watapewa semina ili kuepuka migongano ya kiutendaji. Aidha aliongeza kwa kusema uwajibikaji na kujituma ndio nguzo ya mafaniko kwa Bodi hiyo.

Jukumu jingine la bodi hiyo yenye wajumbe kumi, ni kuhakikisha upatikanaji wa rasilimali na mgawanyo wake kwa kuzingatia mahitaji ya ngazi zote za huduma na matumizi bora.

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA 11.06.2025 June 11, 2025
  • TANGAZO NAFASI YA KAZI- MWENYEKITI BODI YA MFUKO WA ELIMU June 08, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI JUNI 2025 June 07, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 06, 2025
  • Angalia zote

Habari mpya

  • MAFUNZO YA MFUMO WA E-UTENDAJI KWA WATUMISHI.

    June 12, 2025
  • KIKAO CHA MAANDALIZI YA MWENGE WA UHURU 2025

    June 11, 2025
  • WATOTO WA UMISSETA KITETO, WAWATOA JASHO WATU WAZIMA!

    June 10, 2025
  • WALIMU KITETO WAPEWA MAFUNZO YA AFUA JUMUISHI ZA ELIMU YA AFYA SHULENI

    June 05, 2025
  • Angalia zote

Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.

MWENGE MAKABIDHIANO MKOA WA MANYARA 2018
Video Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Hati ya Mshahara

Viunganishi vya Tovuti Nyingine

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • MANYARA
  • NECTA
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Kibaya-Kiteto

    Anwani ya Posta: P.o.Box 98, Kibaya-Kiteto

    Simu ya Mezani: +255 027-2552099

    Simu ya kiganjani:

    Barua Pepe: ded@kitetodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki@2017 Halimashauri ya Kiteto.Haki zote zimehifadhiwa