• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe watumishi |
    • Malalamiko |
Kiteto District Council
Kiteto District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Teknolojia,Habari ,Mawasiliano na Mahusiano
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Uchimbaji Madini
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Ardhi na Maliasili
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • This page is under construction
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi mipya
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

DC Kiteto aendesha harambee ya ujenzi wa shule katika kijiji cha Lergu

Imetumwa : November 26th, 2017


       Mkuu wa wilaya ya Kiteto Mhe. Tumaini Magessa akikagua ujenzi wa shule katika kijiji cha Lergu wilayani Kiteto.Kushoto ni diwani wa kata ya Kijungu mhe. Mandaro Mussa

       Mkuu wa wilaya ya Kiteto Mhe. Tumaini Magessa akiwa katika  harambee ya ujenzi wa shule katika kijiji cha Lergu wilayani Kiteto.Kulia ni diwani wa kata ya Kijungu mhe. Mandaro Mussa na watendaji wengine wa serikali waliombatana nae katika harambee hiyo.


 Diwani wa kata ya Kijungu Mhe. Mandaro Mussa akizungumza na wananchi wa kijiji cha Lergu  wilayani Kiteto kabla ya harambee ya ujenzi wa shule.Kushoto ni mkuu wa wilaya ya Kiteto Mhe. Tumaini Magesa.


                          Wakazi  wa kijiji cha Lergu wilayani Kiteto  wakiwa katika harambee ya  ujenzi wa shule.

               Hatua mbalimbali za ujenzi wa shule katika kijiji cha Lergu kama inavyoonekana katika picha

                                                                                                              

                                                                                                    Habari kamili......


DC Kiteto Aendesha Harambee  ya Ujenzi wa Shule   katika kijiji cha  Lergu


Mkuu wa wilaya ya Kiteto mheshimiwa  Tumaini Magesa  ameendesha  harambee ya ujenzi wa shule katika kijiji cha Lergu kata ya  Kijungu wilayani Kiteto. Mheshimiwa Magessa amesema kwamba ni muhimu kila  mwananchi wa eneo hilo kuchangia katika harambee hiyo kufanikisha ujenzi wa shule , ili kuwawezesha watoto wa kijiji hicho kuweza kupata elimu mara tu wanapofikia umri wa kuanza shule.


Akisisitiza kuhusu umuhimu wa elimu mheshimiwa Magessa anasema ‘‘Mimi tangu niliporipoti hapa nilisema kazi yangu ya kwanza ni elimu .Tukiwa na elimu , hata migogoro itapungua. Hii ni awamu ya tano ndugu zangu, muda wa kusemasema umekwisha, ni muda wa kufanya kazi tu, shule iwepo hapa. Fedha ya kujenga madarasa mawili ipatikane leo hapa.Wafugaji ninaowaona hapa nina amini hakuna  mwenye ngombe wawili ,kila mmoja ana ng’ombe wengi, lakini kijiji hakina shule. Kila mmoja ajisikie kwamba anawajibu wa kuhakikisha kuwa kijiji hiki kina kuwa na shule ili watoto wetu waweze kupata elimu bila kutembea umbali mrefu.Tutumie rasilimali tulizo nazo tuweze kukamilisha ujenzi wa shule’’.

Aidha  mkuu wa wilaya amesema kwamba watu wa kijiji hicho wengi hawajui kusoma na kuandika , si kwamba hawakupenda kwenda shule , isipokuwa mazingira hayakuwaruhusu kwenda  shule  kutokana na kutokuwepo kwa shule katika kijiji hicho tangu mwaka 1993, ambapo shule iko  umbali wa kilomita 30 kutoka kijijini hapo.Na kwamba imefika wakati sasa kijiji hicho na kijiji cha Ngapapa ambacho pia hakina shule , kuwa na shule ili kuondokana na hali hiyo ya kutokujua kusoma na kuandika.

Mheshimiwa Magessa amewataka wananchi wa vijiji vya Lergu na Ngapapa kuhakikisha kwamba ifikapo Disemba mwaka huu, vijiji hivyo vinakuwa na shule .Katika harambee hiyo kiasi cha shilingi milioni  4.9 ziliahidiwa ,ambapo mheshimiwa Magessa amechangia kiasi cha shilingi 1000,000.Fedha zote hizo zitakusanywa katika wiki moja ili kuwezesha ujenzi wa madarasa kuendelea.

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA 11.06.2025 June 11, 2025
  • TANGAZO NAFASI YA KAZI- MWENYEKITI BODI YA MFUKO WA ELIMU June 08, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI JUNI 2025 June 07, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 06, 2025
  • Angalia zote

Habari mpya

  • MAFUNZO YA MFUMO WA E-UTENDAJI KWA WATUMISHI.

    June 12, 2025
  • KIKAO CHA MAANDALIZI YA MWENGE WA UHURU 2025

    June 11, 2025
  • WATOTO WA UMISSETA KITETO, WAWATOA JASHO WATU WAZIMA!

    June 10, 2025
  • WALIMU KITETO WAPEWA MAFUNZO YA AFUA JUMUISHI ZA ELIMU YA AFYA SHULENI

    June 05, 2025
  • Angalia zote

Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.

MWENGE MAKABIDHIANO MKOA WA MANYARA 2018
Video Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Hati ya Mshahara

Viunganishi vya Tovuti Nyingine

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • MANYARA
  • NECTA
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Kibaya-Kiteto

    Anwani ya Posta: P.o.Box 98, Kibaya-Kiteto

    Simu ya Mezani: +255 027-2552099

    Simu ya kiganjani:

    Barua Pepe: ded@kitetodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki@2017 Halimashauri ya Kiteto.Haki zote zimehifadhiwa