• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe watumishi |
    • Malalamiko |
Kiteto District Council
Kiteto District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Teknolojia,Habari ,Mawasiliano na Mahusiano
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Uchimbaji Madini
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Ardhi na Maliasili
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • This page is under construction
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi mipya
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

DC MWEMA AONGOZA KIKAO CHA TATHMINI YA MBIO ZA MWENGE 2024

Imetumwa : August 4th, 2024


Agosti 1,2024 Mkuu wa Wilaya ya Kiteto, Mhe. Remidius Mwema aliongoza Kikao Cha Tathmini ya Mbio za Mwenge wa Uhuru 2024 wilayani hapo.

Kikao hicho kilichohudhuriwa na wajumbe wa kamati ya Maandalizi ya Mwenge wa Uhuru kililenga kujua mafanikio na changamoto zilizojitokeza wakati wa maandalizi na siku husika ya Mwenge wa Uhuru ulipokimbizwa wilayani hapo.

Awali Mratibu wa Mbio za Mwenge Wilayani Kiteto, Ndug. Rodrick Kidenya alitoa taarifa za ujumla za kuanzia  maandalizi ya mapokezi ya Mwenge, taarifa ya  siku husika ya Mwenge wa Uhuru kuwepo Wilayani hapo na taarifa ya makabidhiano ya Mwenge wa Uhuru katika wilaya ya Simanjiro.

Wenyeviti wote wa kamati mbalimbali za Maandalizi ya Mbio za Mwenge 2024, walipata fursa ya kutoa taarifa ya matumizi ya kamati zao , kueleza majukumu waliyotekeleza na kueleza changamoto walizokutana nazo. Aidha wajumbe mbalimbali walipewa nafasi kuchangia taarifa zilizotolewa na wenyeviti wa  kamati hizo.

Mhe. Mwema  alisema kwamba, kikao hicho kilikua muhimu kwani kitasaidia kuboresha Maandalizi ya Mapokezi ya Mwenge wa Uhuru kwa miaka ijayo.

Aidha Mhe. Mwema ametoa shukrani kwa Chama Cha Mapinduzi, Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya, wanakamati,  wananchi, taasisi binafsi na za serikali na watumishi wote kwa ushirikiano wao waliounesha toka wakati wa maandalizi hadi kukamilika kwa Mbio za Mwenge wa Uhuru 2024 Wilaya hapo.

Katika kikao hicho aidha Mhe. Mwema aliweza kukata keki iliyoandaliwa na mmoja wa wanakamati hao, na kuwalisha wajumbe wote ikiwa ni ishara ya kuwapongeza na kuwashukuru kwa kuweza kufanikisha Mbio za Mwenge wa Uhuru 2024.

Mwenge wa Uhuru Wilaya hapo ulipokelewa Julai 17, 2024 na kukimbizwa umbali wa takribani kilomita68 na kuzindua, kufungua na kutembelea miradi yenye jumla ya thamani ya TZS Bilioni 3.37. Mwenge wa Uhuru uliridhia miradi yote wilayani hapo.

“Tunza Mazingira na Shiriki Uchaguzi wa Serikali za Mtaa kwa Ujenzi wa Taifa Endelevu”.

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA 11.06.2025 June 11, 2025
  • TANGAZO NAFASI YA KAZI- MWENYEKITI BODI YA MFUKO WA ELIMU June 08, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI JUNI 2025 June 07, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 06, 2025
  • Angalia zote

Habari mpya

  • MAFUNZO YA MFUMO WA E-UTENDAJI KWA WATUMISHI.

    June 12, 2025
  • KIKAO CHA MAANDALIZI YA MWENGE WA UHURU 2025

    June 11, 2025
  • WATOTO WA UMISSETA KITETO, WAWATOA JASHO WATU WAZIMA!

    June 10, 2025
  • WALIMU KITETO WAPEWA MAFUNZO YA AFUA JUMUISHI ZA ELIMU YA AFYA SHULENI

    June 05, 2025
  • Angalia zote

Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.

MWENGE MAKABIDHIANO MKOA WA MANYARA 2018
Video Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Hati ya Mshahara

Viunganishi vya Tovuti Nyingine

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • MANYARA
  • NECTA
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Kibaya-Kiteto

    Anwani ya Posta: P.o.Box 98, Kibaya-Kiteto

    Simu ya Mezani: +255 027-2552099

    Simu ya kiganjani:

    Barua Pepe: ded@kitetodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki@2017 Halimashauri ya Kiteto.Haki zote zimehifadhiwa