• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe watumishi |
    • Malalamiko |
Kiteto District Council
Kiteto District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Teknolojia,Habari ,Mawasiliano na Mahusiano
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Uchimbaji Madini
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Ardhi na Maliasili
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • This page is under construction
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi mipya
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

KAMATI YA FEDHA YAKAGUA MIRADI YA BILIONI 1.4, YASISITIZA UWAJIBIKAJI

Imetumwa : January 31st, 2026

Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango ya Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto leo Januari 31, 2026 imefanya ziara ya ukaguzi wa miradi minne ya maendeleo yenye jumla ya thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 1.4, hatua inayodhihirisha dhamira ya Serikali katika kusimamia matumizi ya fedha za umma na kuhakikisha wananchi wananufaika moja kwa moja na rasilimali zao.


Akizungumza katika ziara hiyo kwa nyakati tofauti, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mhe. Athumani Hamisi Kilimo, ametoa shukrani kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuiamini Kiteto na kuelekezea fedha nyingi za maendeleo, akisema hatua hiyo ni ushahidi  kuwa wa serikali inasikiliza na  na kutenda.


Mhe. Kilimo amesema fedha hizo zimekuwa chachu ya  kuimarisha huduma za afya na elimu, huku akisisitiza kuwa jukumu la viongozi wa ngazi ya Halmashauri ni kuhakikisha kila shilingi inatumika ipasavyo na kuleta tija kwa wananchi.


Aidha, Kamati hiyo ilitoa shukrani  kwa Mbunge wa Jimbo la Kiteto, Mhe. Edward Ole Lekaita kwa juhudi zake za kisiasa na kiuwakilishi katika kufuatilia na kusimamia upatikanaji wa fedha za miradi ya maendeleo kutoka Serikali Kuu, akielezwa kuwa daraja muhimu kati ya wananchi na Serikali.


Wajumbe wa Kamati walieleza kuridhishwa na maendeleo ya utekelezaji wa miradi hiyo, huku wakisisitiza umuhimu wa miradi kukamilika kwa wakati na kwa kuzingatia viwango vya ubora, ili thamani ya fedha ionekane na wananchi waanze kunufaika na huduma husika kwa mujibu wa malengo ya Serikali.


Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto ambaye ndiye mtekelezaji wa shughuli za Halmashauri CPA, Hawa Abdul Hassan, ameahidi kuendelea kufanya ufuatiliaji wa karibu wa miradi ya maendeleo kwa kushirikiana na Wataalamu ili kuhakikisha thamani ya fedha inayoletwa na serikali inaridhisha.


Miradi iliyokagukiwa na Kamati hiyo ni  ujenzi wa jengo jipya la OPD katika Hospitali ya Wilaya iliyopo Kata ya Kibaya wenye thamani ya shilingi milioni 800. Pia ilikagua ujenzi wa jengo la OPD katika Kijiji cha Irkiushbor katika Kata ya Makame lenye thamani ya shilingi milioni 250.
Mbali na sekta ya afya, Kamati ilikagua pia miradi ya elimu ikiwemo ujenzi wa madarasa matatu na matundu sita ya vyoo kwa elimu ya msingi, pamoja na madarasa mawili na matundu sita ya vyoo kwa elimu ya awali katika Shule ya Msingi Oloimugi (Oltaret) katika kata ya Namelock, mradi wenye thamani ya shilingi milioni 157.7. Aidha, ziara hiyo ilihitimishwa kwa ukaguzi wa ujenzi wa mabweni mawili katika Shule ya Sekondari Dosidosi yenye thamani ya shilingi milioni 260.

Ziara hiyo ni  moja ya mkakati wa  kiutawala wa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto katika kusimamia maendeleo, kuimarisha uwajibikaji na kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora kwa wakati.

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA MAPOKEZI YA FEDHA SEPTEMBA 2025 September 16, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU September 01, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI September 01, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI JUNI 2025 June 07, 2025
  • Angalia zote

Habari mpya

  • KAMATI YA FEDHA YAKAGUA MIRADI YA BILIONI 1.4, YASISITIZA UWAJIBIKAJI

    January 31, 2026
  • BARAZA LA MADIWANI KITETO LAPITISHA BAJETI YA SHILINGI BILIONI 41.9 KWA MWAKA WA FEDHA 2026/2027

    January 27, 2026
  • DC MWEMA AAGIZA USIMAMIZI MADHUBUTI WA SHERIA NA ULINZI WA MIUNDOMBINU YA SERIKALI

    January 26, 2026
  • WATENDAJI WILAYANI KITETO WAKUMBUSHWA KUONGEZA JUHUDI KATIKA UTEKELEZAJI WA AFUA ZA LISHE.

    January 14, 2026
  • Angalia zote

Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.

MWENGE MAKABIDHIANO MKOA WA MANYARA 2018
Video Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Hati ya Mshahara

Viunganishi vya Tovuti Nyingine

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • MANYARA
  • NECTA
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Kibaya-Kiteto

    Anwani ya Posta: P.o.Box 98, Kibaya-Kiteto

    Simu ya Mezani: +255 027-2552099

    Simu ya kiganjani:

    Barua Pepe: ded@kitetodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki@2017 Halimashauri ya Kiteto.Haki zote zimehifadhiwa