• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe watumishi |
    • Malalamiko |
Kiteto District Council
Kiteto District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Teknolojia,Habari ,Mawasiliano na Mahusiano
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Uchimbaji Madini
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Ardhi na Maliasili
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • This page is under construction
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi mipya
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

DC MWEMA ASISITIZA USALAMA KATIKA MACHIMBO YA ILNDORKON

Imetumwa : May 7th, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Kiteto, Mh. Remidius Mwema Emmanuel, amewahimiza wachimbaji wadogo katika eneo la machimbo ya dhahabu  la Ilndorkon pamoja na muwekezaji wa eneo hilo  kufuata kanuni za usalama katika shughuli zao.

Mh. Mwema ameyasema hayo Mei 6,2024 alipotembelea machimbo hayo ili kujionea shughuli za uchimbaji wa madini ya dhahabu katika eneo hilo pamoja na kuongea na muwekezaji  AutoGerm Mining LTD (AGM LTD) pamoja na wachimbaji wadogo wa eneo hilo.

Akiongea mara baada ya  kukagua eneo ambalo uchimbaji unafanyika, Mh. Mwema amesema kwamba amejionea baadhi ya maduara (mashimoi) ya machimbo hayajazingatia kanuni ya umbali kutoka shimo moja hadi jingine.

“Kuna mashimo yapo wazi hii ni hatari kwa usalama. Pia umbali kati ya shimo na shimo inapaswa kua  ni mita 15 hii ni kwaajili ya usalama wa wachimbaji ila nimeona kuna baadhi ya mashimo hayajafuata utaratibu huu” alisema Mh. Mwema.

Kuhusiana na mashimo ambayo yapo wazi na ambayo yapo karibu karibu, Mh. Mwema amemuagiza Msimamizi wa Mgodi huo Ndg Majura Yohana kuhakikisha kua wanasimamia taratibu zote za kiusalama mgodini hapo ili kuhakikisha wachimbaji  wanafanya kazi katika mazingira salama.

Akijibu hoja ya mashimo yaliyo wazi, msimamizi huyo  amesema kwamba wameweka utaratibu mpya wa kuhakikisha kila siku asubuhi wanatumia muda wa saa  moja (1)  kufukia mashimo. Utaratibu huo umepangwa kuanza  Mei 7,2024. Na kwa upande wa mashimo ambayo hayajafuata utaratibu wa umbali kutoka shimo hadi shimo, iliazimiwa mashimo hayo yafungwe miti (matimba).

Aidha Mh.Mwema amesema kwamba ni lazma wachimbaji waliopo eneo hilo kuweka utaratibu maalumu wa kumfahamu kila mmoja aliyepo eneo hilo. Vilevile aliwasisitiza wachimbaji hao kuzingatia maadili na matumizi bora ya fedha wanazozipata na kuwaasa kutozisahau familia zao walizoziacha mbali.

Upande wa afya na mazingira, Mh. Mwema aliagiza kuongezwa kwa matundu ya vyoo katika eneo hilo ili kukidhi mahitaji kwani matundu yaliyopo ni machache kuliko idadi ya watu.

“Mazingira ya usafi hayaridhishi, watu wote wanaouza chakula waweke eneo maalumu la kukusanyia taka. Wote mnapaswa kuzingatia kanunii za afya ili kujikinga dhidi ya magonjwa ya mlipuko” aliongeza Mh. Mwema.

Machimbo ya Ilndorokon yalianza rasmi April 15,2024 na mpaka sasa eneo hilo lina watu wapatao 320.

Matangazo

  • TANGAZO NAFASI ZA KAZI July 23, 2021
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI NAFASI YA UTENDAJI WA KIJlJI III August 26, 2021
  • TANGAZO LA KUKODISHA VIBANDA March 01, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI SEPTEMBA 2023 September 03, 2023
  • Angalia zote

Habari mpya

  • TABIA MBAYA ZA WATUMUSHI ZINAHARIBU SIFA ZA TAASISI

    May 01, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI KITETO LIMEMPONGEZA RAIS SAMIA.

    May 30, 2025
  • PONGEZI KWA WANANCHI KWA KUTUNZA MAZINGIRA

    April 28, 2025
  • TUUENZI MUUNGANO WETU

    April 27, 2025
  • Angalia zote

Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.

MWENGE MAKABIDHIANO MKOA WA MANYARA 2018
Video Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Hati ya Mshahara

Viunganishi vya Tovuti Nyingine

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • MANYARA
  • NECTA
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Kibaya-Kiteto

    Anwani ya Posta: P.o.Box 98, Kibaya-Kiteto

    Simu ya Mezani: +255 027-2552099

    Simu ya kiganjani:

    Barua Pepe: ded@kitetodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki@2017 Halimashauri ya Kiteto.Haki zote zimehifadhiwa