• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe watumishi |
    • Malalamiko |
Kiteto District Council
Kiteto District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Teknolojia,Habari ,Mawasiliano na Mahusiano
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Uchimbaji Madini
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Ardhi na Maliasili
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • This page is under construction
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi mipya
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

JUMUIYA YA HIFADHI YA WANYAMAPORI MAKAME KITETO YANYAKUA TUZO YA SERENGETI KWA UBORA WA UHIFADHI SHIRIKISHI

Imetumwa : February 2nd, 2026

Jumuiya ya Hifadhi ya Wanyamapori Makame (WMA Makame), iliyopo Wilaya ya Kiteto, imeandika historia mpya katika sekta ya uhifadhi nchini baada ya kunyakua Tuzo ya Serengeti, tuzo inayotolewa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa taasisi na wadau waliotoa mchango mkubwa katika kulinda rasilimali za wanyamapori, misitu na mazingira kwa ujumla.


Tuzo hiyo ilitolewa Januari 31, 2026, katika Hoteli ya Mount Meru, jijini Arusha, kwenye hafla maalum iliyoandaliwa na Wizara ya Maliasili na Utalii. Mgeni Rasmi katika hafla hiyo alikuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Mwigulu Nchemba. 

Tuzo hiyo ilipokelewa na Katibu wa Jumuiya ya Hifadhi ya Wanyamapori Makame, Ndg. Supuk Olekao, kwa niaba ya jumuiya hiyo huku tukio hilo likishuhudiwa na Mkuu wa Wilaya ya Kiteto,Mhe.Remidius Mwema Emmanuel.


Jumuiya ya Hifadhi ya Wanyamapori Makame iliibuka mshindi kati ya jumuiya sita (6) za hifadhi za wanyamapori zilizoshindanishwa katika kipengele hicho, huku Tanzania ikiwa na jumla ya jumuiya arobaini (40) za hifadhi za wanyamapori, hali inayoonesha ushindani mkubwa na thamani ya ushindi uliopatikana.


Sababu kuu iliyoifanya jumuiya hiyo kutwaa tuzo hiyo ni utekelezaji wake wa mfumo bora wa uhifadhi shirikishi, unaowashirikisha wananchi kikamilifu katika maamuzi ya uhifadhi na usimamizi wa rasilimali za asili. Kupitia mfumo huo, wananchi wameweza kutambua kuwa uhifadhi si kikwazo cha maendeleo bali ni fursa ya maendeleo ya kijamii na kiuchumi.


Aidha, Jumuiya ya Hifadhi ya Wanyamapori Makame imetajwa kuwa mfano bora wa matumizi ya mfumo wa kisasa wa usimamizi wa taarifa, unaorahisisha upatikanaji wa taarifa kwa wakati, kwa uwazi, na kwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu za nchi. Mfumo huo umeongeza ufanisi katika ulinzi wa rasilimali za asili na kuimarisha uwajibikaji kwa wadau wote.


Sifa nyingine iliyoipa jumuiya hiyo ushindi ni namna manufaa yatokanayo na shughuli za uhifadhi yanavyorejeshwa kwa jamii, kupitia utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo ya kijamii na kiuchumi. Kupitia mkabala huo, wananchi wamekuwa tayari kutenga ardhi yao kwa ajili ya uhifadhi bila migogoro, jambo lililochangia mafanikio endelevu ya jumuiya hiyo.

Wataalamu wa uhifadhi wameielezea Jumuiya ya Hifadhi ya Wanyamapori Makame kama eneo salama na la mfano wa kuigwa, hasa katika usimamizi wa uhifadhi unaoongozwa na jamii, utekelezaji wa sera ya uhifadhi shirikishi, na katika kuleta matokeo chanya yanayogusa maisha ya wananchi moja kwa moja.


Kupatikana kwa tuzo hiyo kunatarajiwa kuongeza hamasa kwa wadau wa maendeleo na sekta ya utalii kushirikiana na jumuiya hiyo, pamoja na kufungua fursa mpya za uwekezaji katika utalii wa ikolojia na utalii wa kitamaduni, ikiwemo utalii wa vyakula vya asili na mila za jamii zinazozunguka hifadhi hiyo.


Kwa ujumla, Tuzo ya Serengeti kwa Jumuiya ya Hifadhi ya Wanyamapori Makame imeonesha dhamira ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kuthamini na kuhamasisha juhudi za wadau wanaolinda rasilimali za asili kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho, huku jumuiya hiyo ikiendelea kuwa kielelezo cha uhifadhi endelevu unaomshirikisha mwananchi.

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA MAPOKEZI YA FEDHA SEPTEMBA 2025 September 16, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU September 01, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI September 01, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI JUNI 2025 June 07, 2025
  • Angalia zote

Habari mpya

  • JUMUIYA YA HIFADHI YA WANYAMAPORI MAKAME KITETO YANYAKUA TUZO YA SERENGETI KWA UBORA WA UHIFADHI SHIRIKISHI

    February 02, 2026
  • DED KITETO AWAPONGEZA WALIMU KWA KUPANDISHA UFAULU KIDATO CHA NNE

    February 01, 2026
  • KAMATI YA FEDHA YAKAGUA MIRADI YA BILIONI 1.4, YASISITIZA UWAJIBIKAJI

    January 31, 2026
  • BARAZA LA MADIWANI KITETO LAPITISHA BAJETI YA SHILINGI BILIONI 41.9 KWA MWAKA WA FEDHA 2026/2027

    January 27, 2026
  • Angalia zote

Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.

MWENGE MAKABIDHIANO MKOA WA MANYARA 2018
Video Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Hati ya Mshahara

Viunganishi vya Tovuti Nyingine

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • MANYARA
  • NECTA
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Kibaya-Kiteto

    Anwani ya Posta: P.o.Box 98, Kibaya-Kiteto

    Simu ya Mezani: +255 027-2552099

    Simu ya kiganjani:

    Barua Pepe: ded@kitetodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki@2017 Halimashauri ya Kiteto.Haki zote zimehifadhiwa