• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe watumishi |
    • Malalamiko |
Kiteto District Council
Kiteto District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Teknolojia,Habari ,Mawasiliano na Mahusiano
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Uchimbaji Madini
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Ardhi na Maliasili
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • This page is under construction
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi mipya
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

DC MWEMA AWEKA JIWE LA MSINGI MRADI WA MAJI MAGUNGU-NHATI

Imetumwa : March 21st, 2024


Mkuu wa Wilaya ya Kiteto Mh. Remidius Mwema Emmanuel, ameweka jiwe la msingi kwenye mradi wa maji wa Magungu –Nhati wenye thamani ya shilingi 1.2bil. uliopo katika kata ya Magungu.

Tukio hilo ambalo lilishuhudiwa na viongozi mbalimbali wa chama na serikali, Kaimu Mkurugenzi pamoja na wananchi, limefanyika Machi 21, 2024 kwenye kijiji cha Magungu katika Maadhimisho ya Wiki ya Maji Kiwilaya.

Akitoa taarifa ya mradi huo, Meneja wa RUWASA Kiteto, Mhandisi Stephano, Mbaruku, amesema kwamba Mradi wa Maji Magungu-Nhati uliibuliwa na RUWASA kwa kushirikiana na jamii na Halmashauri ya Wilaya Kiteto. Mwaka 2022/2023 RUWASA ilipokea  fedha kutoka serikali kuu kwaajili ya utekelezaji wa mradi huo ambao kisima chake kina urefu wa mita 120 na kwasasa  kina uwezo wa kuzalisha maji lita 26,000  kwa saa.

“Mradi wa Maji Magungu –Nhati umetelezwa kwakutumia wataalamu wa ndani kuanzia 15 Septemba 2022 na kakamilika 30/7/2023 na kwasasa utekelezaji wa mradi huu umekalika kwa asilimia 100,” aliongeza Mhandisi Mbaruku.

Akiongea katika hafla hiyo ya uwekaji wa Jiwe la Msingi na Maadhimisho ya Wiki ya Maji, Mgeni Rasmi Mh.Mwema aliishukuru serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mh. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa fedha za mradi huo na pia aliipongeza jamii na RUWASA kwa kutekeleza mradi huo.

Aidha Mh. Mwema alikemea vitendo vya uharibifu wa miundombinu ya maji ambao umekua ukifanywa na baadhi ya wananchi kwenye baadhi ya maeneo na kufanya jamii kukosa huduma ya maji na kuipa serikali hasara.

Mbali na hayo, Mh. Mwema amekataza shughuli za kibinadamu karibu na vyanzo vya maji na kuagiza utunzaji wa mazingira kwenye vyanzo vya maji.

“Lazma vyanzo vya maji vitunzwe maeneo yote yenye vyanzo vya maji, miti ipandwe”, aliongeza  Mh. Mwema.

Mradi wa Maji Magungu- Nhati utahudumia zaidi ya wakazi 7,500 wa kijiji cha Magungu na Nhati. Kukamilika na kuanza kazi kwa mradi huu kunawaongezea wananchi wa vijiji hivyo muda wa kufanya shughuli nyingine za kiuchumi badala ya kutumia muda mwingi kutafuta maji. Aidha kunapunguza magonjwa yatokanayo na ukosefiu wa maji safi na salama.

Kata ya Magungu ina vijiji vitatu ambavyo ni Magungu, Nhati na Emarti ila kwasasa mradi huo unahudumia kijiji cha Nhati na Magungu. Hivyo DC Mwema amewaambia RUWASA kuangalia namna ya kuwawezesha  wanakijiji wa Emarti nao wananufaika na mradi huo.

Katika kutekeleza mradi huo, jamii ilichangia kiasi cha sh 2m, Chombo cha Watumia Maji 37M na serikali kuu 1.2bil.

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA 11.06.2025 June 11, 2025
  • TANGAZO NAFASI YA KAZI- MWENYEKITI BODI YA MFUKO WA ELIMU June 08, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI JUNI 2025 June 07, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 06, 2025
  • Angalia zote

Habari mpya

  • MAFUNZO YA MFUMO WA E-UTENDAJI KWA WATUMISHI.

    June 12, 2025
  • KIKAO CHA MAANDALIZI YA MWENGE WA UHURU 2025

    June 11, 2025
  • WATOTO WA UMISSETA KITETO, WAWATOA JASHO WATU WAZIMA!

    June 10, 2025
  • WALIMU KITETO WAPEWA MAFUNZO YA AFUA JUMUISHI ZA ELIMU YA AFYA SHULENI

    June 05, 2025
  • Angalia zote

Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.

MWENGE MAKABIDHIANO MKOA WA MANYARA 2018
Video Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Hati ya Mshahara

Viunganishi vya Tovuti Nyingine

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • MANYARA
  • NECTA
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Kibaya-Kiteto

    Anwani ya Posta: P.o.Box 98, Kibaya-Kiteto

    Simu ya Mezani: +255 027-2552099

    Simu ya kiganjani:

    Barua Pepe: ded@kitetodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki@2017 Halimashauri ya Kiteto.Haki zote zimehifadhiwa