• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe watumishi |
    • Malalamiko |
Kiteto District Council
Kiteto District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Teknolojia,Habari ,Mawasiliano na Mahusiano
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Uchimbaji Madini
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Ardhi na Maliasili
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • This page is under construction
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi mipya
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

DED Kambona Awataka Washiriki wa UMISETA Kuonyesha Jitihada.

Imetumwa : May 21st, 2018


Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Kiteto Ndg. Tamim Kambona akisalimiana na wachezaji wakati akikagua timu tayari kwa kuanza  UMISETA ngazi ya wilaya.Walio nyuma yake ni Afisa elimu Sekondari (W) Ndg. Mtinga Maleya na Mratibu wa UMISETA (W) Ndg. Riziki Lymo.


Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Kiteto Ndg. Tamim Kambona (aliyesimama katikati) akizungumza na washiriki wa UMISETA  wakati akifungua UMISETA ngazi ya wilaya.

Timu  zikiwa zimejipanga tayari kuanza UMISETA ngazi ya wilaya.




..............HABARI KAMILI............




Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Kiteto ndugu Tamim Kambona,amewataka wanafunzi wanaoshiriki katika Umoja wa Michezo ya Shule za Sekondari Tanzania ( UMISETA ) ngazi ya wilaya kuonyesha jitihada ili waweze kufuzu vigezo vya kushiriki  katika michezo hiyo kimkoa na hata kitaifa.Ndugu Kambona ameyasema hayo wakati akifungua kambi michezo hiyo, ambapo watapatikana washiriki watakaoiwakilisha wilaya katika UMISETA mkoani.



Akisisitiza kuhusu washiriki  washiriki hao kufanya bidii katika michezo hiyo, Kambona amesema “Mimi mkurugenzi kwa nafasi yangu nitaonyesha jitihada,kuhakikisha kwamba mnapata kila mnachotakiwa kupata wakati wote mtakaokuwepo katika michezo hii,walimu kwa nafasi yao wataonyesha jitihada zao.Tunataka tuone mkifanya jitihada.Ni jitihada pekee itakayowawezesha kufika mbali katika michezo hii.Mtafika babati mkoani, mtafika Mwanza kwenye mashindano ya kitaifa,endapo tu mtaonyesha jitihada”.


Aidha ndugu Kambona amesisitiza kuhusu suala la nidhamu kwa washiriki wa michezo hiyo, ambapo amesema kwamba,kama ambavyo wamekuwa wakionyesha nidhamu wakati wakiwa mashuleni kwao,vivyo hiyo waonyeshe nidhamu hiyo wakati wote watakapokuwa katika michezo hiyo kambini hapo,na kwingine kote watakako kwenda katika michezo hiyo.Na sio kwamba waende wakafanye mambo ambayo ni kinyume na lengo lililokusudiwa.


Michezo hiyo itahitimishwa siku ya Ijumaa, washiriki waliochaguliwa kuwakilisha wilaya ngazi ya mkoa ,wataondoka siku hiyo hiyo ya ijumaa kuelekea makao makuu ya mkoa wa manyara ( Babati) .Huko  UMISETA itaendelea ,ambapo watapatikana washiriki watakao wakilisha mkoa wa Manyara katika ngazi ya taifa ambayo hiyo itafanyika mkoani Mwanza.



..........MWISHO...........


Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA 11.06.2025 June 11, 2025
  • TANGAZO NAFASI YA KAZI- MWENYEKITI BODI YA MFUKO WA ELIMU June 08, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI JUNI 2025 June 07, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 06, 2025
  • Angalia zote

Habari mpya

  • MAFUNZO YA MFUMO WA E-UTENDAJI KWA WATUMISHI.

    June 12, 2025
  • KIKAO CHA MAANDALIZI YA MWENGE WA UHURU 2025

    June 11, 2025
  • WATOTO WA UMISSETA KITETO, WAWATOA JASHO WATU WAZIMA!

    June 10, 2025
  • WALIMU KITETO WAPEWA MAFUNZO YA AFUA JUMUISHI ZA ELIMU YA AFYA SHULENI

    June 05, 2025
  • Angalia zote

Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.

MWENGE MAKABIDHIANO MKOA WA MANYARA 2018
Video Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Hati ya Mshahara

Viunganishi vya Tovuti Nyingine

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • MANYARA
  • NECTA
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Kibaya-Kiteto

    Anwani ya Posta: P.o.Box 98, Kibaya-Kiteto

    Simu ya Mezani: +255 027-2552099

    Simu ya kiganjani:

    Barua Pepe: ded@kitetodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki@2017 Halimashauri ya Kiteto.Haki zote zimehifadhiwa