• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe watumishi |
    • Malalamiko |
Kiteto District Council
Kiteto District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Teknolojia,Habari ,Mawasiliano na Mahusiano
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Uchimbaji Madini
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Ardhi na Maliasili
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • This page is under construction
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi mipya
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

DED Kiteto Ahimiza Ujenzi wa Madarasa

Imetumwa : November 1st, 2018

Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Kiteto  Ndg. Tamim Kambona akizungumza   wakati wa kikao cha baraza la Madiwani la halmashauri ya wilaya ya kiteto  kilichofanyika katika ukumbi wa halmashauri, Oktoba 31,2018.



..... HABARI KAMILI.......




Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Kiteto ndugu Tamim Kambona amewataka watendaji wote wilayani hapa kuhakikisha kwamba ujenzi wa madarasa unafanyika  kwa ajili ya kidato cha kwanza mwaka 2019. Ndugu Kambona ametoa maelekezo  hayo oktoba 31 ,2018 katika kikao cha baraza la madiwani kilichofanyika katika ukumbi wa Halmashauri  .


Akizungumza wakati wa kikao hicho ndugu Kambona amesema “ Tunajua kwamba mwezi wa kwanza tutakuwa na mlundikano wa wanafunzi, asilimia 69.5 ya wanafunzi waliofaulu ni kubwa sana, kwa hiyo lazima kutahitajika vyumba vya madarasa, na madawati. Waheshimiwa madiwani wote,maafisa tarafa, watendaji wa kata na watendaji wa vijiji wote  pamoja na waratibu elimu kata tushirikiane kwenye hili, ili tuhakikishe  wanafunzi wetu wote waliofaulu wanapata nafasi ya  kujiunga  na kidato cha kwanza kama ilivyokuwa kwa mwaka huu 2018.


Ndugu Kambona ameomba ushirikiano wa watu wote katika kuhakikisha kwamba wanafunzi wote waliofaulu wanaripoti katika shule walizopangiwa kwa wakati na wanaendelea na masomo yao.


Kadhalika  ndugu Kambona amezungumzia suala la utoro wa wanafunzi mashuleni ambapo  amewataka maafisa tarafa, maafisa watendaji wa kata na vijiji  pamoja na waratibu wa elimu kata kwa kushirikiana na waheshimiwa madiwani kuhakikisha kwamba suala la utoro linaondoka, vile vile kuhakikisha kwamba wanafunzi hawapewi kazi ambazo sio za umri wao, kazi ambazo kwa namna moja ama nyingine zimekuwa zikichangia ongezeko la utoro wa wanafunzi mashuleni,pia kusababisha wanafunzi kutokuwa na muda wa kutosha kujisomea, watendaji hao pia wahakikishe kwamba watoto wote wanaojiunga na kidato cha kwanza wanamaliza kidato cha nne.


Aidha ndugu Kambona amezungumzia suala la uchangiaji wa chakula mashuleni, amesema kwamba wazazi wanatakiwa kuchangia vyakula mashuleni  ili katika shule zote , za msingi na sekondari wanafunzi waweze kula chakula cha mchana , lakini wazazi wasilazimishwe kuchangia maharage , wakati uwezo wao ni kuchangia mbaazi ambazo bei yake ni nafuu zaidi kuliko bei ya maharage.Na kwamba mbaazi ni chakula halali kama vyakula vingine na kina protini kama ilivyo kwa maharage, hivyo wazazi wasikwazwe kwa kulazimishwa kuchangia maharage wakati wao wana magunia ya  mbaazi ndani.


Katika hatua nyingine ndugu Kambona amewaagiza wakuu wote wa shule kununua vyakula vya shule kwa bei ya soko.Ameendelea kusema kwamba kadiri mahindi yanavyoshuka bei, na bei ambazo wakuu hao wa shule wananunua vyakula zinatakiwa ziwe zinashuka, ili fedha zinazobaki katika ununuzi wa vyakula zitumike katika kutekeleza miradi mingine ya maendeleo.


 Ndugu Kambona pia aamezungumzia kuhusu  fedha za mfuko wa pamoja ‘basket fund’  zilizopo katika vituo vya afya na zahanati , ambazo zilitolewa tangu mwaka jana  kwa ajili ya ukarabati , amewaomba waheshimiwa madiwani kuhakikisha kwamba ukarabati unafanyika katika vituo vya afya na zahanati zote .


Wilaya ya Kiteto imekuwa ya mfano wa kuigwa kwa uibuaji na utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo.Miradi ambayo imekuwa ya manufaa makubwa kwa jamii yote.




...........MWISHO............

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA 11.06.2025 June 11, 2025
  • TANGAZO NAFASI YA KAZI- MWENYEKITI BODI YA MFUKO WA ELIMU June 08, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI JUNI 2025 June 07, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 06, 2025
  • Angalia zote

Habari mpya

  • HAYAWI HAYAWI SASA YAMEKUA: HATIMAYE KALOLENI YAPATA SHULE MPYA YA MSINGI

    July 30, 2025
  • SHULE YA MSINGI KINANGALI NAYO YANUFAIKA NA MRADI WA BOOST

    July 30, 2025
  • SERIKALI YA AWAMU YA SITA YAENDELEA KUWEKEZA KWA VITENDO: KURASH YAPATA MRADI MWINGINE WA MILIONI 153 KUPITIA BOOST

    July 30, 2025
  • KATA YA BWAWANI YAPATA MRADI WA SHULE MPYA YA ELIMU MSINGI.

    July 28, 2025
  • Angalia zote

Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.

MWENGE MAKABIDHIANO MKOA WA MANYARA 2018
Video Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Hati ya Mshahara

Viunganishi vya Tovuti Nyingine

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • MANYARA
  • NECTA
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Kibaya-Kiteto

    Anwani ya Posta: P.o.Box 98, Kibaya-Kiteto

    Simu ya Mezani: +255 027-2552099

    Simu ya kiganjani:

    Barua Pepe: ded@kitetodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki@2017 Halimashauri ya Kiteto.Haki zote zimehifadhiwa