• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe watumishi |
    • Malalamiko |
Kiteto District Council
Kiteto District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Teknolojia,Habari ,Mawasiliano na Mahusiano
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Uchimbaji Madini
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Ardhi na Maliasili
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • This page is under construction
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi mipya
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Halmashauri ya wilaya ya Kiteto yazindua SACCOS ya vijana.

Imetumwa : September 12th, 2017

                                                                                               

Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Kiteto  Mh. Lairumbe Mollel  akizungumza na vijana  baada ya uzinduzi wa SACCOS ya vijana uliofanyika katika ukumbi wa halmashauri ya wilaya ya Kiteto


Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Kiteto ndugu Tamim Kambona  akizungumza na vijana  katika uzinduzi wa SACCOS ya vijana uliofanyika katika ukumbi wa halmashauri ya wilaya ya Kiteto.

Mkuu wa idara ya maendeleo ya jamii ndugu Joseph Mwaleba akitoa neno la ukaribisho kabla ya uzinduzi wa SACCOS ya vijana uliofanyika katika ukumbi wa  Halmashauri ya wilaya ya Kiteto.

Mkuu wa idara ya kilimo  ,umwagiliaji na ushirika halmashauri ya wilaya ya Kiteto  ndugu  Robert Urassa akizungumza katika uzinduzi wa SACCOS ya vijana uliofanyika katika ukumbi wa  Halmashauri ya wilaya ya Kiteto.

Afisa ushirika ndugu Joseph Mwanga akitoa maelekezo kuhusu taratibu za uanzishwaji na uendeshaji wa SACCOS baada  ya uzinduzi wa SACCOS ya vijana uliofanyika katika ukumbi wa  Halmashauri ya wilaya ya Kiteto.

Aisa maendeleo ya jamii anayeshughulika na vijana ndugu Rodrick Kidenya akiwasilisha ombi la vijana   kwa mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Kiteto  kuwa mlezi wa SACCOS ya vijana. 

Vijana wakiwa katika picha ya pamoja na mwenyekiti wa halmashauri  ya wilaya ya Kiteto Mh. Lairumbe Mollel,mkurugenzi  mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Kiteto ndugu Tamim Kambona,Mkuu wa idara ya maendeleo ya jamii ndugu  Joseph Mwaleba,mkuu wa idara ya Kilimo ushirika na umwagiliaji ndugu Robert  Urassa,afisa ushirika   ndugu Joseph Mwanga, afisa maendeleo ya jamii anayeshughulika na vijana ndugu Rodrick Kidenya na uongozi wa muda wa Kiteto Vijana SACCOS baada ya uzinduzi wa SACCOS hiyo uliofanyika katika ukumbi wa halmashauri ya wilaya ya Kiteto.

                                                                                                                                                       

                                             Vijana wakisikiliza kwa makini maelekezo  baada ya  uzinduzi wa SACCOS yao uliofanyika katika ukumbi wa halmashauri ya wilaya ya Kiteto                                                                                                   

  HABARI KAMILI

                           

Halmashauri  ya  wilaya  ya Kiteto   yazindua  SACCOs  ya vijana  .

Halmashauri ya wilaya ya kiteto  imezindua SACCOs ya vijana wa wilaya ya kiteto . Uzinduzi huo umefanyika katika ukumbi wa halmashauri ya wilaya ya Kiteto  ambapo mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Kiteto  mheshimiwa Lairumbe Mollel amemkabidhi mwenyekiti wa muda wa bodi ya SACCOS hiyo  ndugu Hamza Ally cheti cha usajili ,sera na katiba ya SACCOs hiyo ambayo  itajulikana kwa jina la Kiteto Vijana SACCOs .

Aidha mheshimiwa Mollel amewapongeza vijana kwa kujiunga na SACCOs , amesema kuna maagizo ya waziri mkuu kwamba katika kuchagua viongozi wa vyama vya ushirika  mtu yeyote ambaye alikuwa kwenye ushirika huko nyuma asichaguliwe kuwa kiongozi, kwa sababu imeonekana kwamba walifanya vibaya, wawachague viongozi wazuri , ambao watasimamia vizuri  fedha watakazokuwa wanapewa na halmashauri.Pia amewaasa  kufuata sheria na taratibu za SACCOs katika kukopeshana na  sio kukopeshana  kwa urafiki au undugu  na kutoingiza siasa katika undeshaji wa SACCOs yao  kwani vyama vya ushirika havitaki siasa.

Akizungumza baada ya uzinduzi huo mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Kiteto ndugu Tamim Kambona  amempomngeza afisa ushirika kwa bidii aliionyesha  katika kuhakikisha usajili wa SACCOs ya vijana inakamilika kwa wakati.Pia amewapongeza  vijana kwa maamuzi mazuri ambayo wamefanya.Mkurugenzi amesema’’ Sisi kama halmashauri tunapata changamoto sana  kwenye ukopeshaji  wa fedha za vijana na wanawake,ndio maana mimi mwaka jana niliamua kubadili utaratibu, badala ya kutoa fedha tukawakopesha pikipiki vijana, lakini tumewakopesha hizo napo tumekutana na changamoto nyingine nyingi zaidi  mpaka sasa hivi tumefikia hatua ya  kunyang’anya zile pikipiki wengine.Sasa uanzishaji wa SACCOs kwa sababu  imesajiliwa rasmi na ina taratibu zake, ina katiba na kila kitu.Nafikiri sasa tumepata  sehemu ambayo ni salama zaidi.Na mimi nimewaambia hata wakuu wa idara  kwamba kuanzia sasa sitatoa fedha za mikopo  ile ya vijana tena kwenye vikundi,hiyo imekufa.Fedha zote za vijana ile asilimia tano tutapeleka kwenye SACCOs tu ya vijana.Kwa sababu ni SACCOs ya vijana na iko wilaya nzima,kwa hiyo tushauri vijana wote wale waliokuwa wagumu kujiunga katika vikundi,waje kujiunga na SACCOs.Wasipojiunga, ule utaratibu wa kuwapa pikipiki haupo tena.Kwa hiyo tunategemea kwamba kuanzia mwezi ujao tuanze kuwaingizia fedha na ninyi muanze kukopesha vijana wenzenu.Pia mkurugenzi amewataka vijana kutobweteka bali waongeze jitihada ili SACCOs yao iweze kuwa na mvuto zaidi.

Naye Afisa kilimo umwagiliaji na ushirika wa wilaya ya Kiteto ndugu  Robert Urassa  amewapongeza vijana kwa kuona umuhimu wa kujiunga na  SACCOs, na kutoa angalizo  kwamba  SACCOs  hiyo ni ya vijana na sio kikundi cha vijana,na kwamba SACCOs zina utaratibu wake, hivyo ni matumaini yake kwamba  watu wa maendeleo ya jamii hawataingilia utaratibu wa uendeshaji wa SACCOs hiyo kwani SACCOs ziko chini ya maafisa ushirika.Pia ndugu Urassa amesisitiza kwamba mpango wa halmashauri ni  fedha zote za vijana kupelekwa  kwenye SACCOs  na zitatolewa kulingana na taratibu na sheria za SACCOs, na  ana matumaini makubwa na SACCOs hiyo kwamba italeta manufaa makubwa kwa vijana na kuwawezesha kutekeleza azma ya hapa kazi tu .

Akitoa maelekezo kuhusu utaratibu wa uendeshaji wa SACCOs, Afisa ushirika ndugu Joseph Mwanga  amesema kwamba SACCOs hiyo imeanzishwa kisheria hivyo jambo lolote watakalo lifanya lazima wafuate sheria, watakapoamua kufanya kitu chochote kile,iwe ni  kupokea fedha au kutoa fedha kwa mwanachama  ,namna ya kukopesha imeandikwa katika sera ya mikopo na kwamba sheria zinazowasimamia  ziko ndani ya sheria ya vyama vya ushirika ambayo  imepititishwa na matawi ya vyama vya ushirika ,na ndiyo katiba yao,na kwamba  inasimama hata mahakamani kutoa maamuzi kwenye mambo ambayo watayafanya. Ndugu mwanga amesisitiza kwamba ni lazima wazingatie kile ambacho wamepewa, lakini pia katika kuandikishwa kuna  masharti na miongozo ambayo wamepewa, wamepewa kwa maandishi, waipitie wakishaipitia ndiyo itakayowaongoza nini wafanye na kwamba uongozi uliopo ni wa mpito, sheria inasema kwamba uongozi uliopo sasa ni uongozi wa mpito , wameandikiwa kwamba lazima waingie kwenye mchakato wa kuchagua uongozi rasmi, ambao  utakuwa ni uongozi baada ya kuandikishwa. Na ndiyo utakaofanya shughuli zote za kisheria  zinazotambulika ambazo zipo ndani ya utaratibu wa sheria mama ya ushirika.Baada ya kujaza fomu uongozi huo utavunjwa rasmi  na utachaguliwa uongozi ambao upo ndani ya utaratibu wa vyama vya ushirika.

Katika hatua nyingine afisa maendeleo ya jamii anayeshughulika na vijana ndugu Rodrick Kidenya aliwasilisha ombi la vijana kwa mkurugenzi wa halmashauri ya Kiteto la kuwa mlezi wa SACCOs ,ombi ambalo Mkurugenzi alisema ‘’nimelipokea kwa mikono miwili,na kwa sababu kazi hii mmenikabidhi mimi, sitaki lelemama, sitaki usanii usanii ,tusimame  kweli ili ifahamike kitaifa kwamba kweli Kiteto kuna SACCOs ya vijana , nitahakikisha fedha zenu zinakuja kwa wakati’’.

SACCOs  hiyo  itaendeshwa kwa mujibu wa sheria na taratibu zilizowekwa , kwa sasa SACCOs ina uongozi wa muda ambao uliteuliwa ili kuhakikisha kwamba inasimama, hivyo baada ya uzinduzi  na ujazaji wa fomu, uongozi kamili utateuliwa ambapo kutakuwa na bodi, kamati  ya SACCOs,meneja na mhudumu .

                                                                                                                                                                                                                                     

Matangazo

  • TANGAZO NAFASI ZA KAZI July 23, 2021
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI NAFASI YA UTENDAJI WA KIJlJI III August 26, 2021
  • TANGAZO LA KUKODISHA VIBANDA March 01, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI SEPTEMBA 2023 September 03, 2023
  • Angalia zote

Habari mpya

  • TABIA MBAYA ZA WATUMUSHI ZINAHARIBU SIFA ZA TAASISI

    May 01, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI KITETO LIMEMPONGEZA RAIS SAMIA.

    May 30, 2025
  • PONGEZI KWA WANANCHI KWA KUTUNZA MAZINGIRA

    April 28, 2025
  • TUUENZI MUUNGANO WETU

    April 27, 2025
  • Angalia zote

Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.

MWENGE MAKABIDHIANO MKOA WA MANYARA 2018
Video Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Hati ya Mshahara

Viunganishi vya Tovuti Nyingine

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • MANYARA
  • NECTA
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Kibaya-Kiteto

    Anwani ya Posta: P.o.Box 98, Kibaya-Kiteto

    Simu ya Mezani: +255 027-2552099

    Simu ya kiganjani:

    Barua Pepe: ded@kitetodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki@2017 Halimashauri ya Kiteto.Haki zote zimehifadhiwa