• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe watumishi |
    • Malalamiko |
Kiteto District Council
Kiteto District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Teknolojia,Habari ,Mawasiliano na Mahusiano
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Uchimbaji Madini
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Ardhi na Maliasili
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • This page is under construction
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi mipya
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Halmashauri ya wilaya ya Kiteto yajenga uzio wa hospitali ya wilaya

Imetumwa : October 9th, 2017

                    

                                                                                                                                                                                                                                                                                                                              

                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                  Uzio wa hospitali ya wilaya ya Kiteto  unaojengwa na halmashauri ya wilaya ya Kiteto unavyoonekana pande zote

                                                                                                                                                 

                                                                 Halmashauri ya wilaya ya Kiteto yajenga uzio wa hospitali ya wilaya


Halmashauri ya wilaya ya kiteto inajenga uzio wa hospitali ya wilaya.Uzio huo ambao  kwa kiasi kikubwa uko katika hatua za mwisho,unajengwa kwa kutumia mapato ya ndani ya halmashauri .


Mganga mkuu wa hospitali ya wilaya ya Kiteto  daktari Ramadhani Maingu amesema kwamba uzio huo utakapokamilika  utaimarisha ulinzi katika eneo la hospitali kwani kwa hali ilivyo sasa watu wamekuwa wakiingia na kutoka eneo la hospitali kwa kupitia maeneo yaliyo wazi , hivyo kuhatarisha usalama wa mali za hospitali na kuleta usumbufu kwa watumishi wa hospitali hiyo wakati wakitekeleza majukumu yao. Pia  baadhi ya wagonjwa  wamekuwa wakitoroka  hospitali kwa kupitia maeneo hayo .

Aidha Katibu wa afya wa  wilaya ya  Kiteto ndugu Dia Ally  amesema kwamba  uzio huo wa hospitali ni muhimu sana katika kudhibiti maambukizi kwani bila ya kuwa na uzio wanyama kama mbwa wanakuchukua taka hatarishi na kuzipeleka kwenye makazi ya watu jambo ambalo linaweza kusababisha maambukizi ya magonjwa.Kadhalika watoto wanaokota taka hizo,hali ambayo ni hatari kwani inaweza  kuwasababishia maambukizi ya magonjwa. Vilevile  Katibu  wa afya wa wilaya amesema kwamba uzio huo utasaidia katika kudhibiti watu kuingia maeneo ya hospitali nje ya muda maalumu uliowekwa, kwani  watu wanaokuja kuangalia wagonjwa wanatakiwa kuingia hospitali kwa muda maalum ili kutoa nafasi  kwa watumishi kuweza kutekeleza majukumu yao  kwa utulivu.

Nao Wauguzi  wa hospitali ya wilaya ya Kiteto walipohojiwa kwa nyakati tofauti wamesema kwamba wamefurahishwa sana na ujenzi wa uzio huo, kwani utakapokamilika utasaidia kuondoa usumbufu wa ndugu na jamaa ambao wamekuwa wakiingia wodini kuwaona wagonjwa  katika muda usioruhusiwa kwa kupitia  maeneo yasiyokuwa na uzio.Pia kukamilika kwa uzio huo kutaongeza usalama wa vifaa vya hospitali hiyo.

Katika hatua nyingine walinzi wa hospitali hiyo wamesema kwamba wanashukuru sana kwa ujenzi wa uzio huo kwani utakapokamilika  utasaidia kuondoa adha wanayoipata sasa ya watu kuingia katika maeneo ya hospitali bila utaratibu hususani nyakati za usiku, jambo ambalo linahatarisha usalama wa wagonjwa na mali za hospitali na linaleta usumbufu mkubwa sana kwa wagonjwa na  kwao pia.

Ujenzi huo ambao unaendelea kwa kasi kubwa, mpaka sasa umegharimu  kiasi cha shilingi milioni ishirini na laki tano(2,500,000).Hata hivyo ujenzi wa Uzio  huo pamoja na miradi mingine inayoendelea kutekelezwa wilayani Kiteto inatokana na jitihada za Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Kiteto ndugu Tamimu Kambona ambaye amedhamiria kuleta maendeleo ya kweli wilayani kiteto akishirikiana na wakuu wa idara za halmashauri ya wilaya ya Kiteto . 

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA 11.06.2025 June 11, 2025
  • TANGAZO NAFASI YA KAZI- MWENYEKITI BODI YA MFUKO WA ELIMU June 08, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI JUNI 2025 June 07, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 06, 2025
  • Angalia zote

Habari mpya

  • HAYAWI HAYAWI SASA YAMEKUA: HATIMAYE KALOLENI YAPATA SHULE MPYA YA MSINGI

    July 30, 2025
  • SHULE YA MSINGI KINANGALI NAYO YANUFAIKA NA MRADI WA BOOST

    July 30, 2025
  • SERIKALI YA AWAMU YA SITA YAENDELEA KUWEKEZA KWA VITENDO: KURASH YAPATA MRADI MWINGINE WA MILIONI 153 KUPITIA BOOST

    July 30, 2025
  • KATA YA BWAWANI YAPATA MRADI WA SHULE MPYA YA ELIMU MSINGI.

    July 28, 2025
  • Angalia zote

Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.

MWENGE MAKABIDHIANO MKOA WA MANYARA 2018
Video Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Hati ya Mshahara

Viunganishi vya Tovuti Nyingine

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • MANYARA
  • NECTA
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Kibaya-Kiteto

    Anwani ya Posta: P.o.Box 98, Kibaya-Kiteto

    Simu ya Mezani: +255 027-2552099

    Simu ya kiganjani:

    Barua Pepe: ded@kitetodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki@2017 Halimashauri ya Kiteto.Haki zote zimehifadhiwa