• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe watumishi |
    • Malalamiko |
Kiteto District Council
Kiteto District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Teknolojia,Habari ,Mawasiliano na Mahusiano
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Uchimbaji Madini
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Ardhi na Maliasili
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • This page is under construction
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi mipya
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Halmashauri ya wilaya ya Kiteto yapata makamu mwenyekiti mpya

Imetumwa : September 1st, 2017


                                                                                                                                               

Makamu mwenyekiti aliyemaliza muda wake Mh. Yahya Masumbuko akibadilishana joho na makamu mwenyekiti mteule Mh. Hassan Benzi mara baada ya  uchaguzi uliofanyika  katika kikao cha baraza la madiwani la halmashauri ya wilaya ya Kiteto

  Makamu mwenyekiti aliyemaliza muda wake Mh. Yahya Masumbuko akiwashukuru wajumbe wa baraza la madiwani la halmashauri ya wilaya ya Kiteto na kumkaribisha makamu mwenyekiti mpya mara baada ya uchaguzi uliowezesha kupatikana kwa  makamu mwenyekiti mpya wa halmashauri ya wilaya ya Kiteto

Mkuu wa wilaya ya Kiteto Mh. Tumaini Magessa  akitoa maelekezo ya Serikali  katika kikao cha baraza la madiwani la halmashauri ya wilaya ya Kiteto.Mkuu wa wilaya alikuwa mgeni rasmi katika kikao hicho .


Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Kiteto  Mh. Lairumbe Mollel akizungumza  na wajumbe wa baraza la madiwani  la Halmashauri ya wilaya ya Kiteto


Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Kiteto Ndg. Tamim  Kambona  akifafanua jambo katika kikao cha baraza la madiwani la halmashauri ya wilaya ya Kiteto


Mbunge wa jimbo la Kiteto Mh.Emmanuel Papian akichangia hoja katika  kikao cha baraza la madiwani la Halmashauri ya wilaya ya Kiteto


Wajumbe wa baraza la madiwani la halmashauri ya wilaya ya Kiteto wakipiga kura kuchagua makamu mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Kiteto



Wajumbe wa baraza la madiwani la halmashauri ya wilaya ya Kiteto wakifuatilia kwa makini taarifa za kamati  za halmashauri.


Mweka hazina wa wilaya ya Kiteto Ndg. Nassoro Mkwanda akiwasilisha taarifa ya mapato na matumizi katika kikao cha baraza la madiwani la Halmashauri ya wilaya ya Kiteto.

Afisa utumishi wa wilaya ya Kiteto Ndg. Rafael Makoninde akiwasilisha hoja za watumishi katika baraza la madiwani la Halmashauri ya wilaya ya Kiteto


HABARI KAMILI

Halmashauri ya wilaya ya Kiteto yapata makamu mwenyekiti  mpya

Halmashauri ya wilaya ya Kiteto imepata makamu mwenyekiti mpya baada ya uchaguzi uliofanyika katika  Kikao cha baraza la madiwani  cha tarehe 29 na 30 Agosti 2017.Katika kikao hicho ajenda kuu ilikuwa ni uchaguzi wa makamu mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Kiteto ambapo vyama vya CUF na CHADEMA  vinavyounda ukawa  havikuweka mgombea, hivyo mgombea wa CCM mheshimiwa Hassan  Benzi  akachaguliwa kuwa makamu mwenyekiti wa halmashari kwa kura 30 kati ya kura 31 zilizopigwa.


 Aidha mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya kiteto mheshimiwa Lairumbe Mollel aliwatangaza  diwani wa Sunya mheshimiwa Musa Brighton kuwa mwenyekiti wa kamati ya huduma za jamii,diwani wa Partimbo Paul Tunyoni  kuwa mwenyekiti wa kamati ya uchumi ,ujenzi  na mazingira na diwani wa lengatei Mainge Lemalali  kuwa mwenyekiti wa kamati ya maadili.
Katika wajumbe wanne wanaoteuliwa na mwenyekiti,mheshimiwa Mollel aliwateua mheshimiwa Nganisi Meshack,mheshimiwa Rehema Chileleo,mheshimiwa Yahaya Masumbuko na mheshimiwa Kidawa  Iyavu.Mheshimiwa Mollel aliwataka madiwani kuhakikisha wanasimamia miradi  ya maendeleo  inayofanyika kwenye kata zao,ili iendane na thamani ya fedha zinazotumika.Pia aliwataka watendaji wa serikali  kukusanya mapato.


Katika hatua nyingine mgeni rasmi katika kikao hicho mkuu wa wilaya ya Kiteto Mheshimiwa Tumaini Magesa  aliwataka waheshimiwa madiwani na watumishi wote wa umma kujiandaa vema kuupokea mwenge wa uhuru ambao utapokelewa wilayani Kiteto tarehe 13/09/2017. Mkuu wa wilaya pia  alielekeza juu ya matumizi bora ya ardhi ,kwamba kila kijiji kiweke mpango wa matumizi bora ya ardhi,na kwamba kinapoweka mpango huo kishirikishe  vijiji vya jirani ili kuondoa kutofautiana katika matumizi na kuleta migogoro baina ya vijiji.Pia alitoa maelekezo juu ya kuwepo na madaftari ya wakazi , kila kijiji kiwe kinaandikisha wakazi wake katika daftari ili  kuwatambua wakazi wa eneo husika na  kuwabaini wageni wanaoingia vijijini na kuvamia maeneo.


Mkuu wa wilaya ametoa angalizo kuhusu sumukuvu,kwamba inatishia maisha ya watu  kwani watoto watano wameathirika na sumu kuvu ambapo watatu kati yao walifariki, kuwaelekeza madiwani kuwasisitiza  wananchi wao kufuata taratibu walizoelekezwa  na wataalamu katika kuhifadhi mazao yao ya chakula.Mkuu wa wilaya pia amezungumzia kuhusu ukosefu wa shule  katika vijiji viwili ndani ya halmashauri ya wilaya ya kiteto ambavyo ni kijiji cha Lareg na Ngapapa,ambapo ameelekeza kwamba baada ya ujio wa  mwenge  madiwani wote pamoja na yeye mkuu wa wilaya kufanya ziara katika vijiji hivyo ili kujionea hali halisi na kuweka mikakati ya kujenga shule katika maeneo hayo.Kuhusu suala la mimba mashuleni, mkuu wa wilaya  amesema kwamba bado ni changamoto kwani  katika mwaka 2016 /2017  jumla ya wanafunzi 156 waliacha shule kutokana na kupata mimba hivyo amewataka madiwani kushirikiana naye katika mapambano ya kuondoa tatizo hilo kwa kukemea vitendo vinavyosababisha  mimba mashuleni kuendelea  katika kata zao.


Aidha shughuli za kawaida za baraza ziliendelea  kulingana na ajenda zilizokuwepo ambapo  taarifa  ya utekelezaji wa miradi  ya maendeleo  kutoka  kwenye kata kwa robo ya nne  April – June 2017) zilipokelewa, zilisomwa na kuthibitishwa .Muhtasari wa mkutano  wa kawaida wa halmashauri uliopita ulisomwa na kuthibitishwa . Maswali  yalijibiwa kufuatana na kanuni ya 21 ya kanuni za mikutano ya halmashauri. Taarifa za kamati  ; kamati ya fedha, uongozi na mipango,kamati ya huduma za jamii (elimu, afya na maji) na kamati ya huduma za uchumi(ujenzi,mazingira,kilimo na mifugo) zilipokelewa kutoka kwa wenyeviti wa kamati na kujadiliwa.Kila kamati ilitoa taarifa yake   na ilipokelewa ,ilijadiliwa na kupitishwa.


Matangazo

  • TANGAZO NAFASI ZA KAZI July 23, 2021
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI NAFASI YA UTENDAJI WA KIJlJI III August 26, 2021
  • TANGAZO LA KUKODISHA VIBANDA March 01, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI SEPTEMBA 2023 September 03, 2023
  • Angalia zote

Habari mpya

  • TABIA MBAYA ZA WATUMUSHI ZINAHARIBU SIFA ZA TAASISI

    May 01, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI KITETO LIMEMPONGEZA RAIS SAMIA.

    May 30, 2025
  • PONGEZI KWA WANANCHI KWA KUTUNZA MAZINGIRA

    April 28, 2025
  • TUUENZI MUUNGANO WETU

    April 27, 2025
  • Angalia zote

Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.

MWENGE MAKABIDHIANO MKOA WA MANYARA 2018
Video Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Hati ya Mshahara

Viunganishi vya Tovuti Nyingine

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • MANYARA
  • NECTA
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Kibaya-Kiteto

    Anwani ya Posta: P.o.Box 98, Kibaya-Kiteto

    Simu ya Mezani: +255 027-2552099

    Simu ya kiganjani:

    Barua Pepe: ded@kitetodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki@2017 Halimashauri ya Kiteto.Haki zote zimehifadhiwa