• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe watumishi |
    • Malalamiko |
Kiteto District Council
Kiteto District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Teknolojia,Habari ,Mawasiliano na Mahusiano
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Uchimbaji Madini
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Ardhi na Maliasili
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • This page is under construction
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi mipya
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

MSIMAMIZI WA UCHAGUZI KITETO AWAASA MAKARANI KUTOKUA CHANZO CHA MALALAMIKO.

Imetumwa : October 25th, 2025



Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Kiteto, Ndg. Ally Kichuri, amewataka Makarani Waongozaji Wapiga Kura kuhakikisha wanajiepusha kuwa chanzo cha malalamiko kutoka kwa vyama vya siasa na badala yake kushirikiana kwa karibu na mawakala wa vyama hivyo katika vituo vya kupigia kura.


Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo kwa makarani waongozaji wapiga kura, wasimamizi wa vituo na wasaidizi wao, yaliyofanyika Oktoba 25, 2025, Ndg. Kichuri alisema ni muhimu watendaji hao wa muda wa uchaguzi wakatenda haki na kuzingatia maadili ili kulinda taswira ya Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC).


 “Ni wajibu wenu kuhakikisha mnafanya kazi kwa weledi, uadilifu na ushirikiano mzuri na mawakala wa vyama vya siasa. Msigeuke kuwa chanzo cha malalamiko au migogoro katika vituo vya kupigia kura,” alisema Kichuri.


Aidha, aliwahimiza makarani hao kusoma kwa umakini Katiba, Sheria, Miongozo na Maelekezo yatakayotolewa na Tume, ili wawe na uelewa mpana wa majukumu yao.



Ndg. Kichuri pia aliwataka makarani hao kufanya kazi kwa ushirikiano, kuhakiki vifaa vya uchaguzi watakavyokabidhiwa na kuhakikisha wanawahi kwenye vituo vyao siku ya uchaguzi.


Mafunzo hayo ya siku tatu yameanza kwa kundi la makarani Oktoba 25, 2025, na yataendelea kwa wasimamizi wa vituo na wasaidizi wao kuanzia Oktoba 26 hadi 27, 2025.


Kabla ya mafunzo hayo kuanza, makarani hao  walikula kiapo cha kutunza siri na kiapo cha kujitoa uanachama kwenye vyama vya siasa.


Mafunzo hayo ambayo yamejumuisha makarani 598,  yamefanyika katika vituo vinne tofauti ambavyo ni Maktaba Kibaya, Kiteto Sekondari, Engusero na Lesoit, ambapo washiriki wamepatiwa mafunzo ya vitendo na maelekezo ya msingi ya jinsi ya kusimamia zoezi la upigaji kura kwa amani na utulivu.

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA MAPOKEZI YA FEDHA SEPTEMBA 2025 September 16, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU September 01, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI September 01, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI JUNI 2025 June 07, 2025
  • Angalia zote

Habari mpya

  • MSIMAMIZI WA UCHAGUZI KITETO AWAASA MAKARANI KUTOKUA CHANZO CHA MALALAMIKO.

    October 25, 2025
  • WAZEE WAHIMIZWA KUJITOKEZA KWA WINGI KUPIGA KURA OKTOBA 29

    October 07, 2025
  • KATIBU MKUU WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI AKABIDHI VIFAA NA CHANJO YA KICHAA CHA MBWA KITETO

    September 29, 2025
  • WITO WA LEO SEPTEMBA 29,2025

    September 29, 2025
  • Angalia zote

Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.

MWENGE MAKABIDHIANO MKOA WA MANYARA 2018
Video Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Hati ya Mshahara

Viunganishi vya Tovuti Nyingine

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • MANYARA
  • NECTA
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Kibaya-Kiteto

    Anwani ya Posta: P.o.Box 98, Kibaya-Kiteto

    Simu ya Mezani: +255 027-2552099

    Simu ya kiganjani:

    Barua Pepe: ded@kitetodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki@2017 Halimashauri ya Kiteto.Haki zote zimehifadhiwa