• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe watumishi |
    • Malalamiko |
Kiteto District Council
Kiteto District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Teknolojia,Habari ,Mawasiliano na Mahusiano
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Uchimbaji Madini
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Ardhi na Maliasili
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • This page is under construction
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi mipya
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

MHE. REMIDIUS MWEMA AONGOZA MATEMBEZI YA AMANI KUHAMASISHA WANANCHI KITETO KUPIGA KURA

Imetumwa : October 27th, 2025

Mkuu wa Wilaya ya Kiteto, Mhe. Remidius Mwema, leo Oktoba 27, 2025 ameongoza Matembezi ya Amani yaliyolenga kuhamasisha wananchi kujitokeza kwa wingi kupiga kura kwa amani na utulivu kuelekea Uchaguzi Mkuu  Oktoba 29, 2025.


Akizungumza baada ya matembezi hayo, Mhe. Mwema alisema matembezi hayo  yalilenga kuelimisha umma kuhusu umuhimu wa kushiriki katika mchakato wa kidemokrasia kwa kufuata misingi ya kikatiba.


“Huu ni uchaguzi wa wote, na kupiga kura ni haki ya kikatiba ya kila Mtanzania mwenye sifa. Ni wajibu wetu kujitokeza kwa amani na utulivu kuchagua viongozi wetu,” alisema Mhe. Mwema.


Aidha aliwapongeza wananchi kwa mwitikio mkubwa, akibainisha kuwa mwamko huo unaonesha uzalendo na umoja wa wana Kiteto. Pia aliwataka viongozi wa dini, taasisi na jamii kuendelea kuhamasisha wananchi wengine hadi siku ya uchaguzi.


Aidha, aliwakumbusha wananchi kuzingatia taratibu za uchaguzi ikiwemo kukaa umbali wa mita 500 kutoka kituo cha kupigia kura baada ya kupiga kura, na kusisitiza kuwa usalama uko imara katika Wilaya nzima ya Kiteto.


 “Hakuna sababu ya kuwa na hofu. Vyombo vya ulinzi vipo tayari kuhakikisha kila mwananchi anapiga kura kwa amani na utulivu. Kiteto ni salama,” alisisitiza.

Mhe. Mwema alitoa wito kwa wananchi kuepuka matumizi mabaya ya mitandao ya kijamii na kutoa taarifa kwa vyombo husika pindi wanapobaini dalili za uvunjifu wa amani.


Matembezi hayo yalihudhuriwa na viongozi wa dini, watumishi wa umma na sekta binafsi na makundi mbalimbali ya kijamii, yalianzia Shule ya Msingi Boma Sidan na kuhitimishwa katika Uwanja wa Michezo Kibaya kwa mazoezi ya viungo na michezo mbalimbali.


"KURA YAKO HAKI YAKO, JITOKEZE KUPIGA KURA"

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA MAPOKEZI YA FEDHA SEPTEMBA 2025 September 16, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU September 01, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI September 01, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI JUNI 2025 June 07, 2025
  • Angalia zote

Habari mpya

  • "KURA YAKO HAKI YAKO, JITOKEZE KUPIGA KURA"

    October 27, 2025
  • MHE. REMIDIUS MWEMA AONGOZA MATEMBEZI YA AMANI KUHAMASISHA WANANCHI KITETO KUPIGA KURA

    October 27, 2025
  • WASIMAMIZI WA VITUO WAHIMIZWA KUZINGATIA UADILIFU NA UWAZI WAKATI WA UCHAGUZI

    October 26, 2025
  • MSIMAMIZI WA UCHAGUZI KITETO AWAASA MAKARANI KUTOKUA CHANZO CHA MALALAMIKO.

    October 25, 2025
  • Angalia zote

Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.

MWENGE MAKABIDHIANO MKOA WA MANYARA 2018
Video Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Hati ya Mshahara

Viunganishi vya Tovuti Nyingine

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • MANYARA
  • NECTA
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Kibaya-Kiteto

    Anwani ya Posta: P.o.Box 98, Kibaya-Kiteto

    Simu ya Mezani: +255 027-2552099

    Simu ya kiganjani:

    Barua Pepe: ded@kitetodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki@2017 Halimashauri ya Kiteto.Haki zote zimehifadhiwa