• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe watumishi |
    • Malalamiko |
Kiteto District Council
Kiteto District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Teknolojia,Habari ,Mawasiliano na Mahusiano
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Uchimbaji Madini
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Ardhi na Maliasili
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • This page is under construction
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi mipya
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

‘‘Hatutaki Kuwa Tegemezi ’’ Mwenyekiti Kiteto DC

Imetumwa : March 28th, 2018

Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Kiteto Mhe. Lairumbe Mollel akiongoza kikao cha baraza la madiwani kilichofanyika katika ukumbi wa halmashauri ya wilaya ya Kiteto. Upande wake wa kulia ni makamu mwenyekiti  wa halmashauri Mhe. Hassan Benzi na upande wake wa kushoto ni Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri Ndg. Tamim Kambona.

Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Kiteto Mhe. Lairumbe Mollel , makamu mwenyekiti  wa halmashauri Mhe. Hassan Benzi na Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri Ndg. Tamim Kambona wakifuatilia kwa makini uwasilishwaji wa taarifa za maendeleo ya kata katika kikao cha baraza la madiwani kilichofanyika katika ukumbi wa halmashauri.

Wahe. Madiwani wakiwa katika Kikao cha baraza la madiwani  ndani ya ukumbi wa halmashauri.



Wahe. Madiwani wakiwasilisha taarifa za maendeleo ya kata zao katika kikao cha baraza la madiwani la  halmashauri  ya wilaya ya Kiteto  kilichofanyika katika ukumbi wa halmashauri .

Wataalamu kutoka idara mbalimbali za halmashauri ya wilaya ya Kiteto wakiwa  katika kikao cha baraza la madiwani kilichofanyika katika ukumbi wa halmashauri



.......... HABARI KAMILI ..........

Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Kiteto mheshimiwa Lairumbe Mollel amewataka Wahe. madiwani  kuhakikisha wanajenga vituo vya afya katika kata zao, ili wilaya  isiwe tegemezi katika huduma za afya.Mhe Mollel ameyasema hayo wakati akiongoza kikao cha baraza la madiwani  kilichofanyika katika ukumbi wa halmashauri  mapema leo .


Mheshimiwa Mollel amesema kwamba yeye binafsi hajisikii vizuri kuona kwamba wananchi wa wilaya ya Kiteto wanakwenda kupata huduma za afya nje ya wilaya kwa sababu tu hakuna vituo vya afya katika maeneo yao hali ya kuwa uwezo wa kujenga vituo vya afya upo.


Akisisitiza kuhusu ujenzi wa vituo vya afya , Mhe. Mollel amesema ‘‘Tunataka wilaya yetu hii isiwe tegemezi,wananchi wetu wanakata CHF halafu wanakwenda kutibiwa nje ya wilaya.Huduma zinaigiliana ,lakini na sisi tujitahidi kwa nguvu zetu, ili watu waje kwetu badala ya sisi kwenda kwao kila wakati. Shida ni kuanzisha ujenzi wa kituo cha afya tu, tukishajenga serikali inaleta hela inamalizia ujenzi, wananchi wetu wanakuwa na huduma ndani ya maeneo yao’’.


Kadhalika Mhe. Mollel amewataka madiwani kujipanga kutekeleza miradi ya maendeleo katika kata zao kwa wakati uliopo. Akisisitiza kuhusu hilo Mhe. Mollel amesema ‘‘Jamani tuna muda mchache sana wa kufanya kazi za maendeleo katika kata zetu.Tunaelekea kwenye uchaguzi, tutachagua kamati ya siasa, tutaenda kuchagua wenyeviti wa vijiji, serikali za mitaa ,tutashindwa kufanya  miradi mwakani, kwa hiyo niwaombe sana  hilo muwe nalo.Tujipange kwa sasa .Vibali vinatolewa kwa DC kwa ajili ya michango,zile kamati za ukusanyaji tuziandae kuanzia sasa,ili hata mwezi wa 5 na wa 6 umeshapata kibali unaendelea kufanya kazi’’.


Kikao hicho cha baraza la madiwani  kimekuwa na ajenda moja tu ambayo ni kuwasilisha taarifa za maendeleo ya kata ambapo waheshimiwa madiwani kutoka katika kata zote 23 wamewasilisha taarifa za maendeleo ya kata zao.



.......... MWISHO..........

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA 11.06.2025 June 11, 2025
  • TANGAZO NAFASI YA KAZI- MWENYEKITI BODI YA MFUKO WA ELIMU June 08, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI JUNI 2025 June 07, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 06, 2025
  • Angalia zote

Habari mpya

  • HAYAWI HAYAWI SASA YAMEKUA: HATIMAYE KALOLENI YAPATA SHULE MPYA YA MSINGI

    July 30, 2025
  • SHULE YA MSINGI KINANGALI NAYO YANUFAIKA NA MRADI WA BOOST

    July 30, 2025
  • SERIKALI YA AWAMU YA SITA YAENDELEA KUWEKEZA KWA VITENDO: KURASH YAPATA MRADI MWINGINE WA MILIONI 153 KUPITIA BOOST

    July 30, 2025
  • KATA YA BWAWANI YAPATA MRADI WA SHULE MPYA YA ELIMU MSINGI.

    July 28, 2025
  • Angalia zote

Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.

MWENGE MAKABIDHIANO MKOA WA MANYARA 2018
Video Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Hati ya Mshahara

Viunganishi vya Tovuti Nyingine

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • MANYARA
  • NECTA
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Kibaya-Kiteto

    Anwani ya Posta: P.o.Box 98, Kibaya-Kiteto

    Simu ya Mezani: +255 027-2552099

    Simu ya kiganjani:

    Barua Pepe: ded@kitetodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki@2017 Halimashauri ya Kiteto.Haki zote zimehifadhiwa