• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe watumishi |
    • Malalamiko |
Kiteto District Council
Kiteto District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Teknolojia,Habari ,Mawasiliano na Mahusiano
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Uchimbaji Madini
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Ardhi na Maliasili
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • This page is under construction
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi mipya
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

HAYAWI HAYAWI SASA YAMEKUA: HATIMAYE KALOLENI YAPATA SHULE MPYA YA MSINGI

Imetumwa : July 30th, 2025

Wahenga walisema "Hayawi hayawi sasa yamekua". Kile kilio cha muda mrefu cha wananchi wa kata ya Kaloleni cha kupata shule mpya ya msingi sasa kimesikiwa na hatimaye kata hiyo inaenda kupata shule yenye thamani ya shilingi milioni 330.7 kutoka serikali kuu kupitia programu ya BOOST.


Akizungumza siku ya Julai 29,2025 mbele ya wananchi wa kata hiyo Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri Ndg. Erasmo Tellun Ndelwa amesema kwamba katika mwaka wa fedha 2025/26 halmashauri imepokea kiasi hicho cha fedha kwaajili ya  mradi wa ujenzi wa miundombinu muhimu ya shule ikiwa ni pamoja na: madarasa sita (06) ya elimu ya msingi, madarasa mawili (02) ya mfano kwa elimu ya awali, matundu ya vyoo sita (06) kwa wanafunzi wa elimu ya msingi na matundu sita(06) ya vyoo kwa wanafunzi wa awali.


Aidha, ujenzi huo utahusisha vyoo matundu mawili (02) kwaajili ya walimu pamoja na jengo moja la utawala.


Nae Afisa kutoka TAKUKURU Ndg. EliBrighton Mmari amesema kwamba taasisi hiyo itakua macho katika utekezaji wa mradi huo na amewaasa wananchi kuwa walinzi wa mradi huo.

"Kuna wananchi wamechaguliwa kwenye kamati za utekelezaji wa mradi huu lengo ni kuhakikisha  wananchi wanashiriki vizuri katika mradi pia kuongeza uwazi" Aliongeza Ndg. Mmari.


Nae Mkuu wa Wilaya ya Kiteto Mhe. Remidius Mwema Emmanuel amewaasa wajumbe wa kamati ya ujenzi wa mradi huo kuhakikisha wanawatafuta wazabuni ambao wana uwezo wa kuleta vifaa kwa wakati kwasababu ucheleweshwaji wa vifaa kutafanya mradi kutokamilika kwa wakati.


Sambamba na hayo alisisitiza juu ya mafundi na kutia mkazo kua wahakikishe wafundi wanaopewa tenda ni wale wenye uwezo.


"Sita sita kumchumkulia hatua yoyote atakaye leta mchezo kwenye mradi huu nawakumbusha Mafundi kuwa makini katika Utekelezaji wa Mradi huu alisisitiza Mhe. Mwema.


Mhe. Mwema aliwaeleza wananchi wa kata hiyo kua wamekua wakiomba shule kwa muda mrefu  na hatimaye serikali sikivu ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais. Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, imewapelekea fedha kwaajili ya ujenzi wa shule hiyo mpya.


"Tuna kila sababu ya kumshukuru Dr.  Samia kwa fedha hizi.", aliongeza Mhe. Mwema.


Nao wananchi wa kata hiyo walimuomba Mhe. Mwema kufikisha salamu zao za shukrani kwa Mheshimiwa Dkt. Samia kwa kuwatatulia kero hiyo ambayo imedumu kwa mda mrefu.


Kukamilika kwa ujenzi wa shule hii kutasaidia kupunguza msongamano wa wanafunzi katika shule ya Msingi Kaloleni.

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA 11.06.2025 June 11, 2025
  • TANGAZO NAFASI YA KAZI- MWENYEKITI BODI YA MFUKO WA ELIMU June 08, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI JUNI 2025 June 07, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 06, 2025
  • Angalia zote

Habari mpya

  • HAYAWI HAYAWI SASA YAMEKUA: HATIMAYE KALOLENI YAPATA SHULE MPYA YA MSINGI

    July 30, 2025
  • SHULE YA MSINGI KINANGALI NAYO YANUFAIKA NA MRADI WA BOOST

    July 30, 2025
  • SERIKALI YA AWAMU YA SITA YAENDELEA KUWEKEZA KWA VITENDO: KURASH YAPATA MRADI MWINGINE WA MILIONI 153 KUPITIA BOOST

    July 30, 2025
  • KATA YA BWAWANI YAPATA MRADI WA SHULE MPYA YA ELIMU MSINGI.

    July 28, 2025
  • Angalia zote

Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.

MWENGE MAKABIDHIANO MKOA WA MANYARA 2018
Video Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Hati ya Mshahara

Viunganishi vya Tovuti Nyingine

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • MANYARA
  • NECTA
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Kibaya-Kiteto

    Anwani ya Posta: P.o.Box 98, Kibaya-Kiteto

    Simu ya Mezani: +255 027-2552099

    Simu ya kiganjani:

    Barua Pepe: ded@kitetodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki@2017 Halimashauri ya Kiteto.Haki zote zimehifadhiwa