• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe watumishi |
    • Malalamiko |
Kiteto District Council
Kiteto District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Teknolojia,Habari ,Mawasiliano na Mahusiano
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Uchimbaji Madini
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Ardhi na Maliasili
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • This page is under construction
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi mipya
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Kamati ya Lishe Yataka Tahadhari Itolewe Dhidi ya Sumukuvu .

Imetumwa : September 5th, 2018

Mkuu wa idara ya maendeleo ya jamii (W) Ndg. Joseph Mwaleba akifungua kikao cha kamati ya lishe ya wilaya ya Kiteto kwa niaba ya Mkurugenzi mtendaji  .Aliyekaa upande wake wa kushoto ni mganga mkuu wa  wilaya ya Kiteto Dkt. Melkiadi Paschal Mbota.


Wajumbe wa kamati ya lishe ya wilaya ya Kiteto wakipitia kwa makini taarifa mbalimbali zilizomo kwenye mafaili,kabla ya kuanza kwa kikao.


Wajumbe wa kamati ya lishe ya wilaya ya Kiteto wakiendelea na kikao .Kikao cha kamati ya lishe kimefanyika katika ukumbi wa hospitali ya wilaya ya Kiteto  mapema jana.



.......HABARI KAMILI...........


 Kamati ya lishe ya wilaya ya Kiteto imezitaka idara ya kilimo, chakula na ushirika pamoja na idara ya mifugo na uvuvi  kwa kushirikiana na idara ya afya  kutoa tahadhari kuhusiana na sumukuvu.Azimio hilo limefikiwa katika kikao cha kamati  hiyo kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa hospitali ya wilaya ya Kiteto mapema jana.


Wakizungumza kwa nyakati tofauti, wajumbe wa kamati hiyo ,wamesema kwamba jamii ya Kiteto bado haina uelewa wakutosha kuhusu sumukuvu ,jambo ambalo linasababisha kuendelea kuhifadhi nafaka katika hali ambayo ni hatarishi kwa walaji wa nafaka hizo.


Wajumbe hao wamesema kwamba kumekuwepo na matumizi ya viuatilifu vya kuhifadhia nafaka ambavyo ni sumu, na viautilifu vingine ambavyo viko katika hali ya kimiminika (maji), viuatilifu hivi ambavyo viko katika hali ya kimiminika vikiwekwa katika nafaka,na nafaka hizo zisipokaushwa vizuri,zinakuwa na unyevu unyevu ambao husababisha nafaka hizo kutengenzeza sumu ijulikanayo  kama sumukuvu, vilevile  wakulima wengi wamekuwa na mazoea ya kuweka nafaka chini kwenye udongo, au kwenye sakafu, nafaka zinapowekwa chini kwenye udongo au kwenye sakafu, huvuta unyevu kutoka ardhini, unyevu huo hutengeneza ukungu katika nafaka, hali hiyo  husababisha  nafaka hizo kuwa na sumukuvu .


Akizungumza wakati wa majadiliano ,mganga mkuu wa wilaya ya Kiteto Daktari Malkiadi Paschal Mbota amesema” Sumukuvu bado ni tatizo kubwa ,jamii bado haina uelewa wa kutosha  katika kuhifadhi mazao yao,hususani nafaka kama mahindi, karanga na mtama ,ili mazao hayo yasiweze kupata sumukuvu,jambo ambalo ni hatari sana kwani madhara ya sumukuvu ni makubwa.Sumukuvu inapoingia mwilini kidogo kidogo,madhara yake  hayawezi kuonekana kwa mara moja,lakini  moja wapo ya madhara yanayoweza kuonekana baada ya muda mrefu ni  saratani ya ini”. 


Daktari Mbota pia amezungumzia kuhusu matumizi ya dawa zisizoruhusiwa  kama DDT ambazo baadhi ya wakulima wamekuwa wakizitumia kuweka katika nafaka zao ili zisishambuliwe na wadudu.Amesema kwamba dawa hizo zinapotumika , ni sumu , hivyo zina madhara makubwa sana katika miili ya walaji wa nafaka hizo.Hivyo jitihada za ziada zinahitajika  kuweza kuwajengea wakulima uelewa wa kutosha kuhusu madhara ya dawa hizo.


Kwa upande wake Mkuu wa idara ya Mifugo na uvuvi Daktari Wiliam Msuya amefafanua zaidi kuhusu sumukuvu , hapa daktari Msuya amesema “ Sumukuvu haiko kwenye nafaka peke yake,bali inaweza kuwepo hata kwenye nyama, pamoja na mazao ya mifugo kama vile maziwa, kutokana na mifugo kula vyakula ambavyo vina sumukuvu, hivyo jamii inapaswa pia kutahadharishwa kwamba mifugo inapokula mabua,au pumba ambazo zina sumukuvu, nyama  pamoja na mazao yake yote ambayo hutumika kama chakula kwa binadamu vyote vinaweza kuwa na sumu hiyo”.


Naye  mjumbe wa kamati ya lishe, mchungaji  wa kanisa la kiinjili la Kirutheri Tanzania ( KKKT)  usharika wa Kibaya ambaye amewakilisha viongozi wa madhehebu ya kikristo wilayani Kiteto, Mchungaji Wankembeta Marco Msingi amesema kwamba ni vema tahadhari ikatolewa mapema kuhusiana na sumukuvu,na namna ya kuiepuka, na kwamba wahusika wanaopaswa kutoa elimu pamoja na tahadhari hiyo watumie njia zozote zinazowezekana kwa haraka, ili kuepuka maangamizi yanayoweza kutokea kwa siku za usoni kutokana na ulaji wa vyakula ambavyo vina sumukuvu badala ya kukaa kusubiri bajeti.


Katika hatua nyingine mjumbe wa kamati ya lishe ambaye pia ni muwakilishi wa BAKWATA wilaya ya Kiteto,ndugu Ibrahim M. Bory ameitaka idara ya Kilimo,chakula na ushirika   kwa kushirikiana na idara ya afya, kupita na kukagua  bidhaa ya unga wa lishe unaotengenezwa na vikundi mbalimbali  pamoja na watu binafsi,kuhakikisha kama bidhaa hiyo ni salama kwa matumizi ya binadamu, lengo likiwa ni kuepuka madhara yanayoweza kuwapata watumiaji ,ambao kwa asilimia kuwa ni watoto.


Kamati ya lishe wilaya ya Kiteto imekaa kikao chake cha robo ya kwanza kwa mwaka wa fedha 2018/2019, ambapo taarifa za shughuli za lishe kutoka  BAKWATA, idara na vitengo mbalimbali vya halmashauri kama vile idara ya kilimo,chakula na ushirika, idara ya mipango, idara ya elimu msingi, idara ya elimu sekondari, idara ya mifugo na uvuvi, idara ya afya na usafi wa mazingira, idara ya maendeleo ya jamii, kitengo cha Afya ya uzazi na mtoto, Kitengo cha dawa na vifaa tiba pamoja na Kitengo cha lishe zimewasilishwa.



.............MWISHO...............

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA 11.06.2025 June 11, 2025
  • TANGAZO NAFASI YA KAZI- MWENYEKITI BODI YA MFUKO WA ELIMU June 08, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI JUNI 2025 June 07, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 06, 2025
  • Angalia zote

Habari mpya

  • MAFUNZO YA MFUMO WA E-UTENDAJI KWA WATUMISHI.

    June 12, 2025
  • KIKAO CHA MAANDALIZI YA MWENGE WA UHURU 2025

    June 11, 2025
  • WATOTO WA UMISSETA KITETO, WAWATOA JASHO WATU WAZIMA!

    June 10, 2025
  • WALIMU KITETO WAPEWA MAFUNZO YA AFUA JUMUISHI ZA ELIMU YA AFYA SHULENI

    June 05, 2025
  • Angalia zote

Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.

MWENGE MAKABIDHIANO MKOA WA MANYARA 2018
Video Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Hati ya Mshahara

Viunganishi vya Tovuti Nyingine

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • MANYARA
  • NECTA
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Kibaya-Kiteto

    Anwani ya Posta: P.o.Box 98, Kibaya-Kiteto

    Simu ya Mezani: +255 027-2552099

    Simu ya kiganjani:

    Barua Pepe: ded@kitetodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki@2017 Halimashauri ya Kiteto.Haki zote zimehifadhiwa