• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe watumishi |
    • Malalamiko |
Kiteto District Council
Kiteto District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Teknolojia,Habari ,Mawasiliano na Mahusiano
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Uchimbaji Madini
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Ardhi na Maliasili
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • This page is under construction
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi mipya
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

KATIBU MKUU WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI AKABIDHI VIFAA NA CHANJO YA KICHAA CHA MBWA KITETO

Imetumwa : September 29th, 2025

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Bi. Agnes Meena, amekabidhi vifaa vya kazi kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto, CPA. Hawa Abdul Hassan, katika kilele cha maadhimisho ya Siku ya Kichaa cha Mbwa Kitaifa yaliyofanyika leo Septemba 29,2025.


Vifaa vilivyokabidhiwa ni pamoja na vishikwambi 32 kwa ajili ya wataalamu wa mifugo pamoja na dozi 15,000 za chanjo ya Kichaa cha Mbwa. Hatua hii inalenga kuongeza ufanisi wa utoaji huduma za mifugo  kwa wananchi wa Kiteto na kuhakikisha chanjo za kichaa cha mbwa zinaendelea kutolewa ili kuilinda jamii na ugonjwa huu hatari.


Kupokelewa kwa vishikwambi hivyo kutarahisisha ukusanyaji na uhifadhi wa taarifa za mifugo, kufuatilia mwenendo wa utoaji chanjo, na kurahisisha mawasiliano kati ya wataalamu wa mifugo katika ngazi za kata, vijiji na wilaya. 


Aidha, upatikanaji wa dozi 15,000 za chanjo ya kichaa cha mbwa utaiwezesha Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto kuendelea kutoa chanjo hizo bure kwa wananchi wote. Utoaji huu wa chanjo bila malipo ni msaada mkubwa kwa jamii na utachochea mwitikio wa wananchi kuwachanja wanyama wao ili kuzuia maambukizi.


Huduma ya chanjo hiyo ya Kichaa cha Mbwa itaendelea kutolewa bure na wataalamu wa mifugo kupitia ofisi za kata na vijiji wilayani hapa ikiwa ni sehemu ya juhudi endelevu za serikali kuhakikisha kila mnyama anapata kinga.


Maadhimisho haya ya kitaifa yalilenga kuhamasisha jamii kuhusu umuhimu wa chanjo kama kinga bora dhidi ya Kichaa cha Mbwa na kuonesha dhamira ya Serikali katika kulinda afya za binadamu na wanyama.

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA MAPOKEZI YA FEDHA SEPTEMBA 2025 September 16, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU September 01, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI September 01, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI JUNI 2025 June 07, 2025
  • Angalia zote

Habari mpya

  • WAZEE WAHIMIZWA KUJITOKEZA KWA WINGI KUPIGA KURA OKTOBA 29

    October 07, 2025
  • KATIBU MKUU WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI AKABIDHI VIFAA NA CHANJO YA KICHAA CHA MBWA KITETO

    September 29, 2025
  • WITO WA LEO SEPTEMBA 29,2025

    September 29, 2025
  • TANZANIA YA TATU AFRIKA MPANGO RASMI WA KUDHIBITI KICHAA CHA MBWA

    September 29, 2025
  • Angalia zote

Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.

MWENGE MAKABIDHIANO MKOA WA MANYARA 2018
Video Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Hati ya Mshahara

Viunganishi vya Tovuti Nyingine

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • MANYARA
  • NECTA
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Kibaya-Kiteto

    Anwani ya Posta: P.o.Box 98, Kibaya-Kiteto

    Simu ya Mezani: +255 027-2552099

    Simu ya kiganjani:

    Barua Pepe: ded@kitetodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki@2017 Halimashauri ya Kiteto.Haki zote zimehifadhiwa