• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe watumishi |
    • Malalamiko |
Kiteto District Council
Kiteto District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Teknolojia,Habari ,Mawasiliano na Mahusiano
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Uchimbaji Madini
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Ardhi na Maliasili
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • This page is under construction
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi mipya
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Kijungu Watakiwa Kufuata Mpango wa Matumizi bora ya Ardhi

Imetumwa : September 4th, 2018

Mbunge wa jimbo la Kiteto Mhe. Emmanuel Papian akizungumza na wakazi wa kijiji cha Kijungu katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika uwanja wa ofisi ya kata ya kijungu.

Wakazi wa kijiji cha Kijungu wakiwa wamekusanyika kumsikiliza mbunge wao sambamba na kuwasilisha kero zao .



...........HABARI KAMILI...............



Mbunge wa jimbo la Kiteto Mheshimiwa Emmanuel Papian amewataka wakazi wa kijiji cha Kijungu kufuata mpango wa matumizi bora ya ardhi waliojiwekea  ili kuepuka migogoro ya ardhi ambayo imekuwa ikijitokeza mara kwa mara.Mhe. Papian ameyasema hayo wakati akizungumza na wakazi hao katika mkutano wa hadhara uliofanyika  katika  uwanja wa  ofisi ya kata ya Kijungu,wilayani Kiteto.



Akizungumza katika mkutano huo Mhe. Papian amesema  “Wananchi wa kijungu tuna tatizo la migogoro ya ardhi,tulizungumza hapa kama mnakumbuka ,wananchi mnatakiwa kuhakikisha kwamba mnafuata mpango wa matumizi bora ya ardhi, mnapokwenda kupata mwenyekiti,mnapokwenda kupata serikali ya kijiji, hakikisheni mnafuata mpango wa matumizi bora ya ardhi, na  muache udalali  wa kuuza maeneo, ili kuepuka migogoro isiyo ya lazima. Udalali wa maeneo umesababisha vijana ambao ni wazawa wa hapa kukosa maeneo ya kulima,kukosa maeneo ya kujenga”.


Aidha Mhe. Papian  ameahidi kushughulikia matatizo mbalimbali yanayowakabili wakazi wa kijiji hicho, Akisisitiza kuhusu kuhusu hilo Mhe. Papian  amesema “Hapa kuna matatizo mawili matatu,tatizo la kwanza ni chanzo cha maji, hakuna maji,na yaliyopo yako mbali.Hili tunalo ,tumekwenda nalo kwa Mkurugenzi,tunafanya jitihada kuhakikisha kwamba kwa pesa mliyonayo ya mfuko wa maji, na tutaangalia ni namna gani kwa kutumia mapato ya halmashauri ,tunaweza kufunga bomba kule, tusogeze bomba huku tuweke walau kichoteo kimoja,wananchi wapate maji”.


Kadhalika Mhe. Papian amezungumzia kuhusu suala la upungufu wa Mkunga,katika zahanati ya Kijungu, Mhe Papian amesema “  kuna upungufu wa muuguzi mkunga,katika ajira za serikali kwa mwaka 2018/2019  tutapata mtumishi mwingine hapa ili aweze kusaidiana na watumishi wengine walioko hapa, huduma ziendelee kwa salama”.


Mhe. Papian pia ameahidi kushughulikia suala la chumba cha kujifungulia na kitanda cha kujifungulia, ambapo amesema kwamba anafahamu kwamba eneo la wakina mama kujifungulia haliko sawasawa,ni dogo ,na kitanda cha kujifungulia hakiko vizuri , na kwamba jambo hilo wameshalifikisha kwa Mkurugenzi, watalifanyia kazi, eneo hilo litarekebishwa, na kitanda hicho kitapatikana.


Katika mkutano huo wakazi wa kata ya kijungu waliwasilisha kero zao, kero kubwa ikiwa ni ukosefu wa maeneo ya kujenga na maeneo ya kulima, ambapo Mhe. Papian amewataka wanachi hao kuwa watulivu wakati yeye pamoja na serikali ya wilaya wakiendelea kuangalia ni namna gani tatizo hilo linaweza kushughulikiwa,na wananchi hao kupata maeneo kwa ajili ya makazi na ya shughuli za kilimo.


Mhe. Papian amefanya ziara katika kijiji cha Kijungu ,ikiwa ni sehemu ya ziara zake katika jimbo lake kukagua shughuli za maendeleo na kusikiliza kero za wananchi .




..........MWISHO............

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA 11.06.2025 June 11, 2025
  • TANGAZO NAFASI YA KAZI- MWENYEKITI BODI YA MFUKO WA ELIMU June 08, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI JUNI 2025 June 07, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 06, 2025
  • Angalia zote

Habari mpya

  • MAFUNZO YA MFUMO WA E-UTENDAJI KWA WATUMISHI.

    June 12, 2025
  • KIKAO CHA MAANDALIZI YA MWENGE WA UHURU 2025

    June 11, 2025
  • WATOTO WA UMISSETA KITETO, WAWATOA JASHO WATU WAZIMA!

    June 10, 2025
  • WALIMU KITETO WAPEWA MAFUNZO YA AFUA JUMUISHI ZA ELIMU YA AFYA SHULENI

    June 05, 2025
  • Angalia zote

Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.

MWENGE MAKABIDHIANO MKOA WA MANYARA 2018
Video Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Hati ya Mshahara

Viunganishi vya Tovuti Nyingine

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • MANYARA
  • NECTA
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Kibaya-Kiteto

    Anwani ya Posta: P.o.Box 98, Kibaya-Kiteto

    Simu ya Mezani: +255 027-2552099

    Simu ya kiganjani:

    Barua Pepe: ded@kitetodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki@2017 Halimashauri ya Kiteto.Haki zote zimehifadhiwa