• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe watumishi |
    • Malalamiko |
Kiteto District Council
Kiteto District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Teknolojia,Habari ,Mawasiliano na Mahusiano
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Uchimbaji Madini
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Ardhi na Maliasili
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • This page is under construction
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi mipya
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Kikao cha Robo ya Tatu ya Mwaka wa Fedha 2016/2017 cha Baraza la Madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto Kilichoanza Leo Tarehe 16.05.2017 Hadi Tarehe 17.05.2017

Imetumwa : May 16th, 2017

Mh. Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto Lairumbe Mollel Akisoma Dua Kabla ya Kufungua Kikao.

Mkurugenzi Mtendaji (W) Bw. Tamim H. Kambona Akisalimia Wajumbe na Kumkaribisha Mh.Mwanyekiti Lairumbe Mollel 



Waheshimiwa Madiwani (waliovaa majoho ya rangi ya Damu ya Mzee) Wakiwa Katika Kikao. 

Wakuu wa Idara Wakifuatilia Kikao cha Baraza la Madiwani Kiteto

Ndipo Ilipofika Wakati wa Waheshimiwa Madiwani Kuwasilisha Taarifa za Miradi ya Maendeleo ya Kata Wanazotoka 

kwa Kipindi cha Robo Mwaka ya Tatu (Januari - Machi 2017)


 



Baadhi ya Waheshimiwa Madiwani Katika Uwasilisha wa Taarifa za Miradi ya Maendeleo ya Kata zao.

Kaimu Afisa Ardhi na Maliasili Wilaya Bw. Emmanuel Gulisha, Akitoa Ufafanuzi wa Kitaalamu kuhusu Ardhi katika Kikao

Afisa Mifugo na Uvuvi Wilaya Bw. William E. Msuya, Akitoa Ufafanuzi wa Kitaalamu Kuhusu  Usajili wa Masoko ya Mifugo (Minada)

Kaimu Mganga Mkuu wa Wilaya ya Kiteto Dr. G. Lupembe Akitoa Ufafanuzi wa Kitaalamu Katika Kikao


Ndipo Siku Iliyofuata Wenyeviti wa Kamati Mbalimbali Waliwasilisha Taarifa za ili Ziweze Kufanyiwa Kazi.

Mwenyekiti wa Kamati za Jamii Mh. Diwani kata ya Dosidosi,  Benzi Hassan Akiwasilisha Taarifa ya Kamati hiyo.

Mwenyekiti wa Kamati za Uchumi na Mazingira Mh. Diwani Paulo Tunyoni wa Kata ya Partimbo Akiwasilisha Taarifa Hiyo.

Mh. Diwani wa Kata ya Bwagamoyo (Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri) Akiwasilisha Taarifa hiyo ya Kamati ya Fedha na Mipango Kwaniaba ya Mwenyekiti wa Kamati hiyo.

TAARIFA KAMILI...

Katika Baraza hilo, majadiliano mbalimbali ya kikao yalikuwa ni kutilia mkazo juu ya usimamizi mzuri wa miradi ya maendeleo ya wananchi kwa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto. Ili kuleta matokeo chanya utaratibu wa namna ya kumpata Mkandarasi bora, ufuatiliaji  na usimamizi wa uhakika katika kutekeleza   mradi husika na ulipaji wa fedha kwa Mkandarasi  kwa kufuata taratibu za kisheria ndiyo suluhisho. Hata hivyo katika miradi mingi iliyooekana kufanya vizuri zingatio la mambo matatu tajwa hapo juu ndiyo yaliyozingatiwa hadi kupata miradi iliyo bora na inaoendana na thamani ya fedha iliyolipwa.

Uwasilishaji wa Taarifa za Kata Januari - Machi 2017.

Katika mawasilisho mbalimbali ya Waheshimiwa Madiwani takwimu zinaonyesha kuna idadi kubwa  ya wananchi wanaojiunga na Bima ya Afya ya Jamii ijulikanayo kama “Mfuko wa Afya ya Jamii Ulioboreshwa” ( iCHF ) ambapo lengo  ni kila mwananchi kupata huduma ya Afya popote katika Hospitali za Serikali na baadhi ya Hospitali Binafsi zilizoidhinishwa kwa gharama ndogo kwa mwaka mzima kwa kuchangia kiasi cha Shilingi (T) 30,000/=.  Kwa Kata 23 za Halmashauri ni safu ya watu kati ya 100 hadi 250 kwa makusanyo ya takribani milioni 3 hadi milioni 7 kwa kila Kata katika kipindi cha Januari hadi Machi 2017, katika hili Waheshimiwa Madiwani wamefanya hamasa kubwa kwa wananchi katika Kata zao.


Mkurugenzi Mtendaji (W) Kiteto Bw. Tamim Kambona akifafanua jambo kuhusu miradi katika Kikao cha Baraza hilo

Mkurugenzi Mtendaji (W) Kiteto amesema hatamvumilia Mzabuni wala Mtumishi yeyote ambaye ataenda kinyume na utaratibu wa utekelezaji wa miradi mbalimbali ya wananchi kuanzia upatikanaji wa vifaa vyenye vigezo vilivyowekwa, kununuliwa vifaa husika kwa wakati uliokubalika, kuwepo vifaa husika katika eneo la mradi, kufanya ukaguzi wa mara kwa mara kisha timu maalumu kujiridhisha kwanza kabla ya malipo kutolewa lakini pia kuhakikisha kwamba kama ni malipo ya vibarua basi yawafikie walengwa; utaratibu huu ndiyo uliosaidia Halmashauri kupata miradi mizuri na unaendelea kutumika katika utekelezaji wa miradi inayoendelea na miradi mipya itakayofuta ya mwaka 2017/2018.


Afisa Utumishi Wilaya Bw. Raphael Makoninde Akiwasilisha Taarifa Maalumu Kuhusu UHAKIKI wa Watumishi

 kwa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto na Maagizo Rasmi ya Kitaifa Juu ya Zoezi Hilo.


Uwasilishaji wa Taarifa za Uhakiki wa Watumishi wa Serikali

Watumishi 1476 Walihakikiwa Vyeti vya Kuhitimu Kidato cha IV na VI na Vyeti vya Taaluma kwa Walimu Kati Yao Watumishi 1383 Walikuwa na Vyeti Halali, Watumishi 66 Vyeti vya Kugushi, Watumishi 5 Vyeti Vyenye Utata na Watumishi 22 walikuwa na vyeti Visivyokamilika (incomplete).

Hata Hivyo Maagizo Kuhusu Uhakiki Huu kwa Watumishi wa Serikali ni Haya Yafuatayo :-

  1. kuwaondoa watumishi wote waliogushi vyeti kwenye orodha ya malipo ya mishahara na kuwaandikia barua ya kuwaachisha kazi 

  2. kuwaondoa watumishi wote wenye vyeti vya utata kwenye orodha ya malipo ya mishahara na kuwasilisha umiliki wa vyeti vyao Balaza la Mitihani Tanzania kabla ya tarehe 15.05.2017

  3. kuwajulisha watumishi wote wenye vyeti pungufu kuwasilisha vyeti vyao Balaza la Mitihati Tanzania kabla ya tarehe 15.05.2017 kwa ajili ya kuhakikiwa upya

  4. watumishi wanaokata rufaa kwa Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Menejimenti Utumishi wa Umma na Utawala Bora  wafanye hivyo kabla ya Tarehe 15.05.2017


Mkurugenzi Mtendaji (W) Bw. Tamim Kambona alipongezwa kwa kuwa mstari wa mbele katika kuifutatilia miradi yote kwa kujiridhisha katika ukaguzi yeye mwenyewe.


Pia Baraza la Madiwani liliipongeza  Kamati ya ulinzi na usalama inayoongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Kiteto Mh.Tumaini Magessa kwa kuimarisha usalama Wilayani kwetu Kiteto kwani  hadi sasa wakulima, wafugaji na wafanyabiashara mbalimbali na wananchi kwa ujumla wao wanaendelea na shuguli zao za kila siku bila shida.


Hitimisho.


Mh. Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto, Lairumbe Mollel akiahirisha Kikao cha Baraza la Madiwani tarehe 17.05.2017

Mh. Mwenyekiti wa Halmashauri Kiteto Lairumbe Mollel alisisitiza kwamba hakuna mgogoro wa wakulima na wafugaji Wilayani Kiteto kwani kuko shwari na watu wote waendelee kufanya shughuli zao kama kawaida. Pia aliongeza kuwa Watumishi na Madiwani ni muhimu kushirikiana na kufanya kazi kwa kufuata sheria, taratibu na kanuni zilizowekwa kwani hatutasita kumchukulia hatua yeyote atakayebainika kukwamisha shughuli za maendeleo katika Halmashauri anayoisimamia yeye.





Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA 11.06.2025 June 11, 2025
  • TANGAZO NAFASI YA KAZI- MWENYEKITI BODI YA MFUKO WA ELIMU June 08, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI JUNI 2025 June 07, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 06, 2025
  • Angalia zote

Habari mpya

  • JAMII YAASWA KUZINGATIA HAKI ZA WATOTO.

    June 16, 2025
  • MAFUNZO YA MFUMO WA E-UTENDAJI KWA WATUMISHI.

    June 12, 2025
  • KIKAO CHA MAANDALIZI YA MWENGE WA UHURU 2025

    June 11, 2025
  • WATOTO WA UMISSETA KITETO, WAWATOA JASHO WATU WAZIMA!

    June 10, 2025
  • Angalia zote

Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.

MWENGE MAKABIDHIANO MKOA WA MANYARA 2018
Video Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Hati ya Mshahara

Viunganishi vya Tovuti Nyingine

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • MANYARA
  • NECTA
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Kibaya-Kiteto

    Anwani ya Posta: P.o.Box 98, Kibaya-Kiteto

    Simu ya Mezani: +255 027-2552099

    Simu ya kiganjani:

    Barua Pepe: ded@kitetodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki@2017 Halimashauri ya Kiteto.Haki zote zimehifadhiwa