• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe watumishi |
    • Malalamiko |
Kiteto District Council
Kiteto District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Teknolojia,Habari ,Mawasiliano na Mahusiano
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Uchimbaji Madini
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Ardhi na Maliasili
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • This page is under construction
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi mipya
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

UGONJWA WA HOMA YA INI (HEPATITIS B) NI TISHIO LA MAISHA LAKINI TUMAINI LIPO KUPITIA CHANJO

Imetumwa : September 4th, 2025

Katika mwili wa binadamu, ini ni kiungo muhimu kinachohusika na kuchuja na kuondoa  sumu zinazotengenezwa mwilini, kumeng’enya virutubisho, kutengeneza nyongo na protini na pia ini linahusika kwenye kinga ya mwili. Miaka ya hivi karibuni, kiungo hiki kimekua hatarini kutokana na kuenea kwa maambukizi yanaojulikana kama Homa ya Ini (Hepatitis).

Homa ya ini (Hepatitis) ni ugonjwa wa maambukizi unaosababisha uvimbe kwenye ini kutokana na maambukizi ya virusi. Ugonjwa huu umegawanyika katika makundi A mpaka E ambapo kundi A na E husababisha madhara  ya muda mfupi kwenye ini wakati kundi B,C na D inasababisha madhara ya muda mfupi na muda mrefu.

Katika makundi yote hayo kundi B (Hepatitis B) imetajwa na wataalamu wa afya kuwa ni hatari zaidi na na hivyo makala hii inajikita zaidi kutoa elimu kuhusu kundi hilo kwani huathiri watu wengi zaidi.

Kwa mujibu wa daktari kutoka katika Hospitali ya Wilaya ya Kiteto Dkt. Honest Michael, kutokana na takwimu za watu wanaojitolea damu wilayani hapa, katika kila watu  100 wanaopimwa Hepatitis B, watu wanne hupatikana na maambukizi ya Hepatitis B. Takwimu hizi zinaashiria kwamba ugonjwa huu upo karibu nasi.

NJIA YA MAAMBUKIZI.

Virusi vya  Hepatiis B huenezwa kupitia damu au aina zote za maji maji yanatengenezwa mwilini ikiwemo mate, maji maji yanatoka ukeni pamoja na mbegu za kiume. Kutokana na hayo njia kuu  za mambukizi ya virusi vya Hepatitis B ni pamoja na kufanya ngono bila kinga, kuchangia sindano au vitu venye ncha kali, kuchangia miswaki, kuongezewa damu  isiyo salama pamoja na kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto wakati wa kujifungua au wakati wa kunyonyesha.

DALILI ZA MAAMBUKIZI YA HOMA YA INI

Dalili za maambukizi ya Homa ya Ini kwa kiasi kikubwa hufanana na dalili za homa za kawaida hivyo mtu apatapo dalili hizo anaweza kudhani amepata homa za kawaida. Dalili hizo ni pamoja na uchovu wa mwili, kutapika, kuharisha, maumivu ya tumbo, pamoja na mabadiliko ya ngozi au macho kuwa ya njano.

MATIBABU YA HEPATITIS B

Mwili wa binadamu una uwezo wa kutengeneza kinga na kupambana na maambukizi ya homa ya ini endapo ugonjwa huo upo kwenye hatua za awali. Hivyo watu wanaopatikana na maambukizi hayo wataalamu wa afya hushauri kuzingatia kanuni bora za maisha ikiwa ni pamoja na kula vyakula bora, kufanya mazoezi, kuepuka matumizi ya pombe pamoja na kujilinda kupata maambukizi mapya. Takwimu zinaonesha kwamba katika watu 100 wenye  Hepatitis B, asilimia 95 hupona kwa kutengeneza kinga mwilini huku asilimia 5 miili yao hushindwa kutengeneza kinga na kuwafanya wabaki na maambukizi ya muda mrefu yanayohitaji tiba ili kuzuia madhara

Kwa wagonjwa wanaoshindwa kupambana na maambukizi hayo ya Hepatitis B matibabu yao  hutegemea hatua mgonjwa aliyofikia, na wakati mwingine hulazimika kutumia dawa maalumu zinazozuia uzalishaji wa virusi  hivi ili kuipa kinga ya mwili nafasi ya kuviondoa.

MADHARA YA HEPATITIS B

Endapo mgonjwa atachelewa kuanza matibabu mapema  ugonjwa huu huweza kuleta madhara mbalimbali ikiwa ni pamoja na ini  kusinyaa (cirrhosis) na kupelekea kushindwa kufanya kazi, kusababisha kansa ya ini na pia huweza kupelekea kifo.

NJIA ZA KUJIKINGA.

Mtu anaweza kujilinda dhidi ya Hepatitis B kwa kuepuka kufanya ngono isiyo salama, kuepuka kuwa na wenza wengi, kujenga tabia ya kupima afya haswa kuangalia kama ana maambukizi ya Hepatitis B pamoja na kupata chanjo ya Hepatitis B.

UTOAJI WA CHANJO YA HEPATITIS B

Serikali imewezesha upatikanaji wa chanjo ya Hepatitis B katika vituo vya kutolea huduma za afya nchini kwa gharama nafuu.  Wilayani Kiteto chanjo hii hutolewa katika Hospitali ya wilaya. Chanjo hiyo hutolewa katika dozi tatu ambapo dozi ya kwanza hutolewa wakati wowote, dozi ya pili baada ya mwezi mmoja na dozi ya tatu baada ya miezi sita.

Kabla ya chanjo, ni lazma kupima ili kubaini  kama mtu ana maambukizi ya Hepatitis B na endapo atakutwa hana maambukizi ndipo huanzishiwa chanjo.

MUITIKIO WA WANANCHI KITETO DHIDI CHANJO YA HEPATITIS B NA WITO WA MTAALAMU WA AFYA

Kwa mujibu wa Dkt. Honest, muitikio wa wananchi wa Kiteto juu ya kupata chanjo ya Hepatitis B bado hauridhishi, hivyo ametoa wito kwa wananchi kujitokeza kwenda kupima ugonjwa huo na kupata chanjo.

“Ninatoa wito kwa wananchi kuja kupima ili wajue kama wana maambukizi ya Hepatitis B ama hawana. Gharama za kupima shilingi 10,000 na kila dozi inagharimu shilingi 10,000 hivyo jumla hapo ni 40,000. Gharama hii ni ndogo  ukilinganisha na matibabu ya Hepatitis B”, amesema Dkt. Honest.

Wataalamu wa afya wanasema kila mtu yupo kwenye hatari ya kupata maambukizi ya Hepatitis B. Hivyo wananchi wanashauriwa na kuhimizwa  kuchukua hatua mapema  kupima afya zao na kupata chanjo ili kujilinda maana KINGA NI BORA KULIKO TIBA.

Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAILI September 01, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU September 01, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI JUNI 2025 June 07, 2025
  • TANGAZO NAFASI YA KAZI- MWENYEKITI BODI YA MFUKO WA ELIMU June 08, 2025
  • Angalia zote

Habari mpya

  • UGONJWA WA HOMA YA INI (HEPATITIS B) NI TISHIO LA MAISHA LAKINI TUMAINI LIPO KUPITIA CHANJO

    September 04, 2025
  • DC MWEMA AFUNGUA RASMI ZAHANATI YA ENGUSERO SIDAN

    August 31, 2025
  • SAFARI YA KM 42 KUFUATA HUDUMA ZA AFYA SASA NI HISTORIA NDIRIGISHI

    August 30, 2025
  • WATAALUMU KUTOKA WRRB WATEMBELEA KITETO KUKAGUA MFUMO WA STAKABADHIZA GHALA

    August 28, 2025
  • Angalia zote

Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.

MWENGE MAKABIDHIANO MKOA WA MANYARA 2018
Video Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Hati ya Mshahara

Viunganishi vya Tovuti Nyingine

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • MANYARA
  • NECTA
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Kibaya-Kiteto

    Anwani ya Posta: P.o.Box 98, Kibaya-Kiteto

    Simu ya Mezani: +255 027-2552099

    Simu ya kiganjani:

    Barua Pepe: ded@kitetodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki@2017 Halimashauri ya Kiteto.Haki zote zimehifadhiwa