• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe watumishi |
    • Malalamiko |
Kiteto District Council
Kiteto District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Teknolojia,Habari ,Mawasiliano na Mahusiano
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Uchimbaji Madini
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Ardhi na Maliasili
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • This page is under construction
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi mipya
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Kiteto Yaadhimisha Siku ya Macho Duniani kwa Kutoa Huduma za Macho Bure

Imetumwa : October 11th, 2018

Mratibu wa Macho(W) Dkt. Enock Thomas Awary Akimfanyia uchunguzi wa macho mmoja wapo wa watu wenye matatizo ya macho wakati wa maadhimisho ya siku ya macho duniani.

Mganga mkuu (W) Dkt. Paschal Malkiadi Mbota akizungumza wakati wa maadhimisho hayo.

Mratibu wa Macho (W) Dkt. Enock Thomas Awary akizungumza wakati wa maadhimisho hayo.Mratibu wa Trakoma Mkoa  mkoa wa manyara  kutoka KCCO  bi Agnes Lukumay akizungumza wakati wa maadhimisho hayo.Wataalamu wa macho kutoka hospitali ya wilaya ya Kiteto pamoja na Mratibu wa Trakoma Mkoa wa Manyara  kutoka KCCO wakiendelea kutoa huduma wakati wa maadhimisho  hayo.

Baadhi ya vitendea kazi vinavyotumika katika huduma za uchunguzi na matibabu ya macho kama vinavyoonekana katika picha.

Wagonjwa wa macho wakisubiri kuitwa majina kwa ajili ya kupatiwa huduma katika maadhimisho ya siku ya macho duniani.


Mmoja wa wagonjwa wa macho( Aliye simama mbele ya meza) akiandikisha jina kwa ajili ya kupatiwa huduma,huku wengine (waliokaa kwenye viti ) wakiendelea kupatiwa huduma,na wengine wakisubiri kupatiwa huduma.

Mratibu wa Macho(W) Dkt. Enock Thomas Awary Akiwafanyia uchunguzi wa macho wagonjwa mbalimbali waliofika katika maadhimisho ya siku ya macho duniani.



......HABARI KAMILI......



Wilaya ya Kiteto imeadhimisha siku ya macho duniani kwa kutoa huduma za macho bure.Maadhimisho hayo yamefanyika  katika uwanja mkuu wa michezo uliopo katika mji mdogo wa Kibaya.


Katika kuazimisha siku hiyo wataalamu wa macho kutoka idara ya macho hospitali ya wilaya ya Kiteto kwa ufadhili wa shirika lisilo la kiserikali la 'Kilimanjaro Center for Community Opthmology ( KCCO) kupitia mradi wa 'Trachoma  Safe ’ wametoa huduma ya uchunguzi wa macho, ushauri, dawa sambamba na kuwapangia tarehe ya kurudi kwa ajili ya upasuaji  wagojwa ambao baada ya uchunguzi wameonekana kuhitaji upasuaji.


Akizungumza katika mahojiano mafupi yaliyofanyika uwanjani hapo,Mganga  Mkuu wa wilaya ya Kiteto daktari Malkiadi Paschal Mbota amesema kwamba katika wilaya ya Kiteto kuna matatizo mbalimbali ya macho kama Trakoma, mtoto wa jicho,presha ya macho na matatizo ya macho ambayo yanatokana na mionzi.Lakini ugonjwa ambao kitakwimu uko juu zaidi ni ugonjwa wa Trakoma, Trakoma bado ni tatizo kubwa, na kwamba  idara ya Afya wilaya kwa kushirikiana na KCCO  wamekuwa wakienda katika maeneo yote ya vijijini  kutoa huduma za uchunguzi, ushauri, dawa,upasuaji na elimu juu ya umuhimu wa kusafisha uso kwa maji safi pamoja na usafi wa mazingira kwa ujumla kwa lengo la kutokomeza ugonjwa huo.


Kadhalika Daktari Mbota ametoa wito kwa jamii,hususani jamii ya kifugaji kujenga tabia ya kunawa uso kwa maji safi mara kwa mara ili kuepuka ugonjwa wa Trakoma.Sambamba na wito huo, ameeleza kuhusu mkakati wa wilaya  katika kukabiliana na ugojwa wa Trakoma pamoja na magonjwa mengine ya macho, daktari Mbota amesema ''Kwa kushirikiana na KCCO tumekuwa tukifika kijiji hadi Kijiji  kuwatambua wagonjwa,na tukishawatambua ,madaktari wetu na manesi wamejengewa uwezo wa kutosha kuwapatia huduma zote zinazotakiwa ikiwemo upasuaji,wanaweka mahema hukohuko vijijini wanawafanyia upasuaji ''.


Naye mratibu  wa macho wilaya ya Kiteto Daktari Enock Thomas Awary  amesema kwamba wamejipanga kuhudumia watu wote watakaofika uwanjani hapo kwa lengo la kupata huduma za  macho,na kwamba wale ambao hawatakuwa wamehudumiwa kwa siku ya leo , huduma hiyo itaendelea hadi siku ya Jumamosi ,na watachukua namba za wagonjwa  watakaotakiwa kufanyiwa upasuaji kwa ajili ya kuwapangia tarehe za upasuaji na kuwafuatilia kuhakikisha wanafanyiwa upasuaji.


Daktari Awary ameendelea kusema kwamba huduma wanazotoa ni bure,hivyo watu wote wenye matatizo ya macho wasiache kufika  ili wapate huduma.Daktari Awary pia amesema kwamba huduma hiyo itafika hadi vijijini, na kwamba  wameshaweka utaratibu mzuri,wameandika barua kwa waganga wafawidhi wa  vituo vya afya na zahanati zote ,kuhakikisha kwamba watu wote wanaohitaji huduma hata katika maeneo ya pembezoni  wanafikiwa na huduma hiyo.


Katika hatua nyingine mratibu wa mradi wa Trakoma Mkoa wa Manyara kutoka KCCO  Bi Agnes Lukumay amesema kwamba lengo la KCCO kufadhili utoaji wa huduma hizo za uchunguzi na matibabu ya macho katika maadhimisho ya siku ya macho duniani ni kuzuia upofu unaoweza kuzuilika.Lukumay pia amesema kwamba takwimu zinaonyesha kwamba kwa mkoa wa Manyara ugonjwa wa Trakoma uko juu zaidi katika wilaya za Kiteto na Simanjiro.


Aidha bi Lukumay amesema kwamba ni vema wananchi wakajitokeza kwa wingi ili kupata huduma hizo za uchunguzi na matibabu ya macho, kwa sababu zinatolewa bure, na ni kwa ajili ya wananchi wote,hivyo  wasiache fursa hiyo  iwapite.


Shirika la 'Kilimanjaro Center for Community Opthmology' limeanza kazi zake mwaka 2015, kwa mkataba wa miaka 5.Dhima ya shirika hilo ni kutokomeza ugonjwa wa Trakoma ifikapo 2020.Hadi sasa shirika limeshahudumia kwa kuwafanyia upasuaji  wa macho wagonjwa wa Trakoma 600.


Katika maadhimisho hayo ,wagonjwa wa macho 379 wamefika uwanjani hapo kwa lengo la kupata huduma, ambapo wagonjwa 205 wamehudumiwa na wengine waliobaki wataendelea kuhudumiwa siku ya kesho Ijumaa  na kesho kutwa Jumamosi . Kauli mbiu ya siku ya macho duniani kwa mwaka 2018 ni ’Afya ya macho kwa wote,huduma ya macho kila mahali’




....MWISHO......

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA 11.06.2025 June 11, 2025
  • TANGAZO NAFASI YA KAZI- MWENYEKITI BODI YA MFUKO WA ELIMU June 08, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI JUNI 2025 June 07, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 06, 2025
  • Angalia zote

Habari mpya

  • MAFUNZO YA MFUMO WA E-UTENDAJI KWA WATUMISHI.

    June 12, 2025
  • KIKAO CHA MAANDALIZI YA MWENGE WA UHURU 2025

    June 11, 2025
  • WATOTO WA UMISSETA KITETO, WAWATOA JASHO WATU WAZIMA!

    June 10, 2025
  • WALIMU KITETO WAPEWA MAFUNZO YA AFUA JUMUISHI ZA ELIMU YA AFYA SHULENI

    June 05, 2025
  • Angalia zote

Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.

MWENGE MAKABIDHIANO MKOA WA MANYARA 2018
Video Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Hati ya Mshahara

Viunganishi vya Tovuti Nyingine

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • MANYARA
  • NECTA
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Kibaya-Kiteto

    Anwani ya Posta: P.o.Box 98, Kibaya-Kiteto

    Simu ya Mezani: +255 027-2552099

    Simu ya kiganjani:

    Barua Pepe: ded@kitetodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki@2017 Halimashauri ya Kiteto.Haki zote zimehifadhiwa