• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe watumishi |
    • Malalamiko |
Kiteto District Council
Kiteto District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Teknolojia,Habari ,Mawasiliano na Mahusiano
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Uchimbaji Madini
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Ardhi na Maliasili
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • This page is under construction
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi mipya
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

KITETO YAADHIMISHA SIKU YA AFYA NA LISHE KWA VIJIJI KUMI.

Imetumwa : September 14th, 2024

Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto kupitia Idara ya Afya Kitengo cha Lishe imefanikiwa kufanya maadhimisho ya Siku ya Afya na Lishe ya Kijiji (SALIKI) katika vijiji 10 kupitia ufadhili wa USAID Afya Yangu Mama na Mtoto.

Katika maadhimisho hayo ambayo yalianza Septemba 10, wataalam wa Lishe kutoka Ofisi ya Mkurugenzi (W) walitumia majukwaa ya SALIKI kuifundisha jamii kuhusu makundi sita ya chakula na kuhamasisha ulaji wa mlo kamili ili kujenga afya bora kwa Taifa bora.  


Aidha wataalamu hao walitumia majukwaa hayo kuifundisha jamii kwa vitendo namna bora ya kupika chakula kwa kuzingatia makundi mbalimbali ya chakula na kwa kutumia mahitaji yanayopatikana kwenye jamii husika kama vile maziwa, viazi na na mbogamboga kama vile maboga.

Aidha katika majukwaa hayo ya SALIKI kumefanyika zoezi la tathmini ya hali ya lishe kwa watoto na vijana balehe pamoja na kutoa dawa za minyoo na chanjo kwa watoto walio na umri wa chini ya miaka mitano.

Mkuu wa Kitengo na Lishe (W) Ndg. Beatrice Lutanjuka amesema kwamba maadhimisho haya yanapaswa kufanyika kwenye kila  robo ya mwaka na katika kila kijiji, lengo likiwa ni kusogeza huduma za afya na lishe  karibu na jamii ikiwemo kutoa elimu ya lishe na chanjo ili kuweza kupambana na utapia mlo  kwa watu wa rika mbalimbali pamoja na  kupambana na udumavu.

Aidha Ndg. Lutanjuka amewashukuru wadau ambao ni USAID Afya Yangu Mama na Mtoto kwa ufadhili wao ambao umewezesha kufanyika kwa maadhimisho hayo kwa vijiji kumi ambayo kilele kilifanyika Septemba 13,2024 katika Kijiji cha Mbeli ambapo Mgeni Rasmi alikua Katibu Tawala wa Wilaya Ndg. Mufandii Msaghaa.

Aidha, Ndg. Lutanjuka amewaomba wadau hao kuendelea kushirikiana na Halmashauri katika masuala ya Afya na Lishe ili kuisaidia Halmashauri kuendelea kutekeleza Mpango wa Pili Jumuishi wa Taifa wa Masuala ya Lishe (NMNAP II).

Tanzania Bara inatekeleza  NMNAP II  mpango ambao una lengo la kutoa mwongozo wa utekelezaji wa afua za lishe Tanzania Bara kwa kipindi cha Miaka mitano 2021/22 – 2025/26 ili kuweza kuimarisha mikakati ya kukabiliana na aina zote za utapia mlo kwa watu wa rika zote.

Matatizo ya utapia mlo yana athari kubwa kwa mtu mmoja-mmoja, kaya, jamii na Taifa kwa ujumla wake na hivyo kuchangia kupungua kwa kasi katika kufikia malengo ya maendeleo; kiafya, kiuchumi na kijamii.

Matangazo

  • TANGAZO NAFASI ZA KAZI July 23, 2021
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI NAFASI YA UTENDAJI WA KIJlJI III August 26, 2021
  • TANGAZO LA KUKODISHA VIBANDA March 01, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI SEPTEMBA 2023 September 03, 2023
  • Angalia zote

Habari mpya

  • TABIA MBAYA ZA WATUMUSHI ZINAHARIBU SIFA ZA TAASISI

    May 01, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI KITETO LIMEMPONGEZA RAIS SAMIA.

    May 30, 2025
  • PONGEZI KWA WANANCHI KWA KUTUNZA MAZINGIRA

    April 28, 2025
  • TUUENZI MUUNGANO WETU

    April 27, 2025
  • Angalia zote

Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.

MWENGE MAKABIDHIANO MKOA WA MANYARA 2018
Video Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Hati ya Mshahara

Viunganishi vya Tovuti Nyingine

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • MANYARA
  • NECTA
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Kibaya-Kiteto

    Anwani ya Posta: P.o.Box 98, Kibaya-Kiteto

    Simu ya Mezani: +255 027-2552099

    Simu ya kiganjani:

    Barua Pepe: ded@kitetodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki@2017 Halimashauri ya Kiteto.Haki zote zimehifadhiwa