• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe watumishi |
    • Malalamiko |
Kiteto District Council
Kiteto District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Teknolojia,Habari ,Mawasiliano na Mahusiano
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Uchimbaji Madini
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Ardhi na Maliasili
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • This page is under construction
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi mipya
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

KITETO YAENDELEA KUTEKELEZA MAAGIZO YA SERIKALI KWA VITENDO: GHALA LA KISASA LA MAZAO LAJENGWA KWA MAPATO YA NDANI

Imetumwa : July 23rd, 2025

Katika jitihada za kuinua uchumi wa wananchi na kuhakikisha usalama wa chakula, Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto imeamua kujenga ghala la kisasa la kuhifadhi mazao lililogharimu kiasi cha shilingi milioni 149,680,000 ikiwa chanzo cha fedha ni mapato ya ndani ya halmashauri.


Lengo kuu la mradi huu ni kutoa huduma za kiutawala kupitia mfumo wa stakabadhi za ghala kwa kuwasaidia wakulima kuongeza thamani ya mazao yao na kuhakikisha mazao yanahifadhiwa kwa usalama kabla ya kuingia sokoni. Ghala hili litakuwa na uwezo wa kuhifadhi kati ya tani 437.5 hadi 600.


Kukamilika kwa ghala la kisasa kutakua na manufaa makubwa kwa wakulima na jamii kwa ujumla. Kwanza, litaongeza ubora na thamani ya mazao, jambo litakalowawezesha wakulima kupata bei bora na yenye tija. Pili, litakuwa kituo rasmi cha ukusanyaji wa mazao kwa taasisi kama NFRA pamoja na sekta binafsi.


Faida nyingine ni kuimarika kwa usalama wa chakula, kupunguza gharama za usafirishaji na kuongezeka kwa ajira hasa kwa kina mama na vijana. Vilevile, mradi unatarajiwa kuchangia kuongezeka kwa  mapato ya halmashauri, hivyo kuongeza uwezo wake wa kutoa huduma bora zaidi kwa wananchi.


Kwa ujumla, ujenzi wa ghala la kisasa ambalo limejengwa katika kata ya Kibaya, ni hatua muhimu kuelekea maendeleo endelevu ya kilimo na ustawi wa jamii.


Jiwe la msingi la ujenzi wa ghala la kisasa liliwekwa Julai 13, 2025 na kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru 2025 Ndugu.Ismail Ali Ussi.


Akizungumza kabla ya kuweka jiwe la msingi, kiongozi huyo alimpongeza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri pamoja na watendaji wengine kwa kuendelea kutii maagizo ya kutekeleza miradi ya maendeleo kupitia mapato ya ndani.


"Mkurugenzi nakushukuru wewe pia ni miongoni mwa wakurugenzi pamoja na  watendaji wenzako wote ambao mmeendelea kutii maelekezo na maagizo ya Dkt. Samia  aliwaelekeza  wakurugenzi wote nchini kuhakikisha mnatenga fedha za mapato ya ndani kujenga miradi mbalimbali ya kimaendeleo ambayo inawasaidia wananchi leo hii tumekuja kujionea ghala hili kwakweli ghala  hili la kisasa ni ghala lenye ubora ambalo litaenda kuwasaidia wananchi wengi ambao watakuja kuhifadhi bidhaa zao hapa". Alisema Ndugu. Ussi.


Utekelezaji wa mradi wa ghala la kisasa umefikia asilimia 70.

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA 11.06.2025 June 11, 2025
  • TANGAZO NAFASI YA KAZI- MWENYEKITI BODI YA MFUKO WA ELIMU June 08, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI JUNI 2025 June 07, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 06, 2025
  • Angalia zote

Habari mpya

  • HAYAWI HAYAWI SASA YAMEKUA: HATIMAYE KALOLENI YAPATA SHULE MPYA YA MSINGI

    July 30, 2025
  • SHULE YA MSINGI KINANGALI NAYO YANUFAIKA NA MRADI WA BOOST

    July 30, 2025
  • SERIKALI YA AWAMU YA SITA YAENDELEA KUWEKEZA KWA VITENDO: KURASH YAPATA MRADI MWINGINE WA MILIONI 153 KUPITIA BOOST

    July 30, 2025
  • KATA YA BWAWANI YAPATA MRADI WA SHULE MPYA YA ELIMU MSINGI.

    July 28, 2025
  • Angalia zote

Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.

MWENGE MAKABIDHIANO MKOA WA MANYARA 2018
Video Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Hati ya Mshahara

Viunganishi vya Tovuti Nyingine

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • MANYARA
  • NECTA
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Kibaya-Kiteto

    Anwani ya Posta: P.o.Box 98, Kibaya-Kiteto

    Simu ya Mezani: +255 027-2552099

    Simu ya kiganjani:

    Barua Pepe: ded@kitetodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki@2017 Halimashauri ya Kiteto.Haki zote zimehifadhiwa