• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe watumishi |
    • Malalamiko |
Kiteto District Council
Kiteto District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Teknolojia,Habari ,Mawasiliano na Mahusiano
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Uchimbaji Madini
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Ardhi na Maliasili
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • This page is under construction
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi mipya
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

KITETO YANG’ARA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2023, YAPATA HATI SAFI

Imetumwa : October 8th, 2023

Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto imepata hati safi katika mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2023.

Kauli hiyo imetolewa na Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Taifa, Bw. Abdalla Shaib Kaim, Oktoba 8, 2023 Wilayani Simanjiro wakati Kiteto ikikabidhi Mwenge wa Uhuru kwa Wilaya ya Simanjiro.

Bw. Kaim alisema, Mwenge wa Uhuru katika Mkoa wa Manyara ulipokelewa katika Wilaya ya Kiteto na wilaya hiyo imefanya vizuri na kupata hati safi.  ‘Huo ni mwanzo mzuri kwa Mkoa wa Manyara ninaamini Simanjiro na wilaya nyingine za mkoa huu nazo zitafanya vizuri”, aliongeza Bw. Kaim.

Bwana Kaim pia alimpongeza  Mkuu wa Wilaya ya Kiteto,  SSI. Mbaraka Alhaj Batenga, Mkurugenzi Mtendaji (W), CPA. Hawa Abdul Hassan , wataalamu wote na wananchi kwa utekelezaji na  usimamizi mzuri wa miradi hiyo mizuri.

Sambamba na hilo, nae Mkimbiza Mwenge wa Taifa, Bi. Atupokile Elia Mhalila, aliipongeza Kiteto kwa kua na mradi bora wa afya. “Toka tulipoanza kukimbiza Mwenge wa Uhuru 2023, hatujakutana na mradi mkubwa wa afya  na uliotekelezwa kwa ubora wa kiwango kile kupitia force akaunti”, aliongeza Bi Mhalila.

Oktoba 7,2023 Mkuu wa Mkoa wa Manyara Mh. Queen Cuthbert Sendiga aliupokea Mwenge wa Uhuru kimkoa katika viwanja vya shule ya msingi Dosidosi Wilayani Kiteto  na kisha kuukabidhi kwa Mkuu wa Wilaya Mh Batenga. Ukiwa wilayani Kiteto, Mwenge wa Uhuru umekimbizwa umbali wa takribani  kilometa  208 na umepitia  miradi 9 ambapo miradi 3 ilifunguliwa, miradi 2 ilizunduliwa, mradi 1 uliwekewa jiwe la msingi na miradi  3 kukaguliwa;  yote ikiwa na jumla ya thamani ya bilioni 2.4. Miradi hiyo ni pamoja na miradi ya sekta ya elimu, afya, maji na utunzaji wa mazingira.

Matangazo

  • TANGAZO NAFASI ZA KAZI July 23, 2021
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI NAFASI YA UTENDAJI WA KIJlJI III August 26, 2021
  • TANGAZO LA KUKODISHA VIBANDA March 01, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI SEPTEMBA 2023 September 03, 2023
  • Angalia zote

Habari mpya

  • TABIA MBAYA ZA WATUMUSHI ZINAHARIBU SIFA ZA TAASISI

    May 01, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI KITETO LIMEMPONGEZA RAIS SAMIA.

    May 30, 2025
  • PONGEZI KWA WANANCHI KWA KUTUNZA MAZINGIRA

    April 28, 2025
  • TUUENZI MUUNGANO WETU

    April 27, 2025
  • Angalia zote

Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.

MWENGE MAKABIDHIANO MKOA WA MANYARA 2018
Video Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Hati ya Mshahara

Viunganishi vya Tovuti Nyingine

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • MANYARA
  • NECTA
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Kibaya-Kiteto

    Anwani ya Posta: P.o.Box 98, Kibaya-Kiteto

    Simu ya Mezani: +255 027-2552099

    Simu ya kiganjani:

    Barua Pepe: ded@kitetodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki@2017 Halimashauri ya Kiteto.Haki zote zimehifadhiwa