Mkuu wa Mkoa wa Manyara Mhe. Queen Sendiga ameipongeza Halmashauri ya Wilaya Kiteto kwa kuendelea kupata Hati Safi ya Ukaguzi.
Akizungumza katika Baraza Maalumu la kujibu hoja za Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali ambalo limefanyika Juni 2, 2025 wilayani hapa, Mhe. Sendiga ameeleza kuwa matokeo ya kupata Hati Safi ni dhahiri kua baraza la madiwani pamoja na Ofisi ya Mkurugenzi wamejitahidi katika kusimamia na kufuata sheria na kanuni zilizoweka na hivyo kuiepusha Halmashauri kupata Hati ya Mashaka ama Hati Chafu.
Aidha Mkuu wa Mkoa huyo ametoa pia pongezi kwa Halmashauri kwa kuweza kutekeleza maagizo 10 kati ya 12 yaliyotolewa na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC).
"Naomba pia niwapongeze kwa utekelezaji wa maagizo hayo 10, yaliyobakia hayo mawili naamini mnaweza kuyamaliza harakaharaka, muongeze bidii na nguvu kidogo hapo ili kusudi tuweze kuyamaliza", ameongeza Mhe. Sendiga.
Sambamba na pongezi hizo, Mhe. Sendiga amesema kwamba ni marufuku kwa Idara na Vitengo kusababisha hoja na mtumishi yeyote atakayesababisha hoja ashughulikiwe kwa mujibu wa sheria, taratibu na kanuni.
Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto ilikuwa na Hoja thelathini na mbili (32) zilizofutwa ni hoja kumi na mbili (12) na hoja ishirini (20) ziko kwenye hatua mbalimbali za umalizaji. Mhe. Sendiga ameagiza ifikapo Desemba 31,2025 hoja zote zilizobaki ziwe zimefungwa.
Kibaya-Kiteto
Anwani ya Posta: P.o.Box 98, Kibaya-Kiteto
Simu ya Mezani: +255 027-2552099
Simu ya kiganjani:
Barua Pepe: ded@kitetodc.go.tz
Hakimiliki@2017 Halimashauri ya Kiteto.Haki zote zimehifadhiwa