• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe watumishi |
    • Malalamiko |
Kiteto District Council
Kiteto District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Teknolojia,Habari ,Mawasiliano na Mahusiano
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Uchimbaji Madini
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Ardhi na Maliasili
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • This page is under construction
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi mipya
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

KITETO YAWATUMIA WANAFUNZI KUWA MABALOZI WA LISHE KUPITIA UFUGAJI WA SUNGURA

Imetumwa : July 24th, 2025

Katika kupambana na changamoto za Lishe, Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto imekua ikitekeleza shughuli mbalimbali na hivi karibuni imeanzisha  shughuli ya ufugaji wa sungura  kupitia wanafunzi wa klabu za lishe kutoka shule za msingi na  sekondari.


Mbali na hilo Halmashauri pia inatekeleza mradi wa ufugaji wa samaki  kwenye jamii kwa lengo kuu la kuboresha afya za wananchi ikiwepo kupambana na matatizo  yatokanayo na lishe duni.


Hadi sasa mradi wa ufugaji wa sungura unatekelezwa kupitia klabu za lishe shuleni katika shule 10 na lengo la mradi ni kuzalisha sungura na kusambaza katika shule zote 128 (msingi na sekondari).


Utekelezaji wa mradi kupitia wanafunzi unalenga kuwapa wanafunzi ujuzi na usambazaji elimu ya lishe yenye kuelezea faida za nyama ya sungura na samaki kiafya ikiwa ni nyama nyeupe isiyo na mafuta mabaya hivyo kukabiliana na magonjwa yasiyo ambukizwa kama vile shinikizo la damu.


Aidha lengo la mradi wa samaki ni kuzalisha vifaranga aina ya sato na kupandikiza kwenye mabwawa sita ya asili ambayo ni Pori namba moja, Namelock, Orkitikit Asamatwa, Partimbo na Katikati ili kuongeza upatikanaji wa samaki kwa jamii.


Julai 13, 2025 katika mbio za Mwenge za Mwaka 2025 wilayani hapa , kiongozi wa Mbio za Mwenge Kitaifa, Ndg Ismail Ali Ussi, alitembelea banda la shughuli za mapambano dhidi ya changamoto za lishe.


Akiwa katika banda hilo Ndg. Ussi alisema kwamba wamefarijika kuona wanafunzi wadogo wakiendelea kujifunza mambo ya lishe.


" Ni imani yangu wanafunzi hawa watakua waadilifu na wataenda kuwafundisha wazazi na wenzao na wataenzi klabu hizo za lishe", alisema Kiongozi huyo.


Aidha Kiongozi huyo alisema kwamba  kilimo sio lazma mtu aende shambani na anaamini kwa ufugaji wa samaki na sungura wanafunzi watakua mabalozi wazuri kwa Kiteto.

Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAILI September 01, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU September 01, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI JUNI 2025 June 07, 2025
  • TANGAZO NAFASI YA KAZI- MWENYEKITI BODI YA MFUKO WA ELIMU June 08, 2025
  • Angalia zote

Habari mpya

  • DAS KITETO AWAHIMIZA WANANCHI KUJENGA UTAMADUNI WA UWEKEZAJI.

    September 11, 2025
  • UGONJWA WA HOMA YA INI (HEPATITIS B) NI TISHIO LA MAISHA LAKINI TUMAINI LIPO KUPITIA CHANJO

    September 04, 2025
  • DC MWEMA AFUNGUA RASMI ZAHANATI YA ENGUSERO SIDAN

    August 31, 2025
  • SAFARI YA KM 42 KUFUATA HUDUMA ZA AFYA SASA NI HISTORIA NDIRIGISHI

    August 30, 2025
  • Angalia zote

Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.

MWENGE MAKABIDHIANO MKOA WA MANYARA 2018
Video Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Hati ya Mshahara

Viunganishi vya Tovuti Nyingine

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • MANYARA
  • NECTA
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Kibaya-Kiteto

    Anwani ya Posta: P.o.Box 98, Kibaya-Kiteto

    Simu ya Mezani: +255 027-2552099

    Simu ya kiganjani:

    Barua Pepe: ded@kitetodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki@2017 Halimashauri ya Kiteto.Haki zote zimehifadhiwa