• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe watumishi |
    • Malalamiko |
Kiteto District Council
Kiteto District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Teknolojia,Habari ,Mawasiliano na Mahusiano
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Uchimbaji Madini
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Ardhi na Maliasili
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • This page is under construction
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi mipya
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

KITUO CHA AFYA ENGUSERO CHAANZA KUFANYA UPASUAJI.

Imetumwa : October 12th, 2023

Katika mipango na mikakati  ya serikali  ya kuboresha na kusogeza huduma za afya karibu na wananchi, kituo cha afya cha Engusero kilichopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto kimeanza kufanya upasuaji kwa mama wajazito.

Akizungumza kuhusu huduma hiyo Oktoba 12, 2023, Mganga Mkuu (W), Dr. Vicent Gyunda  amesema kwamba upasuaji wa kwanza umefanyika Oktoba 3, 2023 ikiwa ni baada ya kituo hicho kupokea vifaa vyenye thamani ya zaidi ya shilingi 105,000,000 kutoka serikali kuu.

“Ni shukrani za kipee kwa Mh. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  kwa kuwasogezea karibu huduma za afya wananchi wa Kiteto” alisema Dr. Gyunda.

Nae Mkurugenzi Mtendaji (W), CPA. Hawa Abdul Hassan, amesema kwamba katika mwaka wa fedha 2022/2023 halmashauri yake ilipokea kiasi cha takribani bilioni 1.5 katika sekta ya afya ambapo kati ya fedha hizo kiasi cha shilingi 900,000,000 zilitumika kujenga majengo matatu katika hospitali ya wilaya, ambayo ni jengo la mama na mtoto, jengo la maabara na jengo la upasuaji.

Vilevile  halmashauri ilipokea kiasi cha shilingi 100,000,000 kwaajili ya ukamilishaji wa maboma ya zahanati.  Sambamba na hilo,   halmashauri ilipokea pia kiasi cha shilingi 100,000,000 kwaajili ya ununuzi wa vifaa vya zahanati ya Njiapanda, Magungu, Nchinila na Ngipa.

Upande wa ununuzi wa vifaa tiba katika vituo vya afya Engusero, Mwanya na Kijungu;, halmashauri ilipokea kiasi cha shilingi 450,000,000 na vifaa tiba vyote upande wa zahanati na vituo vya afya vimekwisha nunuliwa.

“Katika mwaka huu wa fedha 2023/2024, mpaka sasa halmashauri imekwisha pokea kiasi cha shilingi 936,000,000 ambapo kati ya hizo sekta ya afya imepokea kiasi cha shilingi  100,000,000 kwaajili ya ukamilishaji wa maboma ya zahanati mbili ambazo ni zahanati ya Mbeli iliyopo kijiji cha Kimana kata ya Partimbo na zahanati ya Olgira iliyopo kijiji cha Olgira kata ya Sunya”,  alisema Mkurugenzi Mtendaji,  CPA. Hawa Abdul Hassan.

Matangazo

  • TANGAZO NAFASI ZA KAZI July 23, 2021
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI NAFASI YA UTENDAJI WA KIJlJI III August 26, 2021
  • TANGAZO LA KUKODISHA VIBANDA March 01, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI SEPTEMBA 2023 September 03, 2023
  • Angalia zote

Habari mpya

  • TABIA MBAYA ZA WATUMUSHI ZINAHARIBU SIFA ZA TAASISI

    May 01, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI KITETO LIMEMPONGEZA RAIS SAMIA.

    May 30, 2025
  • PONGEZI KWA WANANCHI KWA KUTUNZA MAZINGIRA

    April 28, 2025
  • TUUENZI MUUNGANO WETU

    April 27, 2025
  • Angalia zote

Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.

MWENGE MAKABIDHIANO MKOA WA MANYARA 2018
Video Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Hati ya Mshahara

Viunganishi vya Tovuti Nyingine

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • MANYARA
  • NECTA
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Kibaya-Kiteto

    Anwani ya Posta: P.o.Box 98, Kibaya-Kiteto

    Simu ya Mezani: +255 027-2552099

    Simu ya kiganjani:

    Barua Pepe: ded@kitetodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki@2017 Halimashauri ya Kiteto.Haki zote zimehifadhiwa