• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe watumishi |
    • Malalamiko |
Kiteto District Council
Kiteto District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Teknolojia,Habari ,Mawasiliano na Mahusiano
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Uchimbaji Madini
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Ardhi na Maliasili
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • This page is under construction
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi mipya
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

KUELEKEA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA, VIONGOZI WA DINI WAPEWA JUKUMU LA KUSAIDIA MAPAMBANO DHIDI YA RUSHWA KUPITIA ELIMU

Imetumwa : September 29th, 2024

Viongozi wa dini  Wilayani Kiteto wameombwa kwenda kuwapa elimu waumini wao juu ya madhara ya rushwa katika uchaguzi wa serikali za Mitaa unaotarajiwa kufanyika Novemba, 2024.


Rai hiyo imetolewa Septemba 28, 2024 na Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Manyara, Ndg. Bahati Stafu Haule, katika semina maalumu na Masheikhe, Maimamu na Makatibu kata wa misikiti Wilayani  Kiteto.


Akiongea wakati wa ufunguzi wa semina hiyo, Mkuu wa TAKUKURU Wilaya ya Kiteto, Ndg, Venance Sangawe, amesema kwamba lengo la semina hiyo ni kupanua wigo na ushirikiano na wadau  haswa katika kipindi hiki cha uchaguzi ili kuwezesha jamii kuwa macho juu ya vitendo vya rushwa katika mchakato wote wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa.


Akitoa semina hiyo, Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Manyara Ndugu Bahati Stafu Haule amesema kwamba viongozi wa dini hao wana nafasi kubwa ya kukemea rushwa maana  rushwa ni suala mbali ya kuwa ni Jinai la pia kiimani kwani vitabu vyote viwili vya dini, Quran Tukufu na Biblia Takatifu, vinakataza vitendo vya rushwa na kwamba ni dhambi.


Mkuu huyo ameeleza kwamba katika uchaguzi, rushwa inaweza kutokea katika mazingira matatu ambayo ni kwa mgombea, kwa mpiga kura na kwa msimamizi wa uchaguzi hivyo wananchi wanatakiwa  kuhakikisha kuwa vitendo vya rushwa havitokei hasa kabla, wakati na baada ya Uchaguzi.

“Kiongozi anayekupa rushwa ili umchague ina maana hafai kuwa kiongozi ndio maana anatumia nguvu ya ziada achaguliwe. Kiongozi anayepatikana kwa njia ya rushwa akiwa madarakani hawezi kuleta maendeleo kwani atakua anafanya kazi kwa maslahi yake binafsi ili aweze kurudisha gharama alizozitumia kwenye uchaguzi”, ameongeza Ndg. Haule.


Mkuu huyo aliendelea kufafanua kuwa TAKUKURU ina majukumu makuu mawili ambayo ni Kuzuia  na Kupambana Rushwa ambapo majukumu ambapo jukumu la Kuzuia linatekelezwa kupitia utoaji elimu, tafiti, chambuzi za mifumo na ufuatiliaji wa miradi ya maendeleo aidha katika kupambana alielezea kuwa jukumu hilo linatekelezwakupitia hayo wanayatekeleza kupitia  Uchunguzi na Mashtaka.


Mkuu huyo ameongeza kwa kusema kwamba TAKUKURU peke yao hawawezi kutomeza rushwa bali ushirikiano kati yao na taasisi mbalimbali wakiwemo viongozi wa dini na hiyo ndio sababu ya semina hiyo ili kupeana elimu kwa lengo la viongozi hao kwenda kuelimisha waumini wao.


Naye Katibu Tawala wa Wilaya ya Kiteto, Bi. Mufandii Msaghaa , amewashukuru viongozi wa TAKUKURU Wilaya na Mkoa kwa kuona umuhimu wa kutoa elimu hiyo kwa viongozi hao wa dini na kusema kwamba elimu hiyo imekuja wakati muafaka kwani taifa linajiandaa na Uchaguzi wa Serikali za Mitaa ambao utafanyika Novemba 27,2024.


Naye Sheikhe wa Wilaya ya Kiteto, Sheikhe Omari Bakari Fumito, ameishukuru taasisi hiyo ngazi ya Wilaya na Mkoa, kwa elimu waliyowapatiwa na kuwahimiza masheikhe hao na maimamu kuwa elimu hiyo iwanufaishe na kuwafikia waumini wanaowaongoza.

Matangazo

  • TANGAZO NAFASI ZA KAZI July 23, 2021
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI NAFASI YA UTENDAJI WA KIJlJI III August 26, 2021
  • TANGAZO LA KUKODISHA VIBANDA March 01, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI SEPTEMBA 2023 September 03, 2023
  • Angalia zote

Habari mpya

  • TABIA MBAYA ZA WATUMUSHI ZINAHARIBU SIFA ZA TAASISI

    May 01, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI KITETO LIMEMPONGEZA RAIS SAMIA.

    May 30, 2025
  • PONGEZI KWA WANANCHI KWA KUTUNZA MAZINGIRA

    April 28, 2025
  • TUUENZI MUUNGANO WETU

    April 27, 2025
  • Angalia zote

Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.

MWENGE MAKABIDHIANO MKOA WA MANYARA 2018
Video Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Hati ya Mshahara

Viunganishi vya Tovuti Nyingine

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • MANYARA
  • NECTA
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Kibaya-Kiteto

    Anwani ya Posta: P.o.Box 98, Kibaya-Kiteto

    Simu ya Mezani: +255 027-2552099

    Simu ya kiganjani:

    Barua Pepe: ded@kitetodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki@2017 Halimashauri ya Kiteto.Haki zote zimehifadhiwa