• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe watumishi |
    • Malalamiko |
Kiteto District Council
Kiteto District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Teknolojia,Habari ,Mawasiliano na Mahusiano
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Uchimbaji Madini
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Ardhi na Maliasili
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • This page is under construction
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi mipya
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

WAZEE WAHIMIZWA KUJITOKEZA KWA WINGI KUPIGA KURA OKTOBA 29

Imetumwa : October 7th, 2025

Mkuu wa Wilaya ya Kiteto, Mhe. Remidius Mwema Emmanuel, amewahimiza wazee kujitokeza kwa wingi kushiriki katika Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 29, 2025.


Akizungumza  leo Oktoba 7, 2025, katika Maadhimisho ya Siku ya Wazee yaliyofanyika katika Kata ya Kibaya kwa ngazi ya Wilaya,Mhe. Mwema amesema wazee wana nafasi kubwa ya kuleta mabadiliko chanya kupitia sanduku la kura, hivyo wasikose kushiriki kwa mujibu wa kauli mbiu ya mwaka huu isemayo: “Wazee Tushiriki Uchaguzi Mkuu kwa Ustawi wa Jamii Yetu.”


Aidha, aliwasihi wazee kutumia nafasi yao ya heshima na uzoefu kuwashauri vijana kushiriki kikamilifu katika uchaguzi na shughuli za kijamii, alieleza  kuwa ni njia bora ya kuwajenga kimaadili na kuwaepusha na makundi hatarishi.

“Ofisi yangu iko wazi, msisite kufika kunishauri au kunieleza changamoto mnazokutana nazo. Niko tayari kushirikiana nanyi kwa maendeleo ya Kiteto na Taifa kwa ujumla,” aliongeza Mhe. Mwema.


Naye, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto, CPA. Hawa Abdul Hassan, alitumia maadhimisho hayo kupongeza mchango wa wazee katika ustawi wa jamii, akibainisha kuwa Serikali inaendelea kuwajali na kutekeleza sera rafiki kwao.

 “Tunamshukuru Mungu kwa kutupa wazee hawa, kwani wazee ni dawa na faraja kwa vijana,tumehuisha baraza la wazee na tayari tumeanza na vikao. Mapendekezo yote yaliyowasilishwa leo, yale yasiyo hitaji fedha tutayafanyia kazi mara moja, na yanayohitaji fedha tutaanza kuyashughulikia kuanzia sasa,” alisema CPA. Hawa.


Kwa upande wake, Afisa Ustawi wa Jamii wa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto, Bi. Jackline Barongo, aliisihi jamii kuendeleza utamaduni wa kuenzi wazee kama nguzo muhimu ya jamii, akisisitiza umuhimu wa kutambua mchango wao katika kujenga taifa lenye maadili.

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA MAPOKEZI YA FEDHA SEPTEMBA 2025 September 16, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU September 01, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI September 01, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI JUNI 2025 June 07, 2025
  • Angalia zote

Habari mpya

  • WAZEE WAHIMIZWA KUJITOKEZA KWA WINGI KUPIGA KURA OKTOBA 29

    October 07, 2025
  • KATIBU MKUU WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI AKABIDHI VIFAA NA CHANJO YA KICHAA CHA MBWA KITETO

    September 29, 2025
  • WITO WA LEO SEPTEMBA 29,2025

    September 29, 2025
  • TANZANIA YA TATU AFRIKA MPANGO RASMI WA KUDHIBITI KICHAA CHA MBWA

    September 29, 2025
  • Angalia zote

Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.

MWENGE MAKABIDHIANO MKOA WA MANYARA 2018
Video Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Hati ya Mshahara

Viunganishi vya Tovuti Nyingine

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • MANYARA
  • NECTA
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Kibaya-Kiteto

    Anwani ya Posta: P.o.Box 98, Kibaya-Kiteto

    Simu ya Mezani: +255 027-2552099

    Simu ya kiganjani:

    Barua Pepe: ded@kitetodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki@2017 Halimashauri ya Kiteto.Haki zote zimehifadhiwa