• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe watumishi |
    • Malalamiko |
Kiteto District Council
Kiteto District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Teknolojia,Habari ,Mawasiliano na Mahusiano
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Uchimbaji Madini
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Ardhi na Maliasili
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • This page is under construction
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi mipya
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

"Wanawake Tumieni Fursa Zilizopo Kujikwamua Kiuchumi''DC Magessa

Imetumwa : March 14th, 2018

Mgeni Rasmi  katika maazimisho ya siku ya wanawake duniani  yaliyofanyika katika  kijiji cha Mbigiri - kata ya Partimbo  wilayani Kiteto ambaye pia ni Mkuu wa wilaya ya Kiteto Mhe.Tumaini Magessa (aliyesimama) akihutubia wananchi wakati wa maadhimisho hayo. 

Mwenyekiti wa Kijiji cha Mbigiri akiwasalimia wananchi  wakati  wa maadhimisho ya siku ya wanawake duniani  yaliyofanyika katika kijiji cha Mbigiri - kata ya Partimbo wilayani Kiteto.

Katibu wa UWT (W)  Kiteto Bi. Fatuma akiwasalimia wananchi wakati wa maadhimisho ya siku ya wanawake duniani yaliyofanyika katika kijiji cha Mbigiri - kata ya Partimbo, wilayani Kiteto.

Kaimu Katibu Tawala (W) - Kiteto Ndg. Fadhili Didani akimkaribisha mgeni rasmi Mhe. Tumaini Magessa   wakati maadhimisho ya siku ya wanawake duniani  yaliyofanyika katiika kijiji cha mbigiri - kata ya Partimbo wilayani Kiteto.Kulia ni afisa maendeleo ya jamii (W)  Ndg. Joseph Mwaleba

Afisa Ustawi wa Jamii (W) Bi. Jacline Barongo Kiteto akisoma risala  wakati maadhimisho ya siku ya wanawake duniani  yaliyofanyika katiika kijiji cha mbigiri - kata ya Partimbo wilayani Kiteto.

Mratibu wa ICHF (W)  Kiteto Bi.Rufina Haule  akihamasisha wananchi kujiunga na ICHF  iliyoboreshwa wakati maadhimisho ya siku ya wanawake duniani  yaliyofanyika katiika kijiji cha mbigiri - kata ya Partimbo wilayani Kiteto.


Meneja wa Benki ya CRDB - Tawi la Kiteto Bi. Lucia John akiwasilisha mada kuhusu mikopo  wakati wa maadhimisho ya siku ya wanawake duniani  yaliyofanyika katiika kijiji cha Mbigiri - kata ya Partimbo wilayani Kiteto.

 .

Mwenyekiti wa Jukwaa la Wanawake  wilayani Kiteto akiwasilisha mada ya wanawake na maendeleo ya viwanda  wakati wa  maadhimisho ya siku ya wanawake duniani yaliyofanyika katika kijiji cha Mbigiri - kata ya Partimbo  wilayani Kiteto. .

Mshereheshaji  ambaye ni Afisa Maendeleo ya Jamii  Bi.Janeth Kawau  akitekeleza  jukumu  lake  wakati wa maadhimisho ya siku ya wanawake duniani yaliyofanyika katika kijiji cha Mbigiri - kata ya Partimbo  wilayani Kiteto. .



Wananchi wakisikiliza  hotuba ya mgeni rasmi  ambaye ni mkuu wa wilaya  ya Kiteto Mhe. Tumaini Magessa) wakati wa maadhimisho ya siku ya wanawake duniani yaliyofanyika katika kijiji cha Mbigiri - kata ya Partimbo  wilayani Kiteto.




 Vikundi mbalimbali vya wanawake vikitoa burudani mbalimbali  wakati wa maadhimisho ya siku ya wanawake duniani yaliyofanyika katika kijiji cha Mbigiri - kata ya Partimbo  wilayani Kiteto



.....HABARI KAMILI.....


Mkuu wa wilaya ya Kiteto Mheshimiwa Tumaini Magessa amewataka wanawake kutumia fursa zilizopo ndani na nje ya wilaya kujikwamua kiuchumi.Mhe. Magessa ameyasema hayo wakati akihutubia wananchi katika maadhimisho ya siku ya wanawake duniani yaliyofanyika katika kijiji cha Mbigiri - kata ya Partimbo wilayani Kiteto mapema wiki hii.

Mhe. Magessa amesema kwamba kwa sasa fursa za kiuchumi ni nyingi sana na serikali  imekwisha weka mazingira wezeshi  ya wanawake  kujikwamua . Vilevile Mhe. Magessa amewataka wanawake  ambao ni viongozi  kuwasaidia wanawake wenzao ili waweze kuinuka kiuchumi. Akisisitiza kuhusu hilo Mhe. Magessa anasema ‘‘ viongozi wanawake katika maeneo mbalimbali ya kijamii na kiuchumi  watambueni wadau wenzenu  na muone  ni namna gani mtawapa usaidizi wenye tija na endelevu ili kuwainua katika nyanja mbalimbali  na muwasikilize pale wanapohitaji kufanya jambo fulani  la kimaendeleo’’.

Akisoma risala  mbele ya mgeni rasmi ,afisa ustawi wa jamii (W) Kiteto bi Jacline Barongo amesema kwamba katika kipindi cha Januari hadi Novemba 2017 idara ya maendeleo ya jamii wilaya ya Kiteto imepokea malalamiko 157 , malalamiko ambayo yalihusisha kupigwa mke au mume,kutelekeza familia  na kutowapa watoto haki ya kupata elimu.

Naye mratibu wa bima ya afya kwa jamii (ICHF) bi Rufina Haule amewahimiza wanawake kujiunga na ICHF iliyoboreshwa ili wao pamoja na familia zao wawe na afya bora,waweze kufanya shughuli za kiuchumi. Akisisitiza kuhusu umuhimu wa kujiunga na ICHF iliyoboreshwa, bi Haule anasema ‘‘Huwezi ukafanya shughuli yoyote ya kiuchumi kama afya yako ni dhaifu’’ .

Kadhalika bi  Haule amesema kwamba  ICHF imefanya maboresho makubwa , vipengele kadhaa ambavyo vilikuwa kikwazo kwa wanachama katika kupata baadhi ya huduma za matibabu vimeboreshwa.Bi Haule  amevitaja vipengele hivyo ambavyo ni ; Uandaaji na uandikishwaji wanachama.Kupata matibabu , ambapo sasa kwa kutumia kadi ya ICHF mwanachama na wategemezi wake  watapata matibabu katika hospitali ya wilaya na rufaa .Awali  huduma za bima hiyo  zilikuwa ikiishia katika ngazi ya zahanati . Kuongezwa kwa vipimo  kama vile X – Ray, utra sound  na kumuona daktari (Consultation) ,badala ya vipimo vya malaria na homa ya matumbo ( typhoid) tu vilivyokuwa vikilipiwa awali.

Katika hatua nyingine meneja wa benki ya CRDB  tawi  la Kiteto bibi Lucia John amewahamasisha wanawake kuchukua mikopo na kuanzisha viwanda vidogo vidogo ili waweze kuinua uchumi wao,ambapo amewataka  wanawake walio tayari , kufika katika benki ya CRDB tawi la Kiteto lililopo katika mji mdogo wa Kibaya ili kupata mikopo. Sambamba na hayo bibi John amesema kwamba yeye kwa kuwa ni mwanamke atawapa kipaumbele, kwani anataka wanawake wenzake waweze kujikwamua kiuchumi na kuungana na wanaume katika kuimarisha uchumi wa viwanda.

Siku ya wanawake duniani huadhimishwa Machi 8, kila mwaka,ambapo kwa mwaka 2018 maadhamisho ya siku hiyo yamebeba kauli mbiu isemayo ‘‘Kuelekea uchumi wa viwanda, tuimarishe usawa wa kijinsia na uwezeshaji wanawake vijijini’.



....... MWISHO.......







Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA 11.06.2025 June 11, 2025
  • TANGAZO NAFASI YA KAZI- MWENYEKITI BODI YA MFUKO WA ELIMU June 08, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI JUNI 2025 June 07, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 06, 2025
  • Angalia zote

Habari mpya

  • HAYAWI HAYAWI SASA YAMEKUA: HATIMAYE KALOLENI YAPATA SHULE MPYA YA MSINGI

    July 30, 2025
  • SHULE YA MSINGI KINANGALI NAYO YANUFAIKA NA MRADI WA BOOST

    July 30, 2025
  • SERIKALI YA AWAMU YA SITA YAENDELEA KUWEKEZA KWA VITENDO: KURASH YAPATA MRADI MWINGINE WA MILIONI 153 KUPITIA BOOST

    July 30, 2025
  • KATA YA BWAWANI YAPATA MRADI WA SHULE MPYA YA ELIMU MSINGI.

    July 28, 2025
  • Angalia zote

Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.

MWENGE MAKABIDHIANO MKOA WA MANYARA 2018
Video Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Hati ya Mshahara

Viunganishi vya Tovuti Nyingine

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • MANYARA
  • NECTA
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Kibaya-Kiteto

    Anwani ya Posta: P.o.Box 98, Kibaya-Kiteto

    Simu ya Mezani: +255 027-2552099

    Simu ya kiganjani:

    Barua Pepe: ded@kitetodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki@2017 Halimashauri ya Kiteto.Haki zote zimehifadhiwa