• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe watumishi |
    • Malalamiko |
Kiteto District Council
Kiteto District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Teknolojia,Habari ,Mawasiliano na Mahusiano
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Uchimbaji Madini
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Ardhi na Maliasili
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • This page is under construction
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi mipya
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Wataalam wa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto Wapewa Mafunzo ya Mfumo wa Kielektroniki Utakaotumika Kukusanya na Kuhakiki Madeni ya Watumishi Serikalini.

Imetumwa : September 1st, 2020

Mtaalamu Toka OR-Tamisemi Bw. Chance Akifundisha Mfumo Huo Katika Mafunzo Hayo Kwa Vitendo Katika Ukumbi wa Maktaba ya Wilaya ya Kiteto Kama Anavyoonekana Kwenye Picha Hapo Juu.

Wataalamu wa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto Wakiwa Katika Mafunzo Hayo Kwa Vitendo Katika Ukumbi wa Maktaba ya Wilaya ya Kiteto Kama Wanavyoonekana Kwenye Picha Hapo Juu.




------------------------------------     HABARI KAMILI   ------------------------------------ 




Madeni  Management Information System (Madeni MIS) ni mfumo wa kielektroniki wa kitanzania uliotengenezwa na OFISI YA RAIS - TAMISEMI ili kuweza kutumika katika upokeaji wa madeni ya watumishi wa serikali, uhakiki wa madeni hayo na ulipaji wa madeni hayo. Mfumo huu ni rafiki wenye  tija kwa serikali na watumishi kwa ujumla. 

Mfumo huu ili uweze kufanya kazi katika ngazi zote uwezeshwaji wa mafunzo ni muhimu sana ambapo ngazi ya kitaifa tayari walishafanya na sasa ni ngazi ya Wilaya ambapo wataalamu toka OR-TAMISEMI Bw. Chance na Bw. Faustine wamewawezesha wataalamu wa Halmashauri ya wilaya ya kiteto kwa muda wa siku 2 kuanzia tarehe 31.08.2020 hadi 01.09.2020 kwa Mkurugenzi mtendaji wa Wilaya, Maafisa Elimu Msingi na Sekondari, Maafisa Utumishi, Wakaguzi wa ndani, Wahasibu na Maafisa Tehama. Kwa sasa mfumo huu utaanza kwa kada ya elimu msingi na sekondari kwani watumishi wa sekta hii ni sawa na 52% ya watumishi wote wa Tanzania kisha baadaye utatumika kwa watumishi wote wa serikali.

Malengo ya mfumo huu wa kielektroniki ni kutatua changamoto za usimamizi wa uhakika na ufuatiliaji wa malipo ya madai ya watumishi yasiyohusu mishahara ambapo hapo awali rasilimali nyingi sana zilikuwa zinatumika katika kuhakiki kwa usahihi madeni husika, ukosefu wa uwazi na uwajibikaji ambapo matokeo chanya yanayotegemewa ni kupunguza malalamiko ya watumishi, kuongeza moyo wa kufanya kazi na hatimaye kuongeza ufanisi wa shuguli za sekta husika.

Kimsingi mfumo huu utahitaji mtumishi husika kuanzisha madai yake mwenyewe katika kituo chake cha kutolea huduma bila usumbufu wa kusafiri kwenda Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri husika kuwasilisha madai yake kwa kuwa kila atakachokifanya mwalimu mkuu wa shule aliyepo mwalimu atapokea na kuchambua kisha madai haya atayawalisha katika ngazi ya wilaya kwa uchambuzi zaidi na malipo. Katika hatua zote hizi mtumishi mwenye madai husika atakuwa anaona hatua kwa hatua kila kitakachokuwa kinafanyika kwenye mfumo na kwa uwazi zaidi ukiacha madai ya nyuma.

Kwa mfumo huu kila mtumiaji atakuwa na uwezo wa kuona ripoti mbalimbali kulingana na cheo chake, ikiwemo jumla ya waalimu wanaodai, madai na madeni yaliyopo, jumla ya madai na madeni yaliyolipwa na mengineyo.

Mfumo huu tayari umeshaanza kutumika kuanzia tarehe 01.09.2020 katika ngazi ya Halmashauri kwa kuingiza madeni ya nyuma yaliyohakikiwa ambayo yapo kwenye faili la mtumishi husika  kisha kuanzia mwezi  Oktoba 2020, baada ya mafunzo kwa waalimu kukamilika ndipo kila mwalimu ataweza kuingiza madai yake mwenyewe kwa utaratibu maalumu atakaopewa akiwa nyumbani kwake au katika kituo cha kazi au popote pale kwa kutumia simu, kompyuta mpakato, kompyuta na vifaa vingine vya kielektroniki vyenye uwezo wa kufanya kazi kama hizi cha msingi kifaa husika kiwe kimeunganishwa na wavuti "internet" na pia muhusika awe ameshasajiriwa kwenye mfumo huu.

Tunaishukuru sana, serikali ya awamu ya 5 inayoongozwa na Mh. Rais Dkt J.P.Magufuli kwa kuwa sikivu katika kutatua kero za watumishi kwa kutumia teknolojia hii ya mifumo ya kielektroniki ya kompyuta ili kuepusha usumbufu kwa watumishi katika uwazi wa ufuatiliaji wa madai husika, kutembea kwa kutumia fedha nyingi na muda wa kuhudumia wananchi katika maeneo yao utaongezeka.


Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA 11.06.2025 June 11, 2025
  • TANGAZO NAFASI YA KAZI- MWENYEKITI BODI YA MFUKO WA ELIMU June 08, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI JUNI 2025 June 07, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 06, 2025
  • Angalia zote

Habari mpya

  • MAFUNZO YA MFUMO WA E-UTENDAJI KWA WATUMISHI.

    June 12, 2025
  • KIKAO CHA MAANDALIZI YA MWENGE WA UHURU 2025

    June 11, 2025
  • WATOTO WA UMISSETA KITETO, WAWATOA JASHO WATU WAZIMA!

    June 10, 2025
  • WALIMU KITETO WAPEWA MAFUNZO YA AFUA JUMUISHI ZA ELIMU YA AFYA SHULENI

    June 05, 2025
  • Angalia zote

Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.

MWENGE MAKABIDHIANO MKOA WA MANYARA 2018
Video Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Hati ya Mshahara

Viunganishi vya Tovuti Nyingine

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • MANYARA
  • NECTA
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Kibaya-Kiteto

    Anwani ya Posta: P.o.Box 98, Kibaya-Kiteto

    Simu ya Mezani: +255 027-2552099

    Simu ya kiganjani:

    Barua Pepe: ded@kitetodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki@2017 Halimashauri ya Kiteto.Haki zote zimehifadhiwa