• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe watumishi |
    • Malalamiko |
Kiteto District Council
Kiteto District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Teknolojia,Habari ,Mawasiliano na Mahusiano
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Uchimbaji Madini
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Ardhi na Maliasili
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • This page is under construction
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi mipya
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Mamlaka ya Mawasiliano Kanda ya Kaskazini Pamoja na NIDA Waongeza Nguvu Katika Uhamasishaji wa Zoezi la Usajiri wa "LINE" za Simu Wilayani Kiteto.

Imetumwa : October 31st, 2019



Wataalamu Mbalimbali Wakitekeleza Majukumu Yao ya Kuandikisha Wananchi Kisha Kusajiri SIM-CARD zao Hapo Hapo Sehemu ya Chini ya Mti Mjini Kibaya  Kama Inavyoonekana kwenye Picha Hapo Juu.




---------------------------------------------   HABARI KAMILI   ---------------------------------------------


Zoezi la Usajiri wa "LINE" za simu "Subscriber Identification Module CARD - SIM CARD" ni zoezi la kitaifa lililoanza mwezi mei 2019 na litaisha tarehe 31.12.2019 ambapo kwa mtu ambaye hatasajiri kwa muda tajwa hapo juu basi hataweza kutumia sim - card hiyo tena.


Kama ilivyotajwa hapo juu zoezi hili ni la muda maalumu lakini uhamasishaji huu na uandikishaji huu ni kwa kuwafata wananchi katika vituo vya hadhara  kama hiki cha kibaya mjini, ni kwa siku tatu tu kuanzia leo tarehe 31.10.2019 hadi kesho kutwa tarehe 02.11.2019 kwa mujibu wa Bw. Ombeni Mbesele ambaye ni Afisa wa NIDA wa Wilaya ya Kiteto.  Baada ya hapa zoezi hili litaendelea katika vituo vya awali kama kawaida, walengwa wa zoezi hili ni wamiliki wote wa "line" za simu Tanzania wanatakiwa kusajiri "line" zao kwa mujibu wa agizo la serikali kwa mfumo mpana zaidi unaohusisha matumizi ya vidole vya muhusika katika kuweka kumbukumbu za mtumiaji. Lengo  kuu la Serikali ni kuwasaidia wananchi katika masuala mbalimbali ya kiusalama ili kuleta maendeleo yenye tija yanayosukumwa na matumizi ya teknolojia ya mawasiliano ya simu nchini.


Hadi sasa wananchi wengi hutumia simu katika mawasiliano ya sauti, kutumia picha za video na mnato kwa kutumia mitandao ya kijamii pia kutumia pesa mtandao katika kukamilisha miamala mbalimbali kama vile kununua vifurushi vya simu, kununua LUKU, ankara za maji, ving'amuzi, manunuzi ya bidhaa mbalimbali, faini za barabarani, malipo ya Serikali kama vile elimu, ardhi, TRA na zingine nyingi yote haya ni mapinduzi makubwa sana katika tasnia nzima ya mawasiliano yanayopelekea uchumi kukua kutokana na kuongezeka kwa mzunguko wa kifedha mtandaoni kiurahisi muda wowote na popote, ambapo ongezeko kubwa la ajira za kutosha kwa wananchi nchi nzima limeonekana.


Wananchi wa Halmashauri ya Wilaya ya kiteto wamehimizwa kuendelea kusajiri "line" zao kuepuka usumbufu utakaojitokeza baada ya muda wa zoezi hili kuisha.


Hata hivyo wakieleza kwa muda tofauti tofauti wananchi wamefurahishwa na wameishukuru serikali kwa kuwa sikivu kwa kuwafuata maeneo waliyopo ili kukamilisha zoezi hili nyeti.


Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAILI September 01, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU September 01, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI JUNI 2025 June 07, 2025
  • TANGAZO NAFASI YA KAZI- MWENYEKITI BODI YA MFUKO WA ELIMU June 08, 2025
  • Angalia zote

Habari mpya

  • DAS KITETO AWAHIMIZA WANANCHI KUJENGA UTAMADUNI WA UWEKEZAJI.

    September 11, 2025
  • UGONJWA WA HOMA YA INI (HEPATITIS B) NI TISHIO LA MAISHA LAKINI TUMAINI LIPO KUPITIA CHANJO

    September 04, 2025
  • DC MWEMA AFUNGUA RASMI ZAHANATI YA ENGUSERO SIDAN

    August 31, 2025
  • SAFARI YA KM 42 KUFUATA HUDUMA ZA AFYA SASA NI HISTORIA NDIRIGISHI

    August 30, 2025
  • Angalia zote

Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.

MWENGE MAKABIDHIANO MKOA WA MANYARA 2018
Video Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Hati ya Mshahara

Viunganishi vya Tovuti Nyingine

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • MANYARA
  • NECTA
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Kibaya-Kiteto

    Anwani ya Posta: P.o.Box 98, Kibaya-Kiteto

    Simu ya Mezani: +255 027-2552099

    Simu ya kiganjani:

    Barua Pepe: ded@kitetodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki@2017 Halimashauri ya Kiteto.Haki zote zimehifadhiwa