• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe watumishi |
    • Malalamiko |
Kiteto District Council
Kiteto District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Teknolojia,Habari ,Mawasiliano na Mahusiano
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Uchimbaji Madini
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Ardhi na Maliasili
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • This page is under construction
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi mipya
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

MARAFIKI WA DED WAFANYA JAMBO KITETO

Imetumwa : January 31st, 2024

Mkurugenzi Mtendaji  wa Wilaya Kiteto, CPA. Hawa Abdul Hassan kwa niaba ya marafiki zake,  amekabidhi madawati 70  yenye thamani ya shilingi  5,600,000 kwa Mkuu wa Wilaya Kiteto, Mh. Remidius Mwema Emmanuel, kwaajili ya kukabiliana na changamoto ya upungufu wa madawati wilayani hapo.

Akiongea katika hafla  ya makabidhiano ya madawati hayo  iliyofanyika katika Shule ya Msingi Kaloleni Januari 31, 2024, Mkurugenzi huyo alisema kwamba baada ya kuteuliwa na kufika Wilayani Kiteto alikuta kuna mpango mkakati wa kukabiliana na changamoto ya upungufu wa madawati; mpango ambao ulizinduliwa 2.11.2022 na aliyekua Mkuu wa Wilaya Kiteto SSI Mbaraka Alhaji Batenga.

“Huu mkakati  niliupenda na nikaona ni vyema niunge mkono juhudi za Rais Mh. Dkt. Samia Suluhu Hassan pamoja na juhudi za Ofisi ya Mkuu wa Wilaya kwa kuwashirikisha marafiki zangu na kuwaomba wanichangie chochote walichojaliwa ili tuweze kupata madawati kwaajili ya wanafunzi wetu wa Kiteto na hatimaye leo kwa niaba ya marafiki zangu  ninakabidhi madawati haya”.

Aidha Mkurugenzi huyo amewashukuru marafiki zake kwa kumuunga mkono na kuwezesha kupatikana kwa  madawati hayo 70 ambayo yatakaliwa na wanafunzi 210 ambao walikua wanakaa chini wawapo darasani.

Nae Mkuu wa Wilaya ya Kiteto, Mh. Mwema, ambaye ndiye aliyekua Mgeni Rasmi katika hafla ya makabidhiano, aliwashukuru Marafiki wa CPA. Hawa Abdul Hassan kwa mchango wao na alisema kwamba Ofisi ya Mkuu wa Wilaya inathamini mchango wao huo.

Aidha  Mh. Mwema alisema kwamba maana ya kiongozi ni kuongoza njia hivyo alimpongeza Mkurugenzi huyo kwa kuunga mkono mkakati huo na alitoa wito wa viongozi wengine kuiga mfano huo.

Kabla ya kuanza kwa mpango mkakati  huo wa kukabiliana na changamoto ya upungufu wa madawati, Wilaya ya Kiteto ilikua na upungufu wa madawati 9,023 kwa shule za msingi ila kwa sasa wilaya ina upungufu wa madawati 7,702. Hivyo Mh Mwema alitoa wito wa viongozi wengine na wadau mbalimbali kuiga mfano wa Mkurugenzi CPA. Hawa.

“Viongozi wengine wote tuige mfano wa Mkurugenzi . Kila mmoja akitafuta rafiki zake wa kutosha tunaweza kumaliza au kupunguza tatizo hili kwa asilimia kubwa”, alisema Mh. Mwema.

Madawati 70 yaliyotolewa na Marafiki wa CPA. Hawa Abdul Hassan, 50 ni kwaajili ya shule ya Msingi Enguserosidan iliyopo kata ya Laiseri na madawati 20 ni kwa ajili ya Shule ya Msingi Olchaniodo iliyopo kata ya Partimbo.

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA 11.06.2025 June 11, 2025
  • TANGAZO NAFASI YA KAZI- MWENYEKITI BODI YA MFUKO WA ELIMU June 08, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI JUNI 2025 June 07, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 06, 2025
  • Angalia zote

Habari mpya

  • MAFUNZO YA MFUMO WA E-UTENDAJI KWA WATUMISHI.

    June 12, 2025
  • KIKAO CHA MAANDALIZI YA MWENGE WA UHURU 2025

    June 11, 2025
  • WATOTO WA UMISSETA KITETO, WAWATOA JASHO WATU WAZIMA!

    June 10, 2025
  • WALIMU KITETO WAPEWA MAFUNZO YA AFUA JUMUISHI ZA ELIMU YA AFYA SHULENI

    June 05, 2025
  • Angalia zote

Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.

MWENGE MAKABIDHIANO MKOA WA MANYARA 2018
Video Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Hati ya Mshahara

Viunganishi vya Tovuti Nyingine

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • MANYARA
  • NECTA
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Kibaya-Kiteto

    Anwani ya Posta: P.o.Box 98, Kibaya-Kiteto

    Simu ya Mezani: +255 027-2552099

    Simu ya kiganjani:

    Barua Pepe: ded@kitetodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki@2017 Halimashauri ya Kiteto.Haki zote zimehifadhiwa