• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe watumishi |
    • Malalamiko |
Kiteto District Council
Kiteto District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Teknolojia,Habari ,Mawasiliano na Mahusiano
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Uchimbaji Madini
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Ardhi na Maliasili
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • This page is under construction
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi mipya
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

TANZANIA YA TATU AFRIKA MPANGO RASMI WA KUDHIBITI KICHAA CHA MBWA

Imetumwa : September 29th, 2025

Serikali kwa kushirikiana na wadau wa afya ya wanyama imeandaa  Mpango  Rasmi wa kutokomeza Ugonjwa wa Kichaa cha Mbwa ikiwa ni moja ya mkakati wa kufikia azma ya Dunia ya kuondokana kabisa na ugonjwa huo ifikapo mwaka 2030.


Hayo yamebainishwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Bi Agnes Meena katika kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Kichaa cha Mbwa Kitaifa yaliyofanyika leo Septemba 29, 2025 Wilaya ya Kiteto Mkoani Manyara.


Bi. Meena amesema kwamba mpango huo ambao umeshapitiwa na kuridhiwa na Shirika la Afya ya Wanyama duniani (WOAH) unalenga utaratibu wa uchanji wa mbwa na paka wote nchini kwa muda wa miaka mitano.


“Kupitia mpango huo, ni imani yetu kwamba hadi kufikia mwaka 2030 Tanzania itakua ni miongoni mwa nchi zitakazokuwa zimeutokomeza ugonjwa huu wa Kichaa cha Mbwa”,amesema Bi Meena.


Vilevile amesema kuwa mbwa, paka na wanyama wengine  wakitunzwa vizuri wana  umuhimu katika maisha ya kila siku ya binadamu huku akiongeza wasipopewa chanjo ya magonjwa hususani kichaa cha mbwa wanyama hao wanageuka kuwa hatari kwa binadamu. 


“Kwa hiyo lengo la maadhimisho haya ambayo yamesababisha tukusanyike hapa leo ni kukumbushana na kuelimishana zaidi jinsi ya kukabiliana na janga hili la ugonjwa wa kichaa cha mbwa”, amesema Bi Meena.


Kwa upande wake Mkurugenzi wa Huduma za Wanyama wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Dkt. Benezeth Lutege amebainisha kuwa takwimu zinaonesha  katika maadhimisho wilayani hapa mpaka kufikia  Septemba 29, 2025 wametoa chanjo kwa Mbwa 3653, Paka 212, Kuhasi Mbwa 96, Paka 5 na Kufunga Vizazi  Mbwa 52, Paka 26. 


Akisoma taarifa ya Wilaya, kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya, Katibu Tawala wa Wilaya ya Kiteto Bi. Mufandii Msaghaa amesema kwamba wilaya ya Kiteto imejitahidi kuzitekelza sera za serikali kuhusu mifugo hususani kuthibiti magonjwa ya wanyama.


“Serikali imejitahidi kuthibiti magonjwa kwa kutoa kinga ya magonjwa ya wanyama. Kila mwaka wataalam wetu wamekua wakitoa huduma ya chanjo kama sera zinavyotutaka”, amesema Bi. Msaghaa.


Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA MAPOKEZI YA FEDHA SEPTEMBA 2025 September 16, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU September 01, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI September 01, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI JUNI 2025 June 07, 2025
  • Angalia zote

Habari mpya

  • WAZEE WAHIMIZWA KUJITOKEZA KWA WINGI KUPIGA KURA OKTOBA 29

    October 07, 2025
  • KATIBU MKUU WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI AKABIDHI VIFAA NA CHANJO YA KICHAA CHA MBWA KITETO

    September 29, 2025
  • WITO WA LEO SEPTEMBA 29,2025

    September 29, 2025
  • TANZANIA YA TATU AFRIKA MPANGO RASMI WA KUDHIBITI KICHAA CHA MBWA

    September 29, 2025
  • Angalia zote

Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.

MWENGE MAKABIDHIANO MKOA WA MANYARA 2018
Video Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Hati ya Mshahara

Viunganishi vya Tovuti Nyingine

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • MANYARA
  • NECTA
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Kibaya-Kiteto

    Anwani ya Posta: P.o.Box 98, Kibaya-Kiteto

    Simu ya Mezani: +255 027-2552099

    Simu ya kiganjani:

    Barua Pepe: ded@kitetodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki@2017 Halimashauri ya Kiteto.Haki zote zimehifadhiwa