• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe watumishi |
    • Malalamiko |
Kiteto District Council
Kiteto District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Teknolojia,Habari ,Mawasiliano na Mahusiano
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Uchimbaji Madini
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Ardhi na Maliasili
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • This page is under construction
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi mipya
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Mbunge Awataka Wanakijiji Kujenga Nyumba Bora

Imetumwa : July 8th, 2018

Mbunge wa Kiteto Mhe. Emmanuel Papian akizungumza na wakazi wa pori namba moja katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika eneo hilo mwishoni mwa wiki.

Mwenyekiti wa Kitongoji akifungua Mkutano wa hadhara uliofanyika katika kijiji cha Kimana,  eneo la Pori namba moja mwishoni mwa wiki.

Katibu wa CCM(W) Ndg Shekue Pashua akiwasalimia wakazi wa pori namba moja katika Mkutano wa hadhara  uliofanyika katika kijiji cha Kimana,  eneo la Pori namba moja mwishoni mwa wiki.


Afisa mipango (W) ya Kiteto bibi Beatrice Lumbeli akiwasalimia wakazi wa pori namba moja katika Mkutano wa hadhara  uliofanyika katika kijiji cha Kimana,  eneo la Pori namba moja mwishoni mwa wiki.


Wakazi wa Pori namba moja wakiwa wamekusanyika  kumsikiliza Mbunge wao Mhe. Emanuel Papian katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika eneo la pori namba moja mwishoni mwa wiki.

Wakazi wa Pori namba moja wakiwa wakiwasilisha kero  kwa Mbunge wao Mhe. Emanuel Papian katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika eneo la pori moja mwishoni mwa wiki.



..............HABARI KAMILI.............



Mbunge wa Kiteto Mheshimiwa Emanuel Papian amewataka wakazi wa Kijiji cha Kimana, Kitongoji cha Nabirikunya eno maarufu kama pori namba moja kujenga nyumba bora. Mhe Papian  ameyasema hayo wakati akizungumza na wakazi hao katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika katika eneo hilo mwishoni mwa wiki.


Akizungumza katika mkutano huo Mheshimiwa Papian amesema kwamba wakazi wa eneo hilo wanatakiwa kujenga nyumba bora, na  si hivyo tu, bali  wanapokuwa wakijenga wazingatie  mpangilio unaotakiwa ili kuruhusu huduma nyingine  kama vile zima moto na umeme kuweza kufika katika mitaa yote ya eneo hilo kwa urahisi.Akisitiza kuhusu ujenzi wa makazi bora Mhe. Papian amesema“ Tunataka hapa papangike, nyumba bora zijengwe, ili umeme uweze kuletwa hapa, mfanye shughuli za maendeleo,Nyumba za nyasi hapana.Mmeletwa hapa mkae usawa wa barabara. Eneo hili ni la kudumu, jengeni makazi bora ,fanyeni shughuli za maendeleo na muishi kwa amani. Mkishajipanga vizuri ,mkajenga makazi bora, yaliyopangwa vizuri tutawaletea huduma zote muhimu hapa”


Katika hatua nyingine Mhe. Papian ameweka mkazo katika suala la elimu, ambapo amewataka wakazi wa eneo hilo kutokubali kukaa na watoto majumbani ,bila kuwapeleka shule,kwani kufanya hivyo ni kuwanyima haki yao ya msingi ya kupata elimu. Akisisitiza kuhusu hilo Mhe. Papian anasema”Sasa hivi kuna mavuno, mwenyekiti wa kitongoji, changeni, mjenge madarasa, mkifikisha madarasa matatu ,nendeni kwa Mkurugenzi ombeni shule isajiliwe, ikishasajiliwa mimi  pamoja na  serikali tutaongeza nguvu kujenga madarasa mengine, eneo hili kitakuwa na shule”.


Katika mkutano huo wananchi wamewasilisha kero mbalimbali,ambapo Mhe. Papian ametoa majibu kuhusiana na kero hizo na kuahidi kuzifanyia kazi ili ziweze kupatiwa ufumbuzi ndani ya muda mfupi, sambamba na hayo Mhe. Papian ametoa rai kwa wananchi hao kuishi kwa kuheshimiana na kwa upendo ili amani iendelee kutawala katika eneo hilo.


Mhe. Papian yuko katika ziara ya kukagua miradi ya maendeleo na kuzungumza na wananchi katika vijiji mbalimbali jimboni mwake. Ziara hiyo inafanyika kwa muda wa siku saba,ambapo katika siku ya kwanza ya ziara yake hiyo, miongoni mwa vijiji alivyovitembelea ni kijiji cha Kimana,kitongoji cha Nabirikunya, eneo la pori namba moja.



..........MWISHO............

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA 11.06.2025 June 11, 2025
  • TANGAZO NAFASI YA KAZI- MWENYEKITI BODI YA MFUKO WA ELIMU June 08, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI JUNI 2025 June 07, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 06, 2025
  • Angalia zote

Habari mpya

  • HAYAWI HAYAWI SASA YAMEKUA: HATIMAYE KALOLENI YAPATA SHULE MPYA YA MSINGI

    July 30, 2025
  • SHULE YA MSINGI KINANGALI NAYO YANUFAIKA NA MRADI WA BOOST

    July 30, 2025
  • SERIKALI YA AWAMU YA SITA YAENDELEA KUWEKEZA KWA VITENDO: KURASH YAPATA MRADI MWINGINE WA MILIONI 153 KUPITIA BOOST

    July 30, 2025
  • KATA YA BWAWANI YAPATA MRADI WA SHULE MPYA YA ELIMU MSINGI.

    July 28, 2025
  • Angalia zote

Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.

MWENGE MAKABIDHIANO MKOA WA MANYARA 2018
Video Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Hati ya Mshahara

Viunganishi vya Tovuti Nyingine

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • MANYARA
  • NECTA
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Kibaya-Kiteto

    Anwani ya Posta: P.o.Box 98, Kibaya-Kiteto

    Simu ya Mezani: +255 027-2552099

    Simu ya kiganjani:

    Barua Pepe: ded@kitetodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki@2017 Halimashauri ya Kiteto.Haki zote zimehifadhiwa