• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe watumishi |
    • Malalamiko |
Kiteto District Council
Kiteto District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Teknolojia,Habari ,Mawasiliano na Mahusiano
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Uchimbaji Madini
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Ardhi na Maliasili
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • This page is under construction
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi mipya
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Mbunge Papian kuchangia ujenzi wa shule Lerug

Imetumwa : August 14th, 2018

Mbunge wa jimbo la Kiteto Mhe. Emmanuel Papian akizungumza kwenye mkutano wa hadhara katika kijiji cha Lerug wilayani Kiteto ,ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kukagua shughuli za maendeleo  ya jimbo lake.


Mbunge wa jimbo la Kiteto Mhe. Emmanuel Papian ,uongozi  wa CCM wilaya ya Kiteto, viongozi wa kata na kijiji pamoja na wazee wa mila wakikagua vyumba vya madarasa vilivyojengwa kwa ajili ya shule ya msingi ya kijiji cha Lerug.

Mbunge wa jimbo la Kiteto Mhe. Emmanuel Papian ,uongozi  wa CCM wilaya ya Kiteto, viongozi wa kata, viongozi wa kijiji  na wazee wa mila wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kukagua ujenzi wa vyumba vya madarasa.

Wanakijiji wa Lerug wakiwa wamekusanyika kumsikiliza mbunge wao katika mkutano wa hadhara.


Wanakijiji wa Lerug wakiwasilisha kero kwa mbunge wao katika mkutano wa hadhara.




....... HABARI KAMILI.......




Mbunge wa jimbo la Kiteto Mhe. Emmanuel Papian ameahidi kuchangia ujenzi wa madarasa kwa ajili ya  shule ya msingi katika kijiji cha Lerug.Mhe. Papian ametoa ahadi hiyo katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika kijiji cha Lerug  wakati wa ziara yake kijijini hapo .


Akizungumza  katika mkutano huo Mhe. Papian amesema kwamba aliahidi shilingi millioni moja kwa ajili ya ujenzi wa madarasa, lakini  anaongeza shilingi 500,000, iwe 1,500,000, na kwamba atanunua saruji ya kiasi hicho cha fedha,na kuiwasilisha  kijijini hapo ili kuendeleza kazi ya ujenzi. Aidha Mhe. Papian amewahimiza wanakijiji wa Lerug  kuendelea kuchangia ujenzi ,Mhe. Papian  amesema “ Kwenye ile harambee sikuweza kuja, lakini nilituma mwakilishi. Ninyi mmefanya kazi kubwa sana mpaka hapa madarasa yalipofika,tunawapongeza sana, lakini msiishie hapo. Endeleeni kushikamana kuchangia  mpaka idadi ya majengo yanayotakiwa  itakapokamilika”.


Kadhalika Mhe. Papian ameahidi kushughulikia tatizo la maji, tatizo ambalo ndio kero kubwa kwa wanakijiji,ili kuhakikisha kwamba maji yanapatikana katika kijiji hicho sambamba na kushughulikia ubovu wa barabara, ambapo amesema kwamba atazungumza na watu wa TARURA,ili barabara kubwa inayoingia  kijijini hapo iweze kutengenezwa.


Vilevile Mhe. Mbunge amemuagiza Mtendaji wa kijiji  hicho kuhakikisha kwamba wanakijiji wote wanapimiwa maeneo ili waweze kujenga nyumba bora za kuishi pamoja  na vyoo, na katika upimaji huo kusiwe na ubaguzi wa aina yoyote.Pia ametoa rai kwa wafugaji wa kuacha  tabia ya kuingiza mifugo katika mashamba ya wakulima,badala yake wao pamoja na wakulima waishi kwa upendo na maelewano, wawe na utaratibu wa kusubiri mazao yatolewe shambani, baada ya mazao kutolewa wafanye makubaliano ya kupeana mabua ili kudumisha amani kati yao na kutowasababishia wakulima hasara.


Mpaka sasa, wanakijiji wa Lerug wameweza kujenga madarasa manne na ofisi moja ,madarasa mawili na ofisi yakiwa yameshapauliwa na mawili yakiwa katika hatua ya lenta. Majengo hayo  yote yamejengwa kwa nguvu za wananchi.






...........MWISHO............

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA 11.06.2025 June 11, 2025
  • TANGAZO NAFASI YA KAZI- MWENYEKITI BODI YA MFUKO WA ELIMU June 08, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI JUNI 2025 June 07, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 06, 2025
  • Angalia zote

Habari mpya

  • MAFUNZO YA MFUMO WA E-UTENDAJI KWA WATUMISHI.

    June 12, 2025
  • KIKAO CHA MAANDALIZI YA MWENGE WA UHURU 2025

    June 11, 2025
  • WATOTO WA UMISSETA KITETO, WAWATOA JASHO WATU WAZIMA!

    June 10, 2025
  • WALIMU KITETO WAPEWA MAFUNZO YA AFUA JUMUISHI ZA ELIMU YA AFYA SHULENI

    June 05, 2025
  • Angalia zote

Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.

MWENGE MAKABIDHIANO MKOA WA MANYARA 2018
Video Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Hati ya Mshahara

Viunganishi vya Tovuti Nyingine

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • MANYARA
  • NECTA
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Kibaya-Kiteto

    Anwani ya Posta: P.o.Box 98, Kibaya-Kiteto

    Simu ya Mezani: +255 027-2552099

    Simu ya kiganjani:

    Barua Pepe: ded@kitetodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki@2017 Halimashauri ya Kiteto.Haki zote zimehifadhiwa