• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe watumishi |
    • Malalamiko |
Kiteto District Council
Kiteto District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Teknolojia,Habari ,Mawasiliano na Mahusiano
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Uchimbaji Madini
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Ardhi na Maliasili
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • This page is under construction
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi mipya
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Mbunge Ahimiza Amani na Maendeleo Ngapapa

Imetumwa : August 16th, 2018

Mbunge wa jimbo la Kiteto Mhe. Emmanuel Papian akizungumza na wanakijiji wa Ngapapa katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika kijiji hicho ikiwa ni sehemu ya ziara yake kukagua shughuli za maendeleo na kusikiliza kero za wapiga kura wake.

Diwani wa kata ya Kijungu Mhe. Mandaro Mussa akizungumza katika mkutano huo. 

Mtendaji wa kijiji cha Ngapapa Ndg. Gerald M. Dani akitambulisha uongozi wa serikali ya Kijiji  chake katika mkutano huo .



Wakazi wa kijiji cha Ngapapa wakiwa wamekusanyika katika mkutano huo kumsikiliza Mhe. Mbunge .


Wakazi wa kijiji cha Ngapapa wakiwasilisha kero zao kwa Mhe. Mbunge.


............... HABARI KAMILI................


Mbunge wa jimbo la Kiteto Mhe .Emmanuel Papian amewataka wakazi wa kijiji cha Ngapapa ,kata ya Kijungu wilaya ya Kiteto kuishi kwa amani na ushirikiano.Badala ya  kuendeleza chuki na ubaguzi miongoni mwao.Mhe . Papian  ameyasema hayo katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika kijiji hicho.

Akizungumza katika mkutano huo Mhe. Papian amesema “ hatutaki kusikia mtu amelisha mifugo kwenye shamba la mwenzake. “kuchungia mifugo kwenye mashamba , wakati mazao bado yako shambani kunasababisha hasara kwa wakulima,na kujenga chuki kati ya wakulima na wafugaji.Tunataka amani na maendeleo, hatutaki chuki, hatutaki ubaguzi,msiendekeze suala la kubaguana, ni baya sana kwa sababu ,mnapanda mbegu ambayo mavuno yake ni uharibifu na laana.Kila binadamu anastahili kuheshimiwa na kutokubaguliwa”.

Kadhalika Mhe Papian amewaasa wakazi wa kijiji hicho ambao wanaendekeza tabia ya ulevi ,kuacha tabia hiyo, badala yake, wajikite zaidi katika shughuli za kuzalisha kipato ili waweze kujenga nyumba bora,wajiendeleze kimaisha na kuchangie miradi ya maendeleo katika kijiji chao, ili kijiji hicho kiwe na maendeleo.

Katika mkutano huo pia  wanakijiji  wa Ngapapa wamewasilisha kero zao kwa Mhe. Papian, kero namba moja ikiwa ni ukosefu wa chanzo cha maji,ambapo wamesema kwamba  tatizo la maji ni kero kubwa sana kwao.Kero nyingine  ni baadhi ya wakazi wa kijiji hicho ni kutokuwa na makazi baada ya makazi yao  kuvunjwa,kwa  madai ya makazi hayo kujengwa eneo lisiloruhusiwa.

Akijibu kuhusu kero ya maji Mhe. Papian amesema kuwa amesikia tatizo hilo , katika bajeti ijayo watafanya utaratibu ili kijiji hicho kiweze kupata walau kisima kimoja wakati  mipango mingine ya kutafuta vyanzo vingine vya maji katika eneo hilo  ikiwa inaendelea.Vilevile Mhe. Papian  ameahidi kuzungumza na shirika lisilo la Kiserikali la KINAPA  ili katika miradi yao ya kuchimba visima vya maji kwa ajili ya kusaidia vijiji waangalie uwezekano wa kuchimba kisima katika kijiji cha Lerug au Ngapapa, eneo hilo liwe  na chanzo cha maji, na  serikali itakapochimba kisima kingine ,viwepo visima viwili,  maji yapatikane  kwa watu wote.

Kuhusu kero ya baadhi ya wakazi wa kijiji hicho kutokuwa na  makazi baada ya makazi yao kuvunjwa Mhe Papian ametoa maelekezo kwa afisa Mtendaji wa kijiji hicho ndugu Gerald M. Dani ,Mhe. Papian amesema “Moja wapo ya mambo ambayo lazima yafanyike , ni kufanya takwimu, kujua idadi ya watu ambao hawana viwanja, ambao ni wakazi wa kijiji hiki.Mtendaji fanya takwimu ya hawa waliokuwepo,na mpango wa matumizi bora ya ardhi wa hapa uujue, serikali ya kijiji mkae, mpange, watu wote wapate viwanja, mahali pamoja na bila ubaguzi kwamba huyu ni nani na yule ni nani, wajenge, ili iwe rahisi kuleta huduma.Eneo la makazi liwe ni hapa, waende mashambani wakalime ,warudi hapa.Waende machungani wakachunge mifugo yao, warudi hapa, ili huduma zote tulete hapa,kijiji hiki kiweze kuendelea”.

Mhe Papian amezuru katika kijiji cha Ngapapa  ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kukagua shughuli za maendeleo ya jimbo lake, sambamba na kusikiliza kero za wananchi wa jimbo lake kwa lengo la kuzitafutia ufumbuzi.



..............MWISHO..............

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA 11.06.2025 June 11, 2025
  • TANGAZO NAFASI YA KAZI- MWENYEKITI BODI YA MFUKO WA ELIMU June 08, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI JUNI 2025 June 07, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 06, 2025
  • Angalia zote

Habari mpya

  • MAFUNZO YA MFUMO WA E-UTENDAJI KWA WATUMISHI.

    June 12, 2025
  • KIKAO CHA MAANDALIZI YA MWENGE WA UHURU 2025

    June 11, 2025
  • WATOTO WA UMISSETA KITETO, WAWATOA JASHO WATU WAZIMA!

    June 10, 2025
  • WALIMU KITETO WAPEWA MAFUNZO YA AFUA JUMUISHI ZA ELIMU YA AFYA SHULENI

    June 05, 2025
  • Angalia zote

Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.

MWENGE MAKABIDHIANO MKOA WA MANYARA 2018
Video Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Hati ya Mshahara

Viunganishi vya Tovuti Nyingine

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • MANYARA
  • NECTA
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Kibaya-Kiteto

    Anwani ya Posta: P.o.Box 98, Kibaya-Kiteto

    Simu ya Mezani: +255 027-2552099

    Simu ya kiganjani:

    Barua Pepe: ded@kitetodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki@2017 Halimashauri ya Kiteto.Haki zote zimehifadhiwa