• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe watumishi |
    • Malalamiko |
Kiteto District Council
Kiteto District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Teknolojia,Habari ,Mawasiliano na Mahusiano
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Uchimbaji Madini
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Ardhi na Maliasili
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • This page is under construction
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi mipya
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Mbunge Papian Ahamasisha Uanzishaji wa Kidato cha Tano na Sita Ndedo

Imetumwa : July 23rd, 2018

Mbunge wa jimbo la Kiteto Mhe. Emmanuel Papian akizungumza katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye viwanja vya shule ya msingi Ndedo.wakati alipotembelea shuleni  hapo,ikiwa ni sehemu ya ziara yake kukagua shughuli za maendeleo  jimboni mwake.


Mbunge wa jimbo la Kiteto Mhe. Emmanuel Papian akisaini katika kitabu cha wageni  cha shule ya sekondari Ndedo.

Majengo kwa ajili ya Kituo cha afya Ndedo.


Mbunge wa jimbo la Kiteto Mhe. Emmanuel Papian akikagua ujenzi wa choo katika Kituo cha afya Ndedo.




Mabweni mawili yanayojengwa katika shule ya msingi Ndedo,yakiwa katika hatua ya upauzi.

Mbunge wa jimbo la Kiteto Mhe. Emmanuel Papian akikagua ujenzi wa  mabweni katika shule ya msingi Ndedo.Waliosimama pembeni yake ni katibu wake,diwani wa kata ya Ndedo,kaimu mwenyekiti wa kijiji na Mwalimu Mkuu wa shule ya Msingi Ndedo.




Wakazi wa kijji cha Ndedo wakiwa wamekusanyika kumsikiliza Mbunge wao Mhe Emmanuel Papian, katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye viwanja vya shule ya msingi Ndedo

Wakazi wa kijji cha Ndedo wakiwasilisha kero kwa Mbunge wao Mhe Emmanuel Papian, katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye viwanja vya shule ya msingi Ndedo




...........HABARI KAMILI............


Mbunge wa jimbo la Kiteto Mhe. Emmanuel Papiani amemtaka mkuu wa shule kwa kushirikiana na uongozi wa kata ya ndedo na tarafa  kuhamasisha  wakazi wa kata ya Ndedo  kuchangia ujenzi wa majengo kwa ajili ya kuanzisha  kidato cha tano na cha sita katika shule ya Sekondari Ndedo.Mhe. Papian ameyasema hayo wakati akizungumza na mkuu wa shule ya sekondari ndedo,alipotembelea shuleni hapo katika zira yake aliyoifanya katika kata ya Ndedo mwanzoni mwa mwezi huu .


Akizungumza na mkuu wa shule hiyo mwalimu Nicomed Kwahison Mhe. Papian ameshauri kuandaliwa kwa harambee kubwa kwa ajili ya ujenzi wa madarasa na mabweni, na kwamba harambee hiyo isimamiwe na katibu tarafa, watendaji wa kata na watendaji wa vijiji. Akisisitiza kuhusu hilo Mhe Papian amesema “Andaeni harambee, shirikianeni na katibu tawala na watendaji wote. Kila mtu achangie,wakwenda mnadani kuuza ng’ombe aende, wa kuuza mazao aueze, watu wachangie, na watendaji wote washiriki kukusanya hiyo michango,majengo kwa ajili ya kidato cha tano na sita yajengwe hapa.”


Naye Mwl. Kwahison amemueleza Mhe. Mbunge  kuhusu tatizo la nyumba za walimu katika shule hiyo,ambapo amesema kwamba shule hiyo ina uhaba wa nyumba za walimu , na kwamba walimu wawili wamelazimika kuishi katika ofisi za kata.


Aidha Mhe. Papian  amekagua ujenzi wa mabweni mawili katika shule ya msingi Ndedo, ambapo amepongeza kazi iliyofanyika, amesema kwamba  wameitendea haki fedha iliyotolewa kwa ajili ya ujenzi wa mabweni hayo, sambamba na kumtaka mwalimu mkuu wa shule hiyo pamoja na kamati ya shule kuhakikisha kwamba mabweni hayo yanakamilika kwa wakati ili kupungumza msongamano wa wanafunzi kwenye mabweni sambamba na kuwawezesha wanafunzi wengine ambao wamekosa nafasi ya bweni na wanaishi mbali na shule kupata nafasi  ya kulala katika mabweni hayo.


Katika hatua nyingine  Mhe. Papian amezungumza na wakazi wa Ndedo katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika viwanja vya shule ya msingi Ndedo,ambapo ameahidi kushughulikia ukamilishaji wa kituo cha afya cha Ndedo, ili wakazi wa kata hiyo waweze kupata huduma bora za afya  .Kadhalika Mhe. Papian ameahidi kusimamia kuhakikisha kwamba  mabweni yanayojengwa katika shule ya msingi Ndedo yanakamilika mapema na kuanza kutumika.Sambamba na kuendelea kushughulikia tatizo la maji, il kata ya  Ndedo ipate bwawa  la maji kwa ajili ya wakazi wa eneo hilo  na mifugo yao.


Mhe. Papian pia  amewataka wakazi wa Ndedo kuchangia ujenzi kwa ajili ya kidato cha tano na cha sita katika shule ya sekondari ya Ndedo.Hapa Mhe. Papian anasema” Tunataka kuanzisha kidato cha tano na cha sita hapa, tarafa yetu hii haina “A – Level”, changeni fedha tujenge.Wazee watoe madume,mwenye mbuzi atoe ,mwenye mahindi atoe, mwenye alizeti atoe, mpeleke mnadani muuze kwa ajili ya ujenzi.  Na mimi nitapambana huko  kwa waziri, hela zipatikane tukamilishe ujenzi”.


Katika mkutano huo wakazi wa kijiji cha Ndedo wamewasilisha kero mbalimbali kwa mhe. mbunge .Kero hizo ni ukosefu wa maji,ambapo wananchi hao wametaka kupelekewa huduma ya maji katika kijiji chao .Baadhi ya wakazi wa eneo hilo kutokupewa viwanja kwa ajili ya kujenga makazi pamoja na maeneo ya kilimo , ambapo wakazi hao wametaka kujua kwamba ni lini kero hiyo itatatuliwa.


Kero nyingine ni mgogoro kati ya hifadhi ya Mkungunero na vijiji vinavyopakana na hifadhi hiyo ,ambapo wanakijiji hao wameonyesha kusikitishwa na vitendo vya kikatili wanavyofanyiwa wananchi katika maeneo yao na kumuomba Mhe. Mbunge kulitafutia ufumbuzi wa kudumu suala hilo, ili damu isiendelee kumwagika.Kero nyingine ni kutokuwepo kwa alama za barabarani jambo ambalo wamedai kwamba linahatarisha usalama wa wao, hususani kwa watoto.


Akijibu kuhusu kero hizo Mhe Papian amesema kwamba  migogoro ipo katika maeneo mengi ya wilaya ya Kiteto, na kwamba migogoro hiyo inashughulikiwa kwa awamu, haiwezi kwisha kwa siku moja, lakini wanaendelea kuishughulikia kwa lengo la kuimaliza, na kwamba amekwishaanza kushughulikia mgogoro wa Mkungunero na kwamba ana imani kuwa kwa kushirikiana na viongozi wengine wa wilaya,mkoa na taifa mgogoro huo utamalizwa.


Kuhusu suala maji Mhe. Papian amesema kwamba maji ni miongoni mwa vipaumbele vyake ,na kwamba yeye kwa kushirikiana na viongozi wengine wa wilaya wanapamba kuhakikisha kwamba ifikapo 2020  kata hiyo inakuwa na bwawa la maji.


Kwa upande wa kero ya viwanja na mashamba ,Mhe Papian amemtaka mwenyekiti wa kijiji hicho kwa kushirikiana na Mhe. diwani pamoja na serikali ya kijiji kuhakikisha  kwamba wanamaliza kero hiyo mapema iwezekanavyo  kwa kuwapatia wanakijiji hao maeneo kwa ajili ya makazi na kilimo bila kubagua, bali kwa kuzingatia mpango wa matumizi bora ya ardhi waliyojiwekea katika kijiji chao.



........... MWISHO...............



Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA 11.06.2025 June 11, 2025
  • TANGAZO NAFASI YA KAZI- MWENYEKITI BODI YA MFUKO WA ELIMU June 08, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI JUNI 2025 June 07, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 06, 2025
  • Angalia zote

Habari mpya

  • HAYAWI HAYAWI SASA YAMEKUA: HATIMAYE KALOLENI YAPATA SHULE MPYA YA MSINGI

    July 30, 2025
  • SHULE YA MSINGI KINANGALI NAYO YANUFAIKA NA MRADI WA BOOST

    July 30, 2025
  • SERIKALI YA AWAMU YA SITA YAENDELEA KUWEKEZA KWA VITENDO: KURASH YAPATA MRADI MWINGINE WA MILIONI 153 KUPITIA BOOST

    July 30, 2025
  • KATA YA BWAWANI YAPATA MRADI WA SHULE MPYA YA ELIMU MSINGI.

    July 28, 2025
  • Angalia zote

Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.

MWENGE MAKABIDHIANO MKOA WA MANYARA 2018
Video Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Hati ya Mshahara

Viunganishi vya Tovuti Nyingine

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • MANYARA
  • NECTA
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Kibaya-Kiteto

    Anwani ya Posta: P.o.Box 98, Kibaya-Kiteto

    Simu ya Mezani: +255 027-2552099

    Simu ya kiganjani:

    Barua Pepe: ded@kitetodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki@2017 Halimashauri ya Kiteto.Haki zote zimehifadhiwa