• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe watumishi |
    • Malalamiko |
Kiteto District Council
Kiteto District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Teknolojia,Habari ,Mawasiliano na Mahusiano
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Uchimbaji Madini
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Ardhi na Maliasili
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • This page is under construction
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi mipya
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Mbunge Papian Awataka Wafanyabiashara Kulipa Kodi

Imetumwa : January 6th, 2019

Mbunge wa jimbo la Kiteto Mhe. Emmanuel Papian akizungumza  kabla ya uzinduzi wa zoezi la ugawaji wa vitambulisho kwa wafanyabiashara wadogo.

Mkuu wa wilaya ya Kiteto Mhe. Tumaini Magessa , Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri, Kamati ya ulinzi  na Usalama,Wakuu wa idara za Halmashauri ,watumishi wa Halmashauri pamoja na idara na taasisi mbalimbali wakiwa tayari kwa uzinduzi wa zoezi la ugawaji vitambulisho kwa wafanyabiashara wadogo.

Mbunge wa jimbo la Kiteto Mhe.Emmanuel Papian akiwa amemshika mkono  mfanyabiashara mdogo kama ishara ya kumpongeza ,baada ya mfanyabiashara huyo kupewa kitambulisho.

Wafanyabiashara wakiwa wakiwa wamekusanyika kwa ajili ya  kupata vitambulisho.




.................HABARI KAMILI...............





Mbunge wa Kiteto Mheshimiwa Emmanuel Papian  amewataka wafanyabiasha kulipa kodi ili serikali iweze kuleta maendeleo.Mhe Papian ameyasema hayo wakati wa uzinduzi wa zoezi la ugawaji vitambulisho vilivyotolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mheshimiwa John Pombe Joseph Magufuli kwa wafanyabiashara wadogo.Uzinduzi ambao umefanyika Kibaya mjini, katika eneo lijulikanalo  kama chini ya mti mwishoni mwa wiki.

Akizungumza katika uzinduzi huo Mhe. Papian amewataka wafanyabiashara hao kuwaza kukua ili wafike mahali walipe kodi kama wafanyabiashara wengine.Akisisitiza kuhusu kulipa kodi Mhe. Papian amesema “Sisi tunafurahi kwamba leo watu wanakwenda kupata vitambulisho kwa sababu ni wajasiliamali wadogo,lakini ni matumaini yetu kwamba  baada ya muda mtakuwa muelekee pale TRA mlipe kodi.Rais ametoa vitambulisho, na sisi tunasimamia mtapewa ,tunahitaji wafanyabiashara wa Kiteto wakue na wasonge mbele,walipe kodi tupate maendeleo”.

Mhe Papian pia amesema kwamba maendeleo ambayo serikali imekuwa ikiyafanya yanatokana na kodi,hivyo hakuna namna ambayo mtu anaweza akaishi bila kulipa kodi,kwa sababu kulipa kodi  ni lazima, ili nchi iweze kujiendesha na kutekeleza miradi ya maendeleo.

Aidha Mhe. Papian amewataka wafanyabiashara ambao tayari ni walipa kodi TRA kutochukua vitambulisho hivyo kwa sababu  watavitumia kukwepa kulipa kodi,badala yake , wale waendelea kulipa kodi, kwani vitambulisho hivyo sio kiwango chao,bali ni vya wafanyabiashara wadogo,ambao hawajafikia kiwango cha kulipa kodi TRA.
Sambamba na kuwataka wafanyabiashara kulipa kodi, Mhe. Papian ameishauri Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) wilaya ya Kiteto kuacha kufunga biashara za watu,kwani kwa kufanya hivyo kodi haiwezi kupatikana, bali wawaite wafanyabiashara, wakae nao meza moja wazungumze.Amesema kwamba mazungumzo ni njia bora zaidi itakayosababisha  ukusanyaji wa mapato bila kuathiri upande wowote .

Katika hatua nyingine Mhe Papian amesema kwamba ni vema TRA ishirikiane nae yeye pamoja na viongozi wengine, na wadau wa maendeleo  waliopo wilayani hapa ili wawasaidie kubaini vyanzo vingine vya mapato, kwani viko vyanzo ambavyo wao wanavifahamu ,hivyo kwa kushirikiana nao,vyanzo vipya vinaweza kuwekwa bayana na kusababisha ongezeko katika ukusanyaji mapato.

Zoezi la ugawaji wa vitambulisho hivyo litaendelea katika ofisi ya biashara ya halmashauri, ili wafanyabiashara wote wanaostahili kupata vitambulisho hivyo wapate.



 

.............MWISHO.............

Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAILI September 01, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU September 01, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI JUNI 2025 June 07, 2025
  • TANGAZO NAFASI YA KAZI- MWENYEKITI BODI YA MFUKO WA ELIMU June 08, 2025
  • Angalia zote

Habari mpya

  • DAS KITETO AWAHIMIZA WANANCHI KUJENGA UTAMADUNI WA UWEKEZAJI.

    September 11, 2025
  • UGONJWA WA HOMA YA INI (HEPATITIS B) NI TISHIO LA MAISHA LAKINI TUMAINI LIPO KUPITIA CHANJO

    September 04, 2025
  • DC MWEMA AFUNGUA RASMI ZAHANATI YA ENGUSERO SIDAN

    August 31, 2025
  • SAFARI YA KM 42 KUFUATA HUDUMA ZA AFYA SASA NI HISTORIA NDIRIGISHI

    August 30, 2025
  • Angalia zote

Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.

MWENGE MAKABIDHIANO MKOA WA MANYARA 2018
Video Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Hati ya Mshahara

Viunganishi vya Tovuti Nyingine

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • MANYARA
  • NECTA
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Kibaya-Kiteto

    Anwani ya Posta: P.o.Box 98, Kibaya-Kiteto

    Simu ya Mezani: +255 027-2552099

    Simu ya kiganjani:

    Barua Pepe: ded@kitetodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki@2017 Halimashauri ya Kiteto.Haki zote zimehifadhiwa